Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO

July 1, 2025

MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI

June 30, 2025

Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH

June 30, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO
  • MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI
  • Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH
  • MKULIMA NA MFUGAJI WA MBARALI ATIA TIMU KIPUTE JIMBO LA MBARALI USANGU ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE
  • WAKILI MSOMI KAPTENI MSTAAFU SAMBWEE SHITAMBALA ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI.
  • MWAISUMBE: ALIYEJITOSA UBUNGE 2010 AWANIA TENA MBEYA MJINI AAHIDI KUMUUNGA MKONO ATAKAYETEULIWA
  • MHASIBU SUA AJITOSA UBUNGE JIMBO LA SAME MASHARIKI
  • MWANAHABARI MKONGWE CHARLES MWAKIPESILE AJITOSA UBUNGE MBEYA MJINI
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home ยป TIMU YA MADAKTARI NA WAUGUZI KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA, TANZANIA WAMETEMBELEA UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NCHINI ZAMBIA, TAREHE 12 MEI, 2025
Habari za Kitaifa

TIMU YA MADAKTARI NA WAUGUZI KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA, TANZANIA WAMETEMBELEA UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NCHINI ZAMBIA, TAREHE 12 MEI, 2025

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 12, 2025No Comments14 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Lusaka, Zambia โ€“ Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe. Lt Gen Mathew Edward Mkingule, amekutana na kufanya mazungumzo na timu ya wataalamu kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, waliofika Ubalozini leo tarehe 12 Mei, 2025 asubuhi kwa ajili ya kujitambulisha. Wataalamu hao wapo nchini Zambia kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu na wataalamu wa Hospitali ya Kufundishia ya Zambia (University Teaching Hospital – UTH) kuhusu huduma ya uchujaji wa damu kwa njia tumbo (Peritoneal Dialysis).

Katika mazungumzo yake na ujumbe huo Mhe. Balozi Lt Gen Mathew Edward Mkingule aliwakaribisha wataalamu hao waliobeba bendera ya Tanzania, akisema kuwa ni fursa muhimu kwa nchi yetu kushiriki katika kubadilishana utaalamu wenye lengo la kuboresha huduma za afya Barani Afrika. Pia, ameshukuru na kupongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi mahiri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hasan kutokana na mageuzi makubwa yaliyofanyika katika sekta ya afya nchini Tanzania.

“Nawashukuru mmekuja hapa Zambia na mmeona wenyewe na mtafanya ulinganifu, tunayo haki ya kupongeza Serikali ya Tanzania kwa maboresho makubwa katika sekta ya afya yenye nia ya kutoa huduma bora na za kibobezi kwa wananchi wetu pamoja na mataifa jirani. Hii imeifanya Tanzania kuwa kimbilio la nchi nyingi za ukanda wa SADC zinazohitaji huduma za kibingwa na bobezi, hususan katika masuala ya uchujaji wa damu na huduma za magonjwa sugu,” alisema Mhe. Balozi Lt Gen Mkingule.

Ameongeza kuwa, “Huduma hizi zimeboreshwa sana, ikiwa ni pamoja na kuanzisha vituo maalum vya huduma za afya kuanzia ngazi ya Vituo vya Afya, Zahanati, Hospitali kwa kuimarisha miundombuni ya kutolea huduma za afya, ununuzi na ufungaji wa vifaa tiba vya kisasa, pamoja na kuwajengea wataalamu uwezo wa ndani na wa kimataifa. Hii inatoa mwanga wa matumaini kwa wananchi wa Tanzania na jirani zao.” โ€“ Mhe. Balozi Lt Gen Mkingule.

Kwa upande wake, Kiongozi wa timu hiyo ya wataalamu kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya , Dkt. Octaben Kasanga, Daktari Bingwa wa Afya na Magonjwa ya figo, amemshukuru Mhe. Balozi Lt Gen Mkingule kwa ushirikiano na mapokezi mazuri waliyopatiwa kutoka kwake na Maafisa wa Ubalozi. Timu hiyo ya wataalamu kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya wameahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha huduma za tiba na sekta ya afya kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania.

“Tunashukuru sana Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Wizara ya Afya, Ubalozi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuwezesha kushiriki mafunzo haya muhimu katika Hospitali ya Taifa ya Zambia. Lengo letu ni kujifunza zaidi kuhusu teknolojia na mbinu bora za uchujaji wa damu kwa njia tumbo, ili tuweze kuboresha huduma zetu nyumbani Tanzania,” amesema Dkt. Kasanga.

Amesema kuwa hii ni hatua nyingine muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya afya, ambapo Tanzania inaendelea kuonesha njia ya kuwaweka wananchi wake na nchi jirani katika mstari wa mbele wa huduma bora za kibingwa.

Ziara hii ya mafunzo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia WIzara ya Afya na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kuhakikisha inawaendeleza Watumishi wa Seta ya Afya ndani na nje ya nchi ili waweze kutoa huduma za afya zenye viwango vya kimataifa, na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za afya katika ukanda wa SADC.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MHASIBU SUA AJITOSA UBUNGE JIMBO LA SAME MASHARIKI

June 28, 2025

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MAGEREZA NA VYUO VYA MAFUNZO WANOLEWA

June 22, 2025

VIJANA CCM MBEYA DC WAJIPANGA KUPIGA KURA OKTOBA 2025.

June 13, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024173

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202482

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202568

DKT. TULIA ATOA MSAADA WA VIPAZA SAUTI MSIKITI WA MASJID BI FATMA NZOVWE JIJINI MBEYA

March 29, 202459
Don't Miss
Video Mpya

KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO

By Mbeya YetuJuly 1, 20250

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi Julai 1,2025 amefungua kambi ya matibabu bila gharama kwa wagonjwa wa macho Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya inayolenga kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili.

Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema gharama zote za uchunguzi,dawa na matibabu ni bure kupitia wadau wake kutoka Ujerumani na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Dkt Fariji Kilewa Mkuu wa Kitengo cha macho Hospitali ya Mkoa wa Mbeya amesema lengo ni kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili waliopo Mkoa wa Mbeya na mikoa jirani.

Aidha amesema mbali ya upasuaji wa mtoto wa jicho pia wanawafanyia uchunguzi wa macho kwa matatizo mengine ya macho.

Hata hivyo Dkt Fariji Kilewa amesema gharama za upasuaji wa mtoto wa jicho zinagharimu zaidi ya shilingi laki tatu ambazo ni watu wachache wanaoweza kumudu gharama hizo.

Afisa uhusiano Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Agrey Mwaijande amesema gharama zote zinatolewa bure hivyo wito umetolewa kwa wananchi kuitumia vizuri fursa hiyo.

Baadhi ya wagonjwa waliojitokeza kupatiwa watibabu wamepongeza huduma hiyo kutokana na wengi wao kushindwa kumudu gharama za matibabu ya macho.

Hii ni kambi ya pili kwa Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi kuandaa kambi ya macho iliyoanza juni 30,2025 itakayotamatika julai 5,2025kwa ushirikiano na Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.

MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI

June 30, 2025

Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH

June 30, 2025

MKULIMA NA MFUGAJI WA MBARALI ATIA TIMU KIPUTE JIMBO LA MBARALI USANGU ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE

June 30, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO

July 1, 2025

MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI

June 30, 2025

Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH

June 30, 2025
Most Popular

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024173

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202482

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202568
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.