Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Nilichukiwa na Kila Mwanamume, Leo Wananipigania Kama Niko Thamani Ya Dhahabu
- Bwana Afichua Jinsi Wake Wawili Walivyopanga Kumnyang’anya Mali Zote Kimya Kimya
- Shitambala Awajibu Wanaosambaza Uvumi: “Mimi ni Mwanachama Mwaminifu wa CCM”
- Shitambala Atangaza Rasmi Kumuunga Mkono Mwalunenge na Rais Samia
- Nilipunguza Uzito Bila Mazoezi, Siri Ni Majani Haya Maalum
- Nilipigania Shamba La Urithi Kwa Miaka 10 Sasa Nimeibuka Mshindi na Familia Imenitazama Kwa Hofu
- WAWINDAJI PANYA WILAYA MOMBA WASAMBABISHIA HASARA MKULIMA WA MAHINDI MBOZI GUNIA 200 ZATEKETEA MOTO
- Mama Afumaniwa Akimroga Mwanawe Ili Abaki Nyumbani Asiolewe
Author: Mbeya Yetu
Naibu Waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya Mhandisi Maryprisca Mahundi amezidi kuyafikia makundi mbalimbali kwa lengo la kuwakwamua kiuchumi. Miongoni mwa kikundi kilichofikiwa na mkono wa kheri ni kikundi cha Mwanamke Shujaa cha Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ambacho kimechangiwa shilingi milioni tano kwa ajili ya ujenzi wa mabanda ya kufugia mifugo mbalimbali yeye akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika Kiwilaya Tukuyu mjini lengo ni kupata 20m kufanikisha malengo. MAHUNDI ACHANGIA 5M KIKUNDI CHA MWANAMKE SHUJAA RUNGWE Naibu Waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum…
#mbeyayetutv
Miaka 8 ya Jumuiya ya Maridhiano na Amani JMAT ilivyoadhimisha Wilayani Kyela.
Mkuu wa Wilaya ya Kyela Josephine Manase amesema Wilaya ya Kyela imeadhimisha Kitaifa Maridhiano Day kwa kuendesha ligi Maalumu ya Kombe la (Samia Maridhiano Cup)ambalo limefikia kilele kwa michuano ya soka.
DC Manase amesema michezo hiyo ya Samia Maridhiano Amani Cup limeacha ujumbe wa amani na ushirikiano kwa wakazi wa wilaya ya Kyela.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano ya Amani Tanzania JMAT Dkt Sheikh Alhad Mussa Salum amesema kombe hilo limechochea ushirikiano wa kijamii kwa kuwahusisha viongozi wa madhehebu ya dini zote.
Kampuni kubwa zinazojishughulisha na masuala ya utalii duniani zimevutiwa kuwekeza nchini Tanzania katika huduma za malazi, usafirishaji na utangazaji utalii. Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika Maonesho ya Utalii ya ITB yanayoendelea jijini Berlin Ujerumani. “Nimefurahi kukutana na kampuni kubwa ya TUI (TUI Group) yenye Makao Makuu nchini Ujerumani ambayo ina hoteli zaidi ya 400 duniani, meli za kitalii 16, mashirika ya ndege matano na zaidi Mashirika 1,200 ya usafiri” Mhe. Kairuki amesisitiza. Na Mwandishi Wetu-Berlin Kampuni kubwa zinazojishughulisha na masuala ya utalii duniani zimevutiwa kuwekeza nchini Tanzania katika huduma za malazi, usafirishaji…
Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi- Arusha.
Mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Arusha TPF-Net katika kuelekea siku ya wanawake Duniani leo wamefanya ibada maalumu kwa ajili ya kuwaombea Askari Polisi wanandoa waliofariki Dunia kwa ajali ya gari siku mbili baada ya kufunga ndoa.
Akiongea mara baada ya ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Theresia Jijini Arusha Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoani humo Mrakibu Msaidizi wa Polisi ASP Happiness Temu amesema mtandao huo umekuwa na utaratibu wa kuyakumbuka makundi mbalimbali yenye uhitaji katika jamii ambapo kwa mwaka huu waliona ni vyema kuwakumbuka Askari waliofariki kwa ajali.
ASP Temu amebainisha kuwa wameamua kufanya Ibada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuwaombea marehemu hao ambao walikua wanafanya nao kazi Mkoani humo kabla kupatwa na umauti Disemba 20, 2022 ambapo pia katika ibada hiyo wamewaombea Watoto wawili ambao waliachwa na marehemu.
Nao baadhi ya askari wa mtaandao huo waliofanya kazi kwa Karibu na marehemu wamebainisha Pamoja na kuwaombea marehemu, pia wametumia ibada hiyo kumshukuru Mungu kwa kuendelea kuwalinda katika utekelezaji wa majukumu yao.
Kwa upande wake Mrakibu wa Polisi SP Asia Matauka ambaye anafanya kazi katika Mkoa wa Kilimanjaro amesema mara baada kusikia juu ya uwepo wa ibada hiyo aliona ni vyema kuungana na mtaandao huo kuwaombea marehemu.
Askari waliofariki na kufanyiwa ibada leo ni Konstebo Noah Simfukwe na Agness Martin.
Mkurugenzi wa kampuni ya usambazaji mbolea ya Bens Patrick Mwalunenge ameahidi kutekeleza ahadi yake ya kutoa shilingi milioni kumi endapo Tanzania Prisons itazifunga timu za Simba na Yanga.
Akitoa taarifa kwa Waandishi wa habari meneja wa Bens Israel Mwampondele baada ya Tanzania Prisons kufanikiwa kuifunga Simba mabao 2-1 katika uwanja wa Jamhuri Morogoro jumatano machi 6,2024 Mwalunenge ameahidi kuikabidhi timu hiyo pindi itakaporejea Mbeya baada ya kumaliza michezo ya ugenini.
Mbali ya ahadi hiyo Mwalunenge ameahidi kumjengea nyumba mchezaji bora baada ya kutamatika ligi ya NBC.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Mkoa wa Mbeya Patrick Mwalunenge amechangia shilingi milioni kumi kwa ajili ya ukarabati wa Uwanja wa Sokoine ikiwa ni utekelezaji wa agizo la TFF.
Katibu Mwenezi na Siasa Mkoa wa Mbeya Christopher Uhagile amemshukuru Mwalunenge kwa hatua alizozichukua vinginevyo uwanja ungefungiwa.
Aidha Meneja wa Bens inayosambaza mbolea Israel Mwampondele ambao ni wadhamini wa Tanzania Prisons amesema uwanja utakarabatiwa uzio,jukwaa kuu na uwanja wa kuchezea mpira wa miguu.
Meneja wa uwanja Modestus Mwaluka amepongeza juhudi zinazofanywa na viongozi ili kuuboresha uwanja wa Sokoine.
#mbeyayetutv
MBUNGE KINANASI AAHIDI KUJENGA UWANJA WA KISASA WA MPIRA WILAYANI KYELA
Mbunge wa Jimbo la Kyela Ally Jumbe Kinanasi ameahidi kujenga uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu na shughuli mbalimbali za kijamii Wilayani Kyela.
Ameyasema hayo wakati wa kilele cha mashindano ya kuwania Kombe la Samia Maridhiano Cup yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Maridhiano ya Amani Tanzania JMAT yaliyozikutanisha timu za Kasala Fc na Iteya FC ambapo timu ya Kasala ilishinda kwa jumla ya magoli 3-1 na kujitwalia Kombe na kitita cha Shilingi Laki Nane ambapo mshindi wa pili Iteya FC alijinyakulia kiasi cha Shilingi Laki Tano wakati viongozi wa Jumuiya hiyo walipozindua kombe la michuano hiyo wilayani Kyela.
‘RAIS SAMIA AMEONDOSHA VIKWAZO,MAANDAMANO, MIKUTANO YA KISASA ITALETA MARIDHIANO KWA WANASIASA’ JMAT
#mbeyayetutv
RAIS SAMIA AMEONDOSHA VIKWAZO,MAANDAMANO NA MIKUTANO YA KISASA ITALETA MARIDHIANO KWA WANASIASA JMAT
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Maridhiano ya Amani Tanzania JMAT Dkt Sheikh Alhad Mussa Salum amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta maridhiano ya kisiasa yaliyoondoa vikwazo vya kisiasa katika mfumo wa demokrasia ya vyama vingi na kuvifanya vyama vya kisiasa kuwa na Uhuru wa kufanya siasa kwa kufanya maandamano na mikutano ya kisiasa jambo ambalo halikuwepo hapo awali.
Sheikh Alhad amesema hayo wilayani Rungwe wakati alipokutana na baadhi ya wananchi katika muendelezo wa Maridhiano Day ambayo inawahusisha viongozi wa madhehebu mbalimbali ya kidini na viongozi wa kimila ambayo yamefanyika kitaifa Jijini Mbeya.
Wazee wadau wa maendeleo mkoani Mbeya leo wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda na kujionea hali bora ya utoaji huduma. Wazee hao wameridhishwa na hatua za maendeleo zilizofikiwa na hospitali hiyo na wametoa sifa kwa uongozi wa hospitali kwa kazi kubwa wanayofanya.
Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na uboreshaji wa huduma za afya katika hospitali hiyo. Wazee hao walishuhudia usafi wa hali ya juu, upatikanaji wa vifaa tiba, na huduma bora zinazotolewa kwa wagonjwa.
Akizungumza baada ya ziara hiyo, mmoja wa wazee alisema wamefurahishwa na maendeleo waliyoona na wanatambua juhudi zinazofanywa na wafanyakazi wa afya katika kutoa huduma bora kwa wananchi. Hata hivyo, wazee hao wametoa wito kwa serikali na wadau kuhakikisha hospitali hiyo inapata fedha za kutosha ili kuendeleza maendeleo hayo.
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imepokea sifa nyingi kutoka kwa wazee hao na imewasisitizia wananchi kuchukua tahadhari na kutembelea vituo vya afya mara kwa mara kwa ajili ya ukaguzi wa afya zao. Wazee hao pia wameahidi kuendelea kushirikiana na uongozi wa hospitali ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa wazee hao, hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya inaendelea kufanya maendeleo makubwa katika utoaji huduma za afya na wana matumaini makubwa kwa mustakabali wa sekta ya afya mkoani humo.
Jeshi la Polisi Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo Nchini katika kuhakikisha linaboresha huduma bora kwa Wananchi limeendelea kuwatambua na kuwapongeza Askari wa Jeshi hilo wanaofanya kazi vizuri zaidi ya kuhudumia wananchi sambamba na kuzuia uhalifu. Akitoa vyeti vya Pongezi kwa Askari hao leo Machi 01, 2024 katika bwalo la maafisa wa Polisi Arusha, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Utawala na Uchumi Bwana Daniel Luloku pamoja na kuwapongeza Askari waliofanya vizuri zaidi amewataka kwenda kufanya kazi kwa nidhamu na kwa weledi mkubwa ilikuhakikisha raia na mali zao wanabaki kuwa salama wakati wote. Bwana Daniel amewataka Askari wengine kuiga mfano…