Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- Ndoa Yangu Ilikuwa Karibu Kuvunjika Lakini Siri Hii ya Mwisho Iliokoa Mapenzi Yetu
- Walidhani Ni Bahati Tu Lakini Ukweli Uliofichuka Ulishangaza Kila Mtu
- NAIBU WAZIRI MAHUNDI AWASIHI WANAFUNZI TENGERU, KUTUMIA ELIMU KUTATUA CHANGAMOTO ZA JAMII
- Aliiba Kila Siku Bila Kuonekana Siku Moja Hatua Moja Ilimrudisha Mwenyewe Akiwa Ametikisika
- Nilianza Kudhoofika Bila Sababu Nilipogundua Nilikuwa Nachawiwa, Njia Hii Ilinilinda Milele
- Vibaka Wamvamia Mwandishi Rashid Mkwinda wa Mbeya Yetu Ajeruhiwa Vibaya Kichwani na Kulazwa
- Boss Amtesa Mfanyikazi Bila Kujua Ndiye Mke Anayetakiwa Kumuoa, Yaliyojiri Ni Haya
- Mama Wa Kambo Apata Usaidizi Wa Kudumu Baada Ya Kupata Mateso Kutoka Kwa Mabinti Wakorofi

