Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Bi. Erica Yegella, Atoa Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita Siku 100
- TAASISI ZA PICTERUS AS NA GOAL 3 KUANZISHA TEKNOLOJIA YA KISASA YA KUPIMA MANJANO KWA WATOTO WACHANGA TANZANIA
- MAHUNDI: SERIKALI YAELEZA SABABU ZA KUTOWALAZIMISHA WATOTO KUWAHUDUMIA WAZAZI.
- WAZEE WASHIRIKIANA NA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZOEZI LA UPANDAJI MITI DODOMA.
- Wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Waadhimisha Kuzaliwa Rais Samia kwa Mshikamano
- MADAKTARI BINGWA WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA MKOANI MANYARA
- Serikali Yakabidhi Vifaa vya Kujifunzia kwa Wanafunzi Wenye Mahitaji Maalum Nsalala
- Nilipata Miscarriage Mara Tano Hadi Nikapoteza Ndoto Zangu Za Kuwa Mama Mpaka Nilipopata Usaidizi Usio na Madhara

