Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet

October 25, 2025

Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu

October 24, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29

October 24, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet
  • Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu
  • Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29
  • MKONGOMAN ATOA USHUHUDA MZITO KUTOWEKA KWA AMANI NCHINI JAMHURI YA KONGO
  • DKT HARRISON MWAKYEMBE ATOA SOMO ZITO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
  • DC ITUNDA ATETA NA WANA VICOBA AWAPA NENO HILI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKT 29
  • WANANCHI KATA IGANZO MTAA MWAMBENJA WAISHUKURU MBEYA UWSA KWA MRADI WA MAJITAKA
  • TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home ยป TANZANIA WENYEJI WA WARSHA YA WAKUU WA TAASISI ZA KUPAMBANA NA RUSHWA KUTOKA NCHI ZA SADC
Habari za Kitaifa

TANZANIA WENYEJI WA WARSHA YA WAKUU WA TAASISI ZA KUPAMBANA NA RUSHWA KUTOKA NCHI ZA SADC

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 4, 2025No Comments21 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Arusha, Agosti 4, 2025

Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa Warsha ya Wakuu wa Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), itakayofanyika kwa siku tatu kuanzia Agosti 4 hadi 6, 2025, katika Hoteli ya Gran Melia, jijini Arusha.

Warsha hii ya kimataifa inafanyika wakati Tanzania ikiwa na jukumu la Uenyekiti wa Kamati ya Kupambana na Rushwa ya SADC (SADC Anti-Corruption Committee – SACC) kupitia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), nafasi ambayo ilianza rasmi Oktoba 2, 2024.

Hii ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya nchi wanachama chini ya Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC ambayo kwa sasa inaongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tangu Agosti 17, 2024.

Warsha hiyo pia itaambatana na maadhimisho ya miaka 20 ya utekelezaji wa Itifaki ya SADC Dhidi ya Rushwa, itifaki ambayo ilianza kutekelezwa rasmi Julai 2005 kwa lengo la kuimarisha mifumo ya kuzuia, kugundua, kuadhibu na kutokomeza rushwa katika sekta za umma na binafsi ndani ya nchi wanachama.

Malengo mahsusi ya warsha hii ni pamoja na:

  1. Kutafakari miaka 20 ya utekelezaji wa Itifaki ya SADC Dhidi ya Rushwa โ€“ mafanikio na changamoto.

  2. Kutathmini mafanikio yaliyopatikana na kubaini mapungufu katika sheria, uwezo wa taasisi na ushirikiano wa kikanda.

  3. Kuweka vipaumbele vya kimkakati kwa mustakabali wa mapambano dhidi ya rushwa katika ukanda wa SADC.

Katika warsha hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Francis Chalamila, ambaye pia ni Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa SACC, atakabidhi rasmi kijiti cha Uenyekiti kwa mwakilishi kutoka nchi ya Malawi.

Ni muhimu kukumbusha kwamba Tanzania ilipongezwa na Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa SADC katika mkutano wao wa 27 uliofanyika Julai 21โ€“25, 2025 jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo, Katibu Mtendaji wa SADC, Elias Magosi, alisifu juhudi za Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa, akieleza kuwa nchi imeonesha mafanikio makubwa katika maeneo ya mifumo ya kisheria, dhamira ya kisiasa na ushiriki wa wadau.

Kupata heshima ya kuwa mwenyeji wa warsha hii ni ushahidi wa nafasi ya Tanzania katika juhudi za kimataifa za kupambana na rushwa, kuimarisha utawala bora, kuendeleza amani na kukuza maendeleo ya kiuchumi katika kanda.

TAKUKURU imesisitiza kuwa imejipanga kuhakikisha kuwa maazimio ya warsha hii yatakuwa na mchango chanya kwa taifa na ukanda wa SADC kwa ujumla.


Mwisho
Imetolewa na: Kitengo cha Mawasiliano โ€“ TAKUKURU
Arusha, Tanzania

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025

October 23, 2025

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA YA NYAKASUNGWA JIMBO LA BUCHOSA

October 18, 2025

RC Malisa Azindua Wodi ya Watoto Wachanga Hospitali ya Meta Mbeya kwa Ushirikiano wa IHI na NEST360 Tanzania

October 18, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025194

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025126
Don't Miss
Uncategorized

Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet

By Mbeya YetuOctober 25, 20250

Kwa muda mrefu, Paul alikuwa mmoja wa wale vijana waliokuwa hawaamini kabisa katika bahati. Kila…

Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu

October 24, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29

October 24, 2025

MKONGOMAN ATOA USHUHUDA MZITO KUTOWEKA KWA AMANI NCHINI JAMHURI YA KONGO

October 23, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet

October 25, 2025

Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu

October 24, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29

October 24, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025194

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.