Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya.
Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.
“Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau wengine ni msingi wa mafanikio yetu katika kutatua changamoto za kiafya zinazowakabili watoto.” – Bi. Naima Mkingule, Kiongozi wa Msafara.
Mkingule ameeleza kuwa msaada huo wa vifaa tiba na dawa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Wizara ya Afya katika kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya maeneo mbalimbali nchini, hususan kwa watoto, ambao wanahitaji huduma za matibabu ili kuweza kupona magonjwa yanayoathiri maisha yao.
Trending
- KONGAMANO MAFUNDI MBEYA. DC MALISSA AWEKA BAYANA ”UAMINIFU WA MAFUNDI SIRI YA KUWA FUNDI SMART”
- FUNDI SMART YAWA MKOMBOZI KWA MAFUNDI NCHINI 7000 WAJISAJILI KWENYE MFUMO MKOANI WA MBEYA
- KUUNDWA KWA JAB NI HATUA YA KUIMARISHA NA KUBORESHA SEKTA YA HABARI – MAJALIWA
- SPIKA DKT. TULIA ACKSON AFUNGUA KONGAMANO LA WASOMI WA AFRIKA UDSM
- JK ASHIRIKI KUTOA MAFUNZO CHUO KIKUU CHA HAVARD HUKO BOSTON KWA MAWAZIRI WA NCHI ZINAZOENDELEA
- SERIKALI ITAFANYIA KAZI HARAKA MAAZIMIO YA KONGAMANO LA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI- MSIGWA.
- MH. MAHUNDI AKARIBISHWA NA MABANGO JOJO
- MH. MAHUNDI Atembelea Banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA)Atoa Msaada kwa Maendeleo ya Wananchi