Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- HIKI NDICHO ALICHOKISEMA BAHATI NDINGO ALIPOKUWA AKIREJESHA FOMU KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MBARALI
- Mwanamke miaka 50 aoana na kijana wa miaka 21 baada ya penzi lao kuvutia kijiji kizima kwa mshangao
- KAILIMA AFUNGA KIKAO CHA UPANGAJI WA RATIBA YA KAMPENI ZA WAGOMBEA URAIS
- Pastor akimbia baada ya mke wake kuvamia madhabahu akilia
- MAHUNDI Atamka Hadharani: Samia na Tulia Ushindi wa Kishindo 2025
- Jinsi ya Kumkamata Mpenzi Wako Akiwa na Mpango wa Kando Bila Stress
- Masache Kasaka achukua fomu ya Ubunge Lupa Chunya aingia site kibabe
- MAHUNDI: CHAMA CHA MAPINDUZI NA MPEPERUSHA BENDERA MWALUNENGE NDIYO HABARI YA MBEYA MJINI
Author: Mbeya Yetu
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Vyama vya Siasa kuhusu uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika leo Julai 27, 2025 jijini Dodoma na kushirikisha vyama vyote vyenye usajili kamili. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Vyama vya Siasa kuhusu uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume,…
WANAFUNZI WATANO WAMEFARIKI DUNIA BAADA YA KUGONGWA NA GARI MBEYA.
Tarehe 26.07.2025 saa 11:30 alfajiri huko Kijiji cha Itumba kilichopo Kata ya Chalangwa, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya Chunya katika barabara kuu ya Mbeya – Chunya. Gari lenye namba za usajili T.194 DCE aina ya Yutong Bus kampuni ya Safina Coach lililokuwa likitokea Chunya mjini kuelekea Mbeya likiendeshwa na dereva aitwaye Abdul Hassan [28] mkazi wa Mbeya mjini liliwagonga watembea kwa miguu wanafunzi wa Shule ya Sekondari Chalangwa waliokuwa wanakimbia mchaka mchaka (Jogging) na kusababisha vifo vya watu watano.
Waliofariki katika ajali hiyo wametambulika kwa majina ya Seleman Ernest @ msekwa, Samwel Zambi, Kelvin Festo Mwasamba, Hosea Manga Mbwilo na Amina Ndege Ulaya. Aidha, katika ajali hiyo majeruhi ni tisa kati yao saba wamelazwa wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Chunya na Kituo cha Afya Chalangwa ambao ni Benard Mashaka [17], Lilian Raymond [16], Kenedy Masoud [14], Vicent Baraka Malema [17], Siwema Nasibi Simbilo [17], Alex Aules Peter [17], Dethani Adam Charles [15] na wawili ambao wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa ambao ni Getruda Mwakyoma [17], Farida Mwasongole [17].
Chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva kushindwa kulimudu gari hivyo kupelekea kwenda kuwagonga wanafunzi waliokuwa wanafanya mazoezi ya kukimbia (Jogging). Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na msako wa kumtafuta dereva wa Basi hilo ambaye amekimbia mara baada ya kusababisha ajali.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea kutoa wito kwa madereva kuwa makini na kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.
Imetolewa na:
Kaimu Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.
Iramba – Singida Imeelezwa kuwa kukamilika kwa daraja la Masagi linalojengwa katika barabara ya Kibirigi-Masagi kutasaidia kuunganisha vijiji vya Kibirigi, Masagi na Tyeme katika Kata ya Mtoa, Wilaya ya Iramba mkoani Singida. Hayo yameelezwa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Singida Mhandisi Ibrahim Kibasa wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mradi huo mbele ya Kamati ya Ukaguzi ya TARURA inayofanya ziara ya Ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa Miundombinu ya barabara mkoani humo. “Vijiji vya Kibirigi, Masagi na Tyeme vinajishughulisha na shughuli za kilimo hususani pamba, alizeti, dengu, mahindi pamoja na ufugaji, hivyo kukosekana kwa daraja katika Mto sekenke linapojengwa…
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb), amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji kushirikiana na mkandarasi anayetekeleza mradi wa maji wa chanzo cha Mto Kiwira kuweka makubaliano maalum na kiwanda kinachotengeneza mabomba yatakayotumika katika zaidi ya kilomita 30 za mradi huo, ili kuhakikisha mabomba yote yanatengenezwa kwa wakati mmoja. Mhe. Aweso ametoa maelekezo hayo leo alipofanya ziara kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo, ambapo alieleza kuridhishwa na kazi kubwa iliyofanyika chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYAUWSA). Hata hivyo, alieleza kuwa changamoto kubwa iliyobainika ni ucheleweshaji wa ulazaji wa mabomba kutoka kwenye…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 23, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga kuanzia Julai 21 hadi 23 mwaka huu. (Picha na INEC). Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 23, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga kuanzia Julai 21 hadi…