Author: Mbeya Yetu

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 19 Aprili 2025, amezindua gari la kubebea wagonjwa (ambulance) lililotolewa na Serikali kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Mwakibete, jijini Mbeya. Uzinduzi huo unalenga kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wakati kwa wakazi wa Jiji hilo. Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Tulia amewashukuru Viongozi wa Serikali kwa kuendelea kupeleka huduma muhimu kwa wananchi, huku akiwataka wakazi wa Jiji la Mbeya kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba…

Read More

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imepata tuzo ya pongezi kwa kutambuliwa kwa juhudi zake katika utoaji wa mafunzo katika vituo vya kutolea huduma za afya vya ngazi ya msingi (PHC) Mkoa wa Mbeya kwa mwaka 2024. Tuzo hii imetolewa na Kamati ya Usimamizi wa Huduma za Afya Mkoa (RHMT) ya Mbeya, wakati wa kikaoa kazi cha robo ya mwaka kilichojadili changamoto za vifo vinavyotokana na afya ya uzazi na watoto wachanga kilichofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali. Akikabidhi tuzo hiyo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya na Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Elizabeth Nyema, ameeleza wazi kutambua…

Read More

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 18 Aprili 2025, ameongoza wananchi wa Jiji la Mbeya katika zoezi la upimaji na matibabu ya macho.

Zoezi hilo limeanza rasmi leo katika Shule ya Msingi Kagera, iliyopo Kata ya Ilomba na litadumu kwa siku tatu mfululizo. Huduma hiyo ya afya ya macho inatolewa bila malipo kupitia Taasisi ya Tulia Trust kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya.

Katika hotuba yake, Dkt. Tulia amewasihi wananchi wa Mbeya kujitokeza kwa wingi ili kunufaika na huduma hizo muhimu kwa afya zao, akisisitiza dhamira ya Taasisi ya Tulia Trust katika kuboresha ustawi wa jamii kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.

Read More

Rais Mstsaafu wa Awamu ya Nne na Mjumbe Maalum wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kiongozi wa Burkina Faso Kepteni Ibrahim Traore mjini Ouagadougou na kushuhudiwa na baadhi ya maafisa waandamizi wa nchi zote mbili. Mhe. Kikwete aliwasilisha pia salamu za Rais Samia ambazo zilielezea umuhimu wa nchi za Afrika kuimarisha ushirikiano wa kijamii na kiuchumi kama njia muhimu kwa bara hilo kujitegemea, hususan katika kipindi hiki ambapo misaada kutoka nchi za magharibi imepungua kwa kiasi kikubwa.

Read More