Author: Mbeya Yetu

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Tulia Ackson amesema kwenye Sekta ya kilimo ndani ya Kata ya Iganjo Mgombea Uraisi kwa tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya Kazi Kubwa hasa Kuhakikisha Mbolea za Ruzuku na Pembejeo zote za kilimo hivyo ataendelea kuongeza upatikanaji maradufu wa Ruzuku na Pembejeo za kilimo. Dkt. Tulia amesema anafahamu kwamba ndani ya kata hiyo Kuna kilimo cha umwagiliaji hivyo atahakikisha skimu zote za umwagiliaji zinabireshwa zadisi ili wakulima Wafanye kilimo Bora hivyo ifikapo 29 Oktoba 2025 Wananchi wakapige Kura nyingi kwa CCM ili wakulima wa Jimbo la…

Read More

Zaidi ya wanaume 1000 kutoka katika mji wa Tunduma mkoani Songwe wamefunga Barabara kwa saa kadhaa wakifanya matembezi ya aina yake na kuwaacha watu midomo wazi barabarani wakiadhimisha mwaka mmoja wa muungano wa kikundi chao maalum Cha kijamii chenye lengo la kuinuana na kusaidiana wao kwa wao.

Mwenyekiti wa kikundi hicho Herode Jivava anasema waliamua kuanzia kikundi hicho ili kumkomboa mwanaume na aibu ambazo amekuwa akikumbana nazo pindi linapotokea jambo la furaha ama huzuni hivyo wao wapo kwaajili ya kumuinua na kumrejeshea heshima mwanaume huyo.

Read More

Mbeya, Septemba 28, 2025 – Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikisha operesheni maalum iliyopelekea kuuawa kwa watuhumiwa waliodaiwa kuhusika na utekaji na mauaji ya kikatili ya Shyrose Michael Mabula [21], mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Mzumbe Ndaki ya Mbeya, Kitivo cha Sheria.

Shyrose aliripotiwa kutekwa nyara Septemba 14, 2025 na mwili wake kupatikana Septemba 16 usiku katika Mtaa wa Morovian, Kata ya Isyesye Jijini Mbeya ukiwa umechomwa moto. Uchunguzi uliofanywa na Polisi uliwakamata watuhumiwa watatu: Marwa Nyahega John [25], Edward Christopher Kayuni, na Websta William Mwantebele [27], ambao walikiri kupanga njama za kumteka kwa lengo la kujipatia fedha kutoka kwa baba yake, Dkt. Mabula Michael.

Kwa mujibu wa Polisi, baada ya kushindikana kwa mpango huo, walimnywesha sumu ya kuulia magugu aina ya Round Up bila mafanikio, kisha wakamnynonga kwa kamba na kuuchoma moto mwili wake.

Mnamo Septemba 27, 2025, wakati wa operesheni katika Kijiji cha Chalangwa, wilayani Chunya, watuhumiwa Edward na Websta walijaribu kukimbia na kuwashambulia askari kwa kisu. Polisi walifyatua risasi za tahadhari, lakini walipokaidi amri, walijeruhiwa kwa risasi na kufariki dunia wakipelekwa hospitalini. Mtuhumiwa wa tatu, Marwa, naye alifariki baada ya kujirusha kutoka kwenye gari la Polisi wakati akipelekwa kuonyesha vielelezo.

Katika upekuzi, Polisi walipata pingu mbili, vitambulisho feki vya JWTZ, simu zenye picha za utekaji na mawasiliano yao, pamoja na taarifa kwamba kidole na nguo za marehemu vilikuwa vimepelekwa kwa mganga wa jadi kwa ajili ya zindiko. Mganga huyo kwa sasa anatafutwa.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeonya vijana na wananchi kwa ujumla kuacha tamaa ya mali kwa njia za haramu, na kusisitiza kuwa uhalifu haulipi na mkono wa sheria utawafikia popote pale.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mbeya

Read More

Mgombea Udiwani Kata ya Chokaa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya Joshua Mlambalala amefikisha maombi ya minara ya mawasiliano kwa Kijiji cha Mapogolo Kata ya Chokaa mbele ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi Mbunge mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya kutokana na umuhimu mkubwa kibiashara hasa Wachimbaji wa madini ya dhahabu eneo hilo.

Mlambalala amefikisha kilio hicho kwenye kampeni za Urais, Ubunge na Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) zilizofanyika Kata ya Chokaa mgeni rasmi akiwa ni Mhandisi Maryprisca Mahundi.

Akijibu maombi hayo Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema suala hilo lipo ndani ya uwezo wake hivyo anawaagiza wataalam haraka iwezekanavyo ili kuwaondolea kadhia wananchi wa Mapogolo.

Akiomba kura Urais, Ubunge na Udiwani Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan imefanya maendeleo makubwa hivyo kuna kila sababu ya kukipa kura Chama Cha Mapinduzi.

Aidha amesema wananchi wajitokeze kupiga kura kumchagua Masache Kasaka nafasi ya Ubunge na Joshua Mlambalala nafasi ya Udiwani ili kutimiza mafiga matatu kwa maendeleo ya Kata,Wilaya na nchi kwa ujumla.

Uchaguzi mkuu utatamatisha oktoba 29 mwaka huu ambapo Mhandisi Maryprisca Mahundi ameendelea kuomba kura maeneo mbalimbali nchini.

Read More

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi ( CCM) Dkt. Tulia Ackson, ameendelea na Kampeni Zake za Kuomba ridhaa kwa Wananchi wa Jimbo hilo kumchagua kwa kura nyingi kwa nafasi yake ya Ubunge na kura nyingi kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya Urais katika Uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 ili wakaendelee kutatua Changamoto zinazowakabili ikiwemo upatikanaji wa Soko la Kisasa ndani ya Mtaa wa Ituha Kata ya Ilomba. Akizungumza mbele ya Wananchi wa kata ya Ilomba Katika Mitaa wa Ituha leo tarehe 23 Septemba, 2025 , Dkt. Tulia amesema Chama Cha Mapinduzi…

Read More

Mgombea Ubunge Jimbo la Uyole kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Tulia Ackson, leo Septemba 23, 2025 amefanya mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Ndugunya (Isoso) vilivyopo Kata ya Mwasanga, Jijini Mbeya. Katika mkutano huo uliovuta mamia ya wananchi, Dkt. Tulia amenadi sera za Chama Cha Mapinduzi huku akisisitiza mshikamano, mshikikiano na mshirikiano katika utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2025 – 2030. Amewataka wananchi wa Kata ya Mwasanga na Jimbo zima la Uyole kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi ifikapo Oktoba 29, 2025 kushiriki uchaguzi mkuu kwa kuwapigia kura wagombea wote wa CCM kuanzia ngazi ya Udiwani, Ubunge hadi…

Read More