Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- WANANCHI HAI, FUONI , KATA TANO KUPIGA KURA KUCHAGUA WABUNGE NA MADIWANI KESHO
- Mume Wangu Alikuwa Akipoteza Udhibiti Usiku na Kukojoa Kitandani Hatua Moja Ilinirejesha Amani Nyumbani
- Dadangu Aliokota Mchanga Wa Nyayo Zangu Baada Ya Kuenda Kijijini Na Gari Mpya Lakini Maelezo Maalum Yaliniokoa Katika Hofu
- Mhe. Mahundi: Wazee ni Tunu ya Taifa, Wastahili Kulindwa na Kuheshimiwa
- NDELE MWASELELA AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUZINGATIA MAADILI, KUANDIKA HABARI ZA MAENDELEO NA KUWASEMEA WANANCHI
- Sikuweza Kulala Usiku Juu Ya Ndoto Mbaya Lakini Sasa Nalala Kama Mtoto Baada Ya Kupata Suluhisho
- Nilihisi Kuna Kitu Kinazuia Maendeleo Yangu—Baada ya Kufunguliwa, Mambo Yalisonga
- Baada ya miaka minane ya chuki familia yetu ilipata amani ndani ya siku nne tu

