Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji

February 9, 2026

Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo

February 8, 2026

TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya

February 8, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji
  • Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo
  • TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya
  • New Asante Mbeya Yapongeza TAKUKURU Mbeya kwa Elimu ya Uadilifu na Kufungua Uelewa wa Wanachama
  • Utengule Usangu Yapata Jezi, Majiko ya Gesi na Msaada wa Kijamii Kutoka kwa Mbunge Ndingo
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Aga Khan Zaanzisha Ushirikiano wa Kuboresha Huduma za Afya
  • Shule ya Sekondari Utengule Usangu, H
  • Mradi wa Barabara Mlima Nyoka Wamfikisha MCC ASAS, Ataka Kero za Wananchi Zitokomee
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MAPATO MANISPAA YA MOSHI “YAPAA” KUTOKA BILIONI 6.1 HADI BILIONI 9.9
Habari za Kitaifa

MAPATO MANISPAA YA MOSHI “YAPAA” KUTOKA BILIONI 6.1 HADI BILIONI 9.9

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 17, 20251 Comment3 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo akitangaza ongezeko la mapato ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi .
Mkurugenzi wa Hlamshauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akizungumza wakati wa baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi .
Baadhi ya Wakuu wa Divisheni na watendaji katika ofisi za Halmashauri ya Manipaa ya Moshi wakifuatilia kikao cha Bajeti cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo.

Baadhi ya Madiwa wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakichangia mjdala wa Bajeti ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakati wa kikao cha Bajeti .

 Na Dixon Hussein – Moshi  

Manispaa ya Moshi imepiga hatua kubwa
katika ukusanyaji wa mapato ya ndani, ikiongeza mapato kutoka bilioni 6.1 mwaka
2021 hadi bilioni 9.9 mwaka 2025, ongezeko la takribani bilioni 3.7.

Mafanikio haya yanatajwa kuwa matokeo ya mikakati madhubuti
iliyowekwa ili kuboresha vyanzo vya mapato na kuongeza uwajibikaji katika
usimamizi wa rasilimali za umma.

Akizungumza katika kikao cha bajeti cha mwaka wa fedha
2025/26, Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo amesema kuwa ongezeko hilo
limechangiwa na mbinu mpya za ukusanyaji wa mapato pamoja na uwekezaji katika
miradi yenye tija.

“Tumeimarisha mifumo yetu ya ukusanyaji wa mapato kwa
kutumia teknolojia ya kisasa, tumeongeza uwazi katika makusanyo, na pia
tumewekeza katika miradi inayozalisha kipato kwa manispaa. Hatua hizi
zimechangia ongezeko kubwa la mapato,” alisema Zuberi Kidumo .

Alisema miongoni mwa mikakati iliyochangia ongezeko la
mapato ni matumizi ya Mfumo wa Kidigitali katika Ukusanyaji wa Mapato na kwamba
mifumo hiyo imepunguza upotevu wa mapato
na kuongeza uwazi.

“Mfumo huu umesaidia kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato
yanayotokana na malipo ya moja kwa moja bila kufuata taratibu sahihi” alisema
Kidumo

Akiwasilisha hoja kwa wajumbe wa baraza la Halmashauri ya Manispaa
ya Moshi Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo Mwajuma Nasombe amesema ofisi
yake kwa sasa imewekeza kwenye miradi mitatu ya kimkakatai .

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na ni ujenzi wa vibanda
vingi vya biashara katika eneo la Uhuru Park ,Ujenzi wa bustani na kumbi za nje
kwa ajili ya sherehe kwa maharusi pamoja na ukarabati mkubwa wa uwanja wa
michezo wa Majengo .

Mkurugenzi Nasombe anasema Manispaa imeanzisha mfumo wa
ukaguzi wa mara kwa mara kuhakikisha kuwa mapato yanayokusanywa yanafika kwenye
mfuko wa manispaa bila upotevu huku usimamizi mzuri wa rasilimali na
uwajibikaji wa watendaji umeimarishwa ili kuhakikisha kila senti inayokusanywa
inatumika kwa maendeleo ya wananchi.

Aidha ameeleza kuwa kumekuwa na ushirikiano mzuri na  na taasisi mbalimbali za maendeleo,
wafanyabiashara, na mashirika ya kimataifa katika kutafuta njia bora za
kuongeza mapato na kuwekeza katika miradi mipya.

Mafanikio haya yameifanya Manispaa ya Moshi kuwa mfano wa
kuigwa katika usimamizi wa fedha za umma, huku kukiwa na matumaini makubwa kuwa
mapato yataendelea kuongezeka.

Hata hivyo, changamoto kama ukwepaji wa kodi na uhaba wa
baadhi ya miundombinu bado zinahitaji suluhisho la haraka.

Baadhi ya wananchi wamesifu juhudi za manispaa lakini
wakatoa wito wa uwazi zaidi katika matumizi ya mapato hayo.

“Tunafurahia kuona mapato yanaongezeka, lakini
tunahitaji kuona miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa kasi ili wananchi waone
matunda ya mapato haya,” alisema mkazi mmoja wa Moshi”.alisema Idrisa Mombo
mkazi wa manispaa ya Moshi

Kwa ongezeko hili la mapato, Manispaa ya Moshi inaonekana
kuwa na dira thabiti ya maendeleo. Swali linalosalia ni je, mapato haya
yataweza kuendelea kuongezeka kwa miaka ijayo na kubadili kabisa taswira ya
kiuchumi ya manispaa?

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA

February 4, 2026

TGNP na CARE Watoa Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabia Nchi kwa Jamii Mbeya

January 31, 2026

JUMUIYA YA WAZAZI CCM YAFUNGUA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 KWA MATEMBEZI YA AMANI – MBEYA MJINI

January 30, 2026

1 Comment

  1. 🔗 + 1.518878 BTC.GET - https://graph.org/Binance-04-15?hs=00df76676ae787764fc48c7ceff27b5a& 🔗 on April 22, 2025 3:27 pm

    nk0pl2

    Reply

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025334

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024226

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025139
Don't Miss
Video Mpya

Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji

By Mbeya YetuFebruary 9, 20260

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Mohamed Fakii, ametoa onyo dhidi ya uharibifu wa vyanzo vya maji unaotokana na ukataji miti ovyo na kilimo karibu na vyanzo vya maji.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa Chanzo cha Maji cha Mbawe, kijiji cha Mbawe, Fakii alisema kuwa shughuli za kibinadamu zinaendelea kuhatarisha uendelevu wa vyanzo vya maji licha ya kuwepo kwa maji kwa sasa kutokana na mvua. Alisisitiza kuwa ni marufuku kufanya shughuli zozote ndani ya mita 60 kutoka chanzo cha maji.

Aliwaagiza wananchi wote wanaolima au kufanya shughuli karibu na vyanzo hivyo kuondoka mara moja, huku akizitaka serikali za vijiji na kata kushirikiana kikamilifu katika ulinzi wa vyanzo vya maji na kutoa elimu kwa wananchi.

Ziara hiyo ilifanywa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mheshimiwa Solomon Itunda, akiwa ameambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya.

Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo

February 8, 2026

TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya

February 8, 2026

New Asante Mbeya Yapongeza TAKUKURU Mbeya kwa Elimu ya Uadilifu na Kufungua Uelewa wa Wanachama

February 8, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji

February 9, 2026

Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo

February 8, 2026

TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya

February 8, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025334

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024226
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.