MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini (CCM), Mhe. Patrick Mwalunenge amekutana na viongozi wa vyama vya upinzani kwa ajili ya kujadili masuala ya kisiasa mkoani Mbeya na maendeleo ya wananchi wa mkoa huo.
Katika kikao hicho kimefanyika leo Machi 5,2026 katika ukumbi wa Mkulu ambapo viongozi hao walibadilishana mawazo kuhusu hali ya kisiasa mkoani Mbeya, pamoja na namna bora ya kuimarisha ushirikiano miongoni mwa vyama vya upinzani.
Lengo kuu ni kusukuma mbele ajenda za maendeleo na ustawi wa wananchi.
Akizungumza katika kikao hicho, Mbunge Mwalunenge amesisitiza umuhimu wa viongozi wa vyama vya siasa kuweka mbele maslahi ya wananchi badala ya tofauti za kisiasa.
Amesisitiza kuwa na ushirikiano na mazungumzo ya mara kwa mara ni njia muhimu ya kujenga umoja na kuleta mabadiliko chanya katika jamii,pamoja na kuona umuhumu wao katika katika kulibadilisha Jiji la Mbeya.
Kwa mujibu wa Mwalunenge kuanzia leo anawatambua kama viongozi wa vyama vyenye mawazo mbadala kwa ajili ya ustawi wa Jiji la Mbeya na Taifa kwa ujumla.
Aidha,kikao hicho pia kililenga kuona namna ya kumsaidia Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mkoa wa Mbeya, Hamadi Mbeyale anayembuliwa na maradji ambapo kwa sasa anatibiwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.
Kutokana na kikao hicho, Mbunge Mwalunenge amesema anabeba gharama zote za matibabu za kiongozo huyo wa CHADEMA, ambazo ni Sh.milioni mbili.
Aidha, Mh.Mwalunenge alipendekeza kuundwa kwa chama cha ushirikiano katika shidana raha kwa viongozi hao na kuitwa “CHAMA CHA VIONGOZI WA VYAMA VYENYE MAWAZO MBADALA” ambapo ameahidi kuwachangoa shilingi milioni 20.
Kwa upande wao, baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani waliohudhuria mkutano huo walieleza kuwa mazungumzo kama hayo ni muhimu katika kujenga mshikamano na kuboresha mikakati ya kisiasa, hasa katika kipindi hiki ambacho vyama vinajiandaa na shughuli mbalimbali za kisiasa na kijamii.
Mkutano huo pia ulijadili changamoto zinazowakabili wananchi wa Mkoa wa Mbeya na kusisitiza haja ya viongozi kushirikiana kutafuta suluhisho la kudumu kwa masuala ya maendeleo, ikiwemo miundombinu, huduma za kijamii na fursa za kiuchumi.
Kikao hicho kimeelezwa kuwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha mawasiliano na ushirikiano kati ya viongozi wa vyama vya siasa kwa lengo la kuhakikisha maslahi ya wananchi yanapewa kipaumbele.
Na Mwandishi Wetu,MBEYA

