Author: Mbeya Yetu

NAIBU Waziri wa habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi(Mb), Maryprisca Mahundi amewataka watanzania kuacha kutoa taarifa zao binafsi kwenye mitandao ya kijamii kwani dunia imeharibika. Amesema wao kama viongozi wanaendelea kufanya wajibu wa kuhakikisha wanathibiti tabia hizo ambazo zimekuwa zikifanyika katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Mhandisi Mahundi amesema hayo Julai 12,2024 wakati akizungumza na wanafunzi wa chuo kikuu cha Katoliki cha CUom kilichopo Jijini Mbeya. “Mimi na wewe lazima tudhibiti pamoja tunza taarifa zako usimpe mtu yeyote na usimwamini mtu leo mpo kwenye urafiki kesho mkikosana amezipeleka harafu inakuja kuleta shida”amesema Mhandisi Mahundi. Aidha Mhandisi Mahundi amesema wao kama…

Read More

Mbunge wa Mbeya vijijini Mhe. Oran Njeza amekutana na wananchi wa Izumbwe II na Iwiji na kusikiliza kero zao ili kuendelea kuzitafutia ufumbuzi.

Wananchi wa kijij cha Izumbwe II risala yao iliyosomwa na afisa mtendaji wa kijiji Kambona Mwahalende, wameomba kutatuliwa kero zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa huduma ya maji safi na ubovu wa barabara.

Wananchi hao pia wakitoa kero zao kwa Mbunge wa Mbeya vijijini, wamesema, wamesema barabara bado ni tatizo katani kwao ikiwemo barabara ya Sayuma hadi Ileya B kisha kutokea kijiji jirani cha Mwakasita ambayo wameomba iangaliwe licha ya kwamba daraja katika eneo lililokuwa korofi tayari lilishajengwa.

Hata hivyo wananchi hao wanaomba kumalizia usambazaji wa nishati ya umeme kwenye vitongoji ambavyo bado havijafikiwa ikiwemo shuleni ili wanafunzi wajisomee vizuri.

Akijibu hoja za miundombinu ya barabara Mhandisi Arcad Tesha ambaye ni Kaimu meneja wa Wakala wa barabara mjini na vijijini TARURA wilayani Mbeya amesema barabara inayolalamikiwa kutoka Sayuma kwenda hadi kijiji jirani cha Mwakasita haitambulikani hivyo wataifuatilia ili kuiingiza kwenye mpango wa bajeti.

Naye Mhandisi wa maji kutoka Wakala wa usambazaji maji vijijini RUWASA wilaya ya Mbeya Evetha Nzogela kwa niaba ya meneja wa RUWASA wilaya anasema wadau ambao ni shirika lisilo la kiserikali CRS limejitoa kujenga mradi wa maji katika moja ya vijiji vitatu vya kata ya Iwiji na endapo kijiji cha Izumbwe hakitanufaika RUWASA itahakikisha inakikumbuka kijiji hicho ili kumtua mama ndoo kichwani kwa kutafuta chanzo cha maji ili kujenga mradi kwa maslahi ya wananchi hao.

Mhandisi Nzogela amewaomba wananchi kuendelea kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki wakati wahisani hao wakiandaa mazingira ya kujenga mradi katani humo.

Mbunge wa jimbo la Mbeya vijijini Mhe. Oran Manasse Njeza, amewahakikishia wananchi kuwa kero zao zitaendelea kutatuliwa kama ambavyo baadhi zimeendelea kushughulikiwa.

Read More

Mbunge wa Mbeya vijijini Mhe. Oran Njeza amekutana na wananchi wa Izumbwe II na Iwiji na kusikiliza kero zao ili kuendelea kuzitafutia ufumbuzi. Wananchi wa kijij cha Izumbwe II risala yao iliyosomwa na afisa mtendaji wa kijiji Kambona Mwahalende, wameomba kutatuliwa kero zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa huduma ya maji safi na ubovu wa barabara. Wananchi hao pia wakitoa kero zao kwa Mbunge wa Mbeya vijijini, wamesema, wamesema barabara bado ni tatizo katani kwao ikiwemo barabara ya Sayuma hadi Ileya B kisha kutokea kijiji jirani cha Mwakasita ambayo wameomba iangaliwe licha ya kwamba daraja katika eneo lililokuwa korofi tayari lilishajengwa. Hata…

Read More

Masumbuko Sompo(51)mganga wa jadi mkazi wa Kijiji cha Nyombwe Kata ya Sangambi Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya anatuhumiwa kumbaka binti yake wa kumzaa mwanafunzi kidato cha tatu mwenye umri wa miaka kumi na Saba. Binti amedai kufanyiwa tukio hilo na baba yake juni 23,2024 usiku wa manane baada ya kumtoa kwa nguvu chumba chake cha nje ambacho hakina mlango. Binti huyo anaishi na mama wa Kambi baada ya mama yake mzazi kufariki akiwa na umri wa miaka minane amedai kuwa siku anafanyiwa ukatili huo alikuwa hajitambui na nguo za baba yake na za kwake zilichukuliwa na wake zake ambazo walimpatia…

Read More

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Urusi, Mhe. Vladimir Putin Jijini St. Petersburg nchini Urusi leo tarehe 12 Julai, 2024 ambapo katika mazungumzo yao wamejadili kuhusu namna bora ya kuimarisha amani Duniani. Kuhusiana na mgogoro unaoendelea baina ya Urusi na Ukraine, Dkt. Tulia amesema “Kabla ya kuzungumza naye tayari tulishazungumza na Maspika wa nchi zote hizo mbili na sisi kama Umoja wa Mabunge Duniani tumezungumza naye kama Kiongozi wa nchi katika sura ambayo tunaweza kuziweka pamoja nchi zote…

Read More