Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- DKT. TULIA: NITAHAKIKISHA JIMBO JIPYA LA UYOLE LINAPATA HALMASHAURI
- MAFANIKIO YA MARYS PRIMARY SCHOOL MBEYA YAVUTIA WAZAZI NA WANAFUNZI,154 WAHITIMU DARASA LA 7, 2025
- Timida Fyandomo: Sauti ya Dkt. Tulia Bungeni ni sauti ya wana uyole
- Masache Kasaka: Wana Jimbo la Uyole Msifanye Makosa, 29/10 Chagueni Dkt. Tulia na Dkt. Samia
- Kauli ya Mahundi Uyole: Umoja wa Wanawake na Wanaume Ni Nguvu ya Kura kwa Tulia na Samia
- Bahati Ndingo: Dkt. Tulia Ni Mtu wa Kazi, Wanajimbo la Uyole Chagueni Tulia na Samia
- Mwalunenge Awanadi Dkt. Tulia na Dkt. Samia Jimbo la Uyole Uzinduzi wa Kampeni
- Suma Fyandomo Awahimiza Wananchi Jimbo la Uyole Kuwachagua kwac kura nyingi Dkt. Tulia na Dkt Samia