Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
  • WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI
  • SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA
  • INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO
  • INEC YAWAPIGA MSASA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA PERAMIHO, SHIWINGA
  • MAHUNDI AONYA VIJANA KUTELEKEZA WAZAZI WAO
  • NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATEMBELEA MAKAZI YA WAZEE, ASISITIZA UPENDO NA MATUNZO KWAKUWA WAZEE NI TUNU YA TAIFA.
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MAPATO MANISPAA YA MOSHI “YAPAA” KUTOKA BILIONI 6.1 HADI BILIONI 9.9
Habari za Kitaifa

MAPATO MANISPAA YA MOSHI “YAPAA” KUTOKA BILIONI 6.1 HADI BILIONI 9.9

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 17, 20251 Comment4 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo akitangaza ongezeko la mapato ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi .
Mkurugenzi wa Hlamshauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akizungumza wakati wa baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi .
Baadhi ya Wakuu wa Divisheni na watendaji katika ofisi za Halmashauri ya Manipaa ya Moshi wakifuatilia kikao cha Bajeti cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo.

Baadhi ya Madiwa wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakichangia mjdala wa Bajeti ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakati wa kikao cha Bajeti .

 Na Dixon Hussein – Moshi  

Manispaa ya Moshi imepiga hatua kubwa
katika ukusanyaji wa mapato ya ndani, ikiongeza mapato kutoka bilioni 6.1 mwaka
2021 hadi bilioni 9.9 mwaka 2025, ongezeko la takribani bilioni 3.7.

Mafanikio haya yanatajwa kuwa matokeo ya mikakati madhubuti
iliyowekwa ili kuboresha vyanzo vya mapato na kuongeza uwajibikaji katika
usimamizi wa rasilimali za umma.

Akizungumza katika kikao cha bajeti cha mwaka wa fedha
2025/26, Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo amesema kuwa ongezeko hilo
limechangiwa na mbinu mpya za ukusanyaji wa mapato pamoja na uwekezaji katika
miradi yenye tija.

“Tumeimarisha mifumo yetu ya ukusanyaji wa mapato kwa
kutumia teknolojia ya kisasa, tumeongeza uwazi katika makusanyo, na pia
tumewekeza katika miradi inayozalisha kipato kwa manispaa. Hatua hizi
zimechangia ongezeko kubwa la mapato,” alisema Zuberi Kidumo .

Alisema miongoni mwa mikakati iliyochangia ongezeko la
mapato ni matumizi ya Mfumo wa Kidigitali katika Ukusanyaji wa Mapato na kwamba
mifumo hiyo imepunguza upotevu wa mapato
na kuongeza uwazi.

“Mfumo huu umesaidia kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato
yanayotokana na malipo ya moja kwa moja bila kufuata taratibu sahihi” alisema
Kidumo

Akiwasilisha hoja kwa wajumbe wa baraza la Halmashauri ya Manispaa
ya Moshi Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo Mwajuma Nasombe amesema ofisi
yake kwa sasa imewekeza kwenye miradi mitatu ya kimkakatai .

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na ni ujenzi wa vibanda
vingi vya biashara katika eneo la Uhuru Park ,Ujenzi wa bustani na kumbi za nje
kwa ajili ya sherehe kwa maharusi pamoja na ukarabati mkubwa wa uwanja wa
michezo wa Majengo .

Mkurugenzi Nasombe anasema Manispaa imeanzisha mfumo wa
ukaguzi wa mara kwa mara kuhakikisha kuwa mapato yanayokusanywa yanafika kwenye
mfuko wa manispaa bila upotevu huku usimamizi mzuri wa rasilimali na
uwajibikaji wa watendaji umeimarishwa ili kuhakikisha kila senti inayokusanywa
inatumika kwa maendeleo ya wananchi.

Aidha ameeleza kuwa kumekuwa na ushirikiano mzuri na  na taasisi mbalimbali za maendeleo,
wafanyabiashara, na mashirika ya kimataifa katika kutafuta njia bora za
kuongeza mapato na kuwekeza katika miradi mipya.

Mafanikio haya yameifanya Manispaa ya Moshi kuwa mfano wa
kuigwa katika usimamizi wa fedha za umma, huku kukiwa na matumaini makubwa kuwa
mapato yataendelea kuongezeka.

Hata hivyo, changamoto kama ukwepaji wa kodi na uhaba wa
baadhi ya miundombinu bado zinahitaji suluhisho la haraka.

Baadhi ya wananchi wamesifu juhudi za manispaa lakini
wakatoa wito wa uwazi zaidi katika matumizi ya mapato hayo.

“Tunafurahia kuona mapato yanaongezeka, lakini
tunahitaji kuona miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa kasi ili wananchi waone
matunda ya mapato haya,” alisema mkazi mmoja wa Moshi”.alisema Idrisa Mombo
mkazi wa manispaa ya Moshi

Kwa ongezeko hili la mapato, Manispaa ya Moshi inaonekana
kuwa na dira thabiti ya maendeleo. Swali linalosalia ni je, mapato haya
yataweza kuendelea kuongezeka kwa miaka ijayo na kubadili kabisa taswira ya
kiuchumi ya manispaa?

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA

February 24, 2026

1 Comment

  1. 🔗 + 1.518878 BTC.GET - https://graph.org/Binance-04-15?hs=00df76676ae787764fc48c7ceff27b5a& 🔗 on April 22, 2025 3:27 pm

    nk0pl2

    Reply

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025355

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Video Mpya

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

By Mbeya YetuFebruary 25, 20262

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa kushirikiana na NHIF Mkoa wa Mbeya wamekutana na kundi la watu wenye ulemavu mkoani Mbeya kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bima ya Afya kwa wote.

Akifungua kikao hicho Februari 25, 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo Dkt. Godlove Mbwanji alisema lengo ni kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata uelewa wa bima hiyo, kwani ni miongoni mwa makundi maalumu yaliyopewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Sita katika utekelezaji wa sheria ya Bima ya Afya kwa wote.

Msimamizi wa NHIF mkoa wa Mbeya, Bw. Nicolaus Mwangomo, alieleza kuwa washiriki walipatiwa elimu kuhusu utaratibu wa uchangiaji, faida na dhana ya bima hiyo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya Bima ya Afya kwa wote.

Kwa niaba ya washiriki, Bi. Rebecca Ramadhani alishukuru kwa elimu hiyo akisema itasaidia watu wenye ulemavu kukabiliana na changamoto za matibabu na kuboresha upatikanaji wa huduma za afya.

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA

February 24, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025355

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.