Author: Mbeya Yetu

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ameongoza waombolezaji kutoka Kundi la Afrika pamoja na mataifa rafiki ya Afrika ndani ya IPU kutoa salamu za rambirambi kwa Spika wa Bunge la Zambia, Mhe. Nelly Mutti, kufuatia kifo cha Katibu wa Bunge la Zambia, Marehemu Roy Ngulube, aliyefariki dunia tarehe 7 Aprili 2025 nchini Uzbekistan. Tukio hilo limefanyika leo, tarehe 8 Aprili 2025, jijini Tashkent, Uzbekistan.

Read More

Watumishi wa Afya ambao ni Mabalozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kutoka Dodoma jana wamefanya ziara ya mfano kuitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma (DRRH) na kutoa msaada wa vifaa tiba na dawa kwa watoto wanaohitaji huduma za afya. Akizingumza na Wafanyakazi wa wodi ya Watoto wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Bi. Naima Mkingule ambae ni Kiongozi wa msafara amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi za afya, jamii, na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto wanapata huduma bora na kwa haraka.”Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma bora za afya, ni muhimu kuunganisha nguvu zetu. Ushirikiano…

Read More

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 5 Aprili 2025, amefungua kikao cha 39 cha Jukwaa la Wanawake wa Umoja wa Mabunge Duniani kilichofanyika katika Ukumbi wa Opera, Jijini Tashkent, Uzbekistan.

Kikao hicho kinachoadhimisha miaka 40 ya Jukwaa hilo ni kati ya vikao vya kikatiba vya IPU ambavyo hukutanisha Wabunge Wanawake na kukaribisha pia Wanaume kujadili ajenda za usawa wa kijinsia.

Katika Hotuba yake, Dkt. Tulia amelipongeza Jukwaa hilo kwa kazi nzuri ambayo limekuwa likitekeleza kwa kipindi cha miaka 40 katika kuhakikisha Mabunge Wanachana wanafikia Uwiano na usawa wa Kijinsia na kuendelea kuwahusisha Wabunge wanaume katika kufikia malengo ya Jukwaa.

Read More