anisa lilikuwa limejaa waumini, kila mtu akingoja ibada ya muujiza kuanza. Kila siku ya Jumapili, pasta huyu alijulikana kwa maombi yake yenye nguvu, lakini siku hiyo hakujua kwamba angekumbana na tukio ambalo lingemchanganya akili kabisa.
Mwanamke mmoja aliyevalia nguo ya kijani, uso wake umejaa wasiwasi, alisogea mbele. Akapaza sauti mbele ya madhabahu:
“Mchungaji, nina mimba, na baba wa mtoto huyu alikufa mwaka 2003!”
Kanisa lote likatulia ghafla. Vilio vya mshangao vilisikia kutoka kwa watu walioketi nyuma. Pasta akasimama kidogo, macho yake yakimtazama yule mama kwa makini kana kwamba anajaribu kujua kama anatania au anaongea ukweli.
“Mama, unasema nini?” aliuliza pasta kwa sauti ya kushangaa.
“Ninachosema mchungaji… ni kwamba baba wa mtoto aliyeko tumboni mwangu alikuwa mzee wa heshima sana… na alizikwa zaidi ya miaka 20 iliyopita,” alijibu mama akitetemeka. Soma zaidi hapa