Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- KOCHA MEXIME AAHIDI KUREJESHA FURAHA KWA MASHABIKI MBEYA CITY FC, KUSHUSHA ”VIFAA” DIRISHA DOGO
- *DKT. MWIGULU AMBANA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KITAI-RUANDA*
- MBEYA UWSA YAONGEZA UFANISI, NAIBU WAZIRI WA MAJI AZINDUA MAGARI YA KISASA
- Kila mwanamke mzuri alimuacha kabla ya kupata msaada huu
- Naibu Waziri wa Maji Mathew: Aweka Mkazo Kwenye Miradi ya Maji Mbeya na Chunya
- Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira
- WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI
- MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA

