Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025

MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”

October 27, 2025

“Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo

October 27, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu
  • MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”
  • “Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo
  • Nilivyomfanya Mtu Aliyenidharau Kuniheshimu na Kunitegemea Kwa Mambo Mengi
  • NABII MPANJI AUTANGAZIA UMMA, WAKRISTO WASISHIRIKI MAANDAMANO WAJITOKEZE KWA WINGI KUPIGA KURA
  • Nilivyookoa Biashara Yangu Baada ya Wateja Wote Kupotea Ghafla
  • DED Yegella: Ahamasisha Upigaji Kura, Kamanda Kuzaga Asema Jeshi la Polisi Lipo Tayari Kulinda Amani
  • RC Malisa Atoa Wito wa Kulipa Leseni Wakati Akikabidhi Madawati 1,000 kwa Shule 15 Jijini Mbeya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » RAIS SAMIA NA RAIS MSTAAFU KIKWETE WAPONGEZWA KWA KUFANIKISHA USHINDI WA PROFESA JANABI KATIKA UCHAGUZI WA MKURUGENZI WA WHO KANDA YA AFRIKA
Habari za Kitaifa

RAIS SAMIA NA RAIS MSTAAFU KIKWETE WAPONGEZWA KWA KUFANIKISHA USHINDI WA PROFESA JANABI KATIKA UCHAGUZI WA MKURUGENZI WA WHO KANDA YA AFRIKA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 19, 2025Updated:May 19, 2025No Comments5 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Na Mwandishi `Maalumu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongezwa kwa maono yake ya mbali na uamuzi wa busara wa kumpendekeza Profesa Mohamed Yakub Janabi kugombea nafasi ya Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO).

Wananchi mbalimbali waliohojiwa wametaja hatua hiyo ya Rais Samia kama ishara ya kujiamini kama taifa, na uthibitisho kuwa Watanzania wanao uwezo wa kushika nafasi nyeti katika taasisi kubwa za kimataifa, wakielezea faraja yao kwa jinsi Tanzania inavyozidi kung’ara kwenye majukwaa ya kidiplomasia duniani.

Aidha, Rais Samia amesifiwa kwa kuunda kikosi kazi maalum kilichoongozwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa ajili ya kuratibu na kusimamia kampeni ya kidiplomasia ya Profesa Janabi.

Ushirikiano huo umeibuka na matokeo chanya, ambapo Profesa Janabi ameibuka mshindi kwa kishindo kupitia mchakato wa uchaguzi uliopigiwa kura na nchi wanachama wa WHO Kanda ya Afrika.

Dkt. Kikwete, ambaye ana uzoefu mkubwa katika medani za kimataifa, amepongezwa kwa kutumia umahiri na uhusiano wake wa kidiplomasia kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa. Mchango wake umetajwa kama kichocheo muhimu kilichowezesha Tanzania kupata ushindi dhidi ya wagombea kutoka Côte d’Ivoire, Guinea na Togo.

Katika picha iliyopigwa wakati wa harakati za kampeni hiyo, Dkt. Kikwete anaonekana akiongoza moja ya vikao vya kikosi kazi hicho, ambacho hatimaye kilitimiza azma yake mnamo Jumapili, Mei 18, 2025, kwa ushindi mkubwa wa Profesa Janabi.

Mgombea huyo wa Tanzania alipata kura 32 kati ya 47 zilizopigwa kwa siri na wajumbe wa nchi wanachama wa WHO Afrika, kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu wa WHO.

Uchaguzi huo umefanyika kufuatia kifo cha ghafla cha aliyekuwa Mkurugenzi mteule, Dkt. Faustine Ndugulile, mnamo Novemba 2024. Nafasi hiyo ilivuta wagombea mahiri kutoka mataifa kadhaa, lakini Profesa Janabi alifanikiwa kuungwa mkono kwa wingi, akionesha kuwa jina la Tanzania bado lina nguvu katika diplomasia ya afya barani Afrika.

Kwa mujibu wa taratibu za Shirika la Afya Duniani, jina la Profesa Janabi sasa litawasilishwa kwa ajili ya kuthibitishwa rasmi na Bodi ya Utendaji ya WHO katika kikao chake cha 157 kitakachofanyika Mei 28–29, 2025, mjini Geneva, Uswisi.

Iwapo atathibitishwa, Profesa Janabi ataapishwa na kuanza kutekeleza rasmi majukumu yake kwa kipindi cha miaka mitano, huku akiwa na fursa ya kuongezewa muhula mmoja zaidi kulingana na kanuni za taasisi hiyo.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025

October 23, 2025

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA YA NYAKASUNGWA JIMBO LA BUCHOSA

October 18, 2025

RC Malisa Azindua Wodi ya Watoto Wachanga Hospitali ya Meta Mbeya kwa Ushirikiano wa IHI na NEST360 Tanzania

October 18, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025200

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025126
Don't Miss

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

By Mbeya YetuOctober 27, 20251

Ndoa yangu ilifika hatua ya kutisha. Kila usiku tulikuwa tukilumbana kuhusu kitu kipya, hasa pesa…

MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”

October 27, 2025

“Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo

October 27, 2025

Nilivyomfanya Mtu Aliyenidharau Kuniheshimu na Kunitegemea Kwa Mambo Mengi

October 27, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025

MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”

October 27, 2025

“Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo

October 27, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025200

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.