Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
  • WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI
  • SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA
  • INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO
  • INEC YAWAPIGA MSASA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA PERAMIHO, SHIWINGA
  • MAHUNDI AONYA VIJANA KUTELEKEZA WAZAZI WAO
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
Habari za Kitaifa

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 26, 2026No Comments5 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Serikali imesema itaendelea kuimarisha malezi ya watoto na utoaji wa mafunzo ya ustawi wa jamii kwa wananchi ili kupunguza changamoto za misongo ya mawazo, migogoro ya kifamilia na matatizo ya kisaikolojia, sambamba na kujenga jamii yenye maadili mema, ustawi imara na uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha ya kila siku.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika Taasisi ya Ustawi wa Jamii Kampasi ya Kisangara wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali inatambua umuhimu wa taasisi hiyo katika kutoa wataalamu na elimu kwa jamii kuhusu malezi, makuzi na maendeleo ya watoto pamoja na ustawi wa familia. Amesema hali hiyo inachangia kujenga jamii yenye utulivu na maendeleo endelevu.

“Serikali inaendelea kuweka mkazo katika eneo la malezi ya watoto na utoaji wa elimu ya ustawi wa jamii kwa wananchi kwa sababu tunaamini kuwa familia imara ndiyo msingi wa jamii imara. Kupitia mafunzo haya tunalenga kupunguza misongo ya mawazo, kuimarisha afya ya akili na kuhakikisha watoto wanalelewa katika mazingira salama na yenye maadili mema.” alisema Mahundi.

Aidha, amesema Wizara itaendelea kushirikiana na Taasisi hiyo pamoja na wadau wengine kuhakikisha elimu hiyo inawafikia wananchi wengi zaidi, kuimarisha uwezo wa wataalamu wa ustawi wa jamii ili watoe huduma bora zinazokidhi mahitaji ya jamii na kusaidia kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika familia na jamii kwa ujumla.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Wilaya ya Mwanga Mpapalike Mfaume amepongeza mchango wa Taasisi hiyo katika kutoa elimu na mafunzo kwa wananchi, akisema hatua hiyo imekuwa na manufaa makubwa katika kuimarisha ustawi wa jamii na kusaidia kupunguza changamoto za kijamii katika wilaya hiyo.

“Tutaendelea kuimarisha ushirikiano wetu na Taasisi ya Ustawi wa Jamii Kampasi ya Kisangara ili kuhakikisha wananchi wetu wanaendelea kupata elimu na huduma za ustawi wa jamii, kwa kuwa tunaamini taasisi hii ni nguzo muhimu katika kusaidia kujenga jamii yenye ustawi, maadili mema na maendeleo endelevu,” alisema Mpapalike

Awali, akisoma taarifa ya Taasisi hiyo Meneja wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii Kampasi ya Kisangara Dkt. Leah Mwaisango amesema chuo kinaendelea kutoa mafunzo ya ngazi mbalimbali za taaluma ya ustawi wa jamii pamoja na mafunzo maalum kwa jamii, hatua inayolenga kuongeza uelewa wa masuala ya malezi, makuzi ya watoto, ustawi wa familia na huduma za kijamii ili kujenga jamii yenye ustawi na maendeleo.

“Taasisi imeendelea kutekeleza jukumu lake la kutoa mafunzo kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla, lengo likiwa ni kuzalisha wataalamu wenye ujuzi na kuwajengea uwezo wananchi ili waweze kukabiliana na changamoto za kijamii, kuimarisha malezi ya watoto na kuchangia maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla,” alisema Dkt. Leah.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuimarisha taasisi zake na kuhakikisha zinaendelea kutoa mchango mkubwa katika kukuza ustawi wa jamii, malezi bora ya watoto na afya ya akili, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata elimu na huduma zinazowawezesha kuishi maisha yenye ustawi na tija.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA

February 24, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025356

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Habari za Kitaifa

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

By Mbeya YetuFebruary 26, 20265

Serikali imesema itaendelea kuimarisha malezi ya watoto na utoaji wa mafunzo ya ustawi wa jamii…

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025356

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.