Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- MALKIA WA NGUVU WALIOSHINDA TUZO KANDA NYANDA ZA JUU KUSINI WATOA USHUHUDA WAO
- WIMBO WA WANAFUNZI SEKONDARI YA IWIJI WAMGUSA RC HOMERA , ATOA MAJIBU PAPO KWA HAPO
- MBEYA EXPORT TRADING: TAWA NA JITIHADA ZA KUENDELEZA HISTORIA YA MJI WA KILWA KUWA URITHI WA DUNIA
- MBEYA EXPORT TRADING: WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TFS YAJA NA HUDUMA UDUNGISHAJI NYUKI KUTIBU MARADHI
- RC HOMERA AWAPA ”KIBANO” WATENDAJI MBEYA DC AWAPA SIKU 7 KUKAMILISHA MARUMARU SEKONDARI YA IWIJI
- Waziri Aweso: Miradi Ya Maji Yapiga Hatua, Sasa Tuimarishe Huduma na Udhibiti wa Upotevu wa Maji
- RC HOMERA AAGIZA MIL 200 ZIELEKEZWE KITUO CHA AFYA IYUNGA MAPIDUZI MBEYA DC
- RC HOMERA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SEKONDARI WANAFUZI WA MAHITAJI MAALUMU UTENGULE USONGWE