Author: Mbeya Yetu

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYAUWSA) imefuta madeni ya wateja wa kata ya Mwasenkwa waliokuwa wakitumia mradi wa maji wa kijiji na kushindwa kulipa ankara kwa muda mrefu.

Uamuzi huo umetangazwa wakati wa uzinduzi wa mradi mpya wa kisima kirefu chenye uwezo wa kuzalisha lita 720,000 za maji kwa siku, utakaohudumia wakazi zaidi ya 2,800. Mradi huu unaleta huduma ya maji kwa masaa 24.

Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson, alizindua mradi huo na kuhimiza wananchi kupanda miti rafiki kwa vyanzo vya maji ili kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka.

Read More

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 19 Aprili 2025, amezindua gari la kubebea wagonjwa (ambulance) lililotolewa na Serikali kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Mwakibete, jijini Mbeya. Uzinduzi huo unalenga kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wakati kwa wakazi wa Jiji hilo. Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Tulia amewashukuru Viongozi wa Serikali kwa kuendelea kupeleka huduma muhimu kwa wananchi, huku akiwataka wakazi wa Jiji la Mbeya kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba…

Read More

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imepata tuzo ya pongezi kwa kutambuliwa kwa juhudi zake katika utoaji wa mafunzo katika vituo vya kutolea huduma za afya vya ngazi ya msingi (PHC) Mkoa wa Mbeya kwa mwaka 2024. Tuzo hii imetolewa na Kamati ya Usimamizi wa Huduma za Afya Mkoa (RHMT) ya Mbeya, wakati wa kikaoa kazi cha robo ya mwaka kilichojadili changamoto za vifo vinavyotokana na afya ya uzazi na watoto wachanga kilichofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali. Akikabidhi tuzo hiyo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya na Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Elizabeth Nyema, ameeleza wazi kutambua…

Read More