Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet
- Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu
- Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29
- MKONGOMAN ATOA USHUHUDA MZITO KUTOWEKA KWA AMANI NCHINI JAMHURI YA KONGO
- DKT HARRISON MWAKYEMBE ATOA SOMO ZITO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
- DC ITUNDA ATETA NA WANA VICOBA AWAPA NENO HILI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKT 29
- WANANCHI KATA IGANZO MTAA MWAMBENJA WAISHUKURU MBEYA UWSA KWA MRADI WA MAJITAKA
- TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025
Author: Mbeya Yetu
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga. Washiriki wa mafunzo hayo ambayo yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi…
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetoa vibali vya kutoa elimu ya mpiga kura wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa taasisi na asasi za kiraia 164 na kibali cha uangalizi wa uchaguzi kwa taasisi na asasi 76 za ndani ya nchi na 12 za kimataifa. Taarifa ya Tume kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Julai 19,2025 na kusainiwa na mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ndg. Ramadhani Kailima imesema Tume imefikia uamuzi wa kutoa vibali hivyo katika kikao chake kilichokutana Julai 18, mwaka huu.“Kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 10(1) (g) (h)…
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Cyprian Mbugano, akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa Uchaguzi kutoka mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida. Na Mwandishi Wetu, Morogoro TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewataka Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa ,Wasimamizi wa Uchaguzi,Wasimamizi wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maofisa uchaguzi na maofisa ununuzi kutenga sehemu ya muda wao kusoma Katiba, sheria na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume hiyo. Lengo la kusoma Katiba,sheria na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume hiyo ili yawaongoze katika kusimamia vyema…
Na Mwandish wetu, Dar es Salaam. CHAMA cha Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) kimeshukuru uamuzi wa serikali ya kuwapatia mafunzo maalumu ya kunoa weledi na uzalendo wa wanachama wake kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Mabloga zaidi ya 200 wakiwemo wa diaspora walioanzisha Mtandao huo mwaka 2015 watapata mafunzo hayo. “Tumekuwa na mazungumzo na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambao kimsingi ndio wasimamizi wakuu wa maudhui na wametuthibitishia kwamba wapo hatua za mwisho za kutekeleza maagizo ya serikali ya kutoa mafunzo kwa mabloga wote nchini,” alisema Mwenyekiti wa TBN , Beda Msimbe. Akifafanua kuhusu mafunzo hayo, Msimbe alisema kwamba…
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema yeyote anayefanya kazi za kihabari bila kuwa na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) kinachotolewa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB anavunja sheria ya Huduma za Habari. Waziri Kabudi ametoa kauli hiyo huku akionesha Press Card yake kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika leo tarehe 14 Julai, 2025 alipozungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Phillip Mpango jijini Arusha. #ithibatitz #ithibatikidijitali
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema wakati umefika kwa wanahabari wa Kiafrika kuonesha taswira nzuri ya Bara la Afrika kwa kuandika habari chanya zenye nguvu na za kutia moyo kuhusu Bara hili.Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Mkutano wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika unaofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC). Amesema kwa kipindi kirefu Bara la Afrika limekuwa likitegemea simulizi za vyombo vya habari vya nje ambazo zimejikita katika hatari, vita, migogoro, na kushindwa huku vikipuuza uwezo mkubwa, uthabiti, na maendeleo ya watu wa Afrika.Amesisitiza umuhimu wa kuwa…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Julai 15,2025 amefungua mafunzo kwa watendaji wa Uchaguzi mkuu Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku tatu kwenye mikoa mbalimbali nchini kwa siku tatu na yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo. Tume imeyagawa mafunzo hayo kwenye awamu mbili ambapo awamu hii ya kwanza inahusisha watendaji kutoka mikoa ya Morogoro, Singida, Dodoma, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Mjini Magharibi, Geita, Kagera, Mtwara, Lindi, Tabora, Kigoma, Tanga, Kilimanjaro, Ruvuma, Iringa na Njombe. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC,…
