Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet
- Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu
- Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29
- MKONGOMAN ATOA USHUHUDA MZITO KUTOWEKA KWA AMANI NCHINI JAMHURI YA KONGO
- DKT HARRISON MWAKYEMBE ATOA SOMO ZITO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
- DC ITUNDA ATETA NA WANA VICOBA AWAPA NENO HILI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKT 29
- WANANCHI KATA IGANZO MTAA MWAMBENJA WAISHUKURU MBEYA UWSA KWA MRADI WA MAJITAKA
- TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025
Author: Mbeya Yetu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya mjini, Mhe. Dkt Tulia Ackson, kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust ameigusa familia ya Bi. Lusia Kapangala mkazi wa mtaa wa Mwasote kata ya Itezi jijini Mbeya iliyokuwa imekata tamaa ya maisha kutokana na mapito ya kukosa mahitaji muhimu ikiwemo chakula, mavazi na fedha za kusomesha watoto. Dkt. Tulia hayo tarehe 12 Julai, 2025 ambapo amesema pamoja na kuihudumia familia hiyo mahitaji muhimu, pia amechukua jukumu la kuwasomesha watoto wote wa familia hiyo, akiwemo kijana Nature Nenelo…
Na Mwandishi Wetu Serikali imekubali kutoa mafunzo maalum kwa waandishi wa blogu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025, hatua muhimu itakayowajengea uwezo na kuwaandaa kubeba dhamana kubwa ya usambazaji wa habari sahihi. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa katika Mkutamo wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya habari Katika kufanikisha uchaguzi Mkuu 2025. Katika mkutano huo kipindi cha majadiliano Mwenyekiti wa Chama cha Mabloga Tanzania (TBN), Beda Msimbe, aliomba serikali kuona umuhimu wa kufunza mabloga wengi ambao sio waandishi lakini wanatengeneza maudhui kuwa na weledi kuandika masuala ya…
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Ndele Mwaselela, amekutana na waandishi wa habari na kutoa ufafanuzi kuhusu uvumi unaoenea miongoni mwa baadhi ya wanachama wa chama hicho kuwa amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini.
Katika tamko lake kwa vyombo vya habari, Mwaselela amekanusha taarifa hizo na kusisitiza kuwa hana nia ya kugombea ubunge bali anaendelea kujikita kikamilifu katika kulitumikia Chama katika nafasi yake ya uongozi ndani ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi Julai 1,2025 amefungua kambi ya matibabu bila gharama kwa wagonjwa wa macho Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya inayolenga kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili.
Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema gharama zote za uchunguzi,dawa na matibabu ni bure kupitia wadau wake kutoka Ujerumani na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.
Dkt Fariji Kilewa Mkuu wa Kitengo cha macho Hospitali ya Mkoa wa Mbeya amesema lengo ni kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili waliopo Mkoa wa Mbeya na mikoa jirani.
Aidha amesema mbali ya upasuaji wa mtoto wa jicho pia wanawafanyia uchunguzi wa macho kwa matatizo mengine ya macho.
Hata hivyo Dkt Fariji Kilewa amesema gharama za upasuaji wa mtoto wa jicho zinagharimu zaidi ya shilingi laki tatu ambazo ni watu wachache wanaoweza kumudu gharama hizo.
Afisa uhusiano Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Agrey Mwaijande amesema gharama zote zinatolewa bure hivyo wito umetolewa kwa wananchi kuitumia vizuri fursa hiyo.
Baadhi ya wagonjwa waliojitokeza kupatiwa watibabu wamepongeza huduma hiyo kutokana na wengi wao kushindwa kumudu gharama za matibabu ya macho.
Hii ni kambi ya pili kwa Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi kuandaa kambi ya macho iliyoanza juni 30,2025 itakayotamatika julai 5,2025kwa ushirikiano na Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.
Mbeya, Juni 30, 2025 – Mwanasiasa na mpenda maendeleo, Mwakipesile, amerudisha rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini. Hatua yake inaendelea kuonesha ushindani mkali ndani ya chama chake huku akiweka mbele ajenda za ushirikiano na maendeleo jumuishi kwa wananchi wa Mbeya Mjini.
