Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- PART-2: MTANZANIA AISHIYE ULAYA AELEZEA KAZI NA MAISHA YAKE UGHAIBUNI AENDELEZA UANDISHI WA VITABU
- Kijana Songwe Amwaga Ujumbe Mzito: “Viongozi Msimfiche Ukweli Rais Samia”
- DKT. MWIGULU: TANZANIA NI MALI YETU SOTE, SI MALI YA SERIKALI WALA CHAMA CHA SIASA
- Tiba kwa wanawake wanaokosa hamu ya tendo la ndoa
- Waziri Mkuu Ajibu Maswali Mazito Toka kwa Wahariri wa Vyombo vya Habari
- WAZIRI NANAUKA ATAKA VIJANA WASIKILIZWE
- Je, unatafuta kazi kwa muda mrefu fanya hivi
- Waziri Mkuu aagiza Kanisa la Ufufuo na Uzima kufunguliwa

