Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

VIAZI MVIRINGO VYATAJWA KUHARIBU SOKO LA PARETO,PCT YATOA SOMO KWA MAWAKALA WA UNUNUZI NA WAKULIMA

May 9, 2025

MVUA ILIVYOATHIRI BARABARA MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA SAUTI ,MDAU AJITOKEZA KUTOA SAPOTI

May 7, 2025

MVUA ILIVYOATHIRI MIUNDO MBINU MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA KILIO

May 6, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • VIAZI MVIRINGO VYATAJWA KUHARIBU SOKO LA PARETO,PCT YATOA SOMO KWA MAWAKALA WA UNUNUZI NA WAKULIMA
  • MVUA ILIVYOATHIRI BARABARA MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA SAUTI ,MDAU AJITOKEZA KUTOA SAPOTI
  • MVUA ILIVYOATHIRI MIUNDO MBINU MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA KILIO
  • KUSUASUA KWA UJENZI BARABARA NJIA NNE JIJINI MBEYA WANANCHI WATOA MAONI YAO
  • CHAKAMWATA YAJA NA TAMKO KWA RAIS ONGEZEKO LA MSHAHARA KIMA CHA CHINI
  • MADAKTARI BINGWA 36 WA DKT SAMIA WAWEKA KAMBI SIKU 5 MBEYA KUTOA MATIBABU MIKOA NYANDA ZA JUU KUSINI
  • WAANDISHI WA HABARI KUANZA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA TAI-HABARI – MSIGWA
  • “Meya: Deni la Kuipandisha Mbeya City Limelipwa!” Maandalizi Mapya Yaanza kwa Kishindo”
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » KAMATI YA SIASA CCM WILAYA YA MBEYA YATEMBELEA UWANJA WA KIMATAIFA SONGWE YASIFU UTEKELEZAJI ILANI
Video Mpya

KAMATI YA SIASA CCM WILAYA YA MBEYA YATEMBELEA UWANJA WA KIMATAIFA SONGWE YASIFU UTEKELEZAJI ILANI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuDecember 22, 2022No Comments0 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

#MbeyaYetuTv
Serikali inaendelea kujenga jengo kubwa la abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe (SIA) uliopo katika kata ya Bonde la Songwe jimbo la Mbeya vijijini ikiwa ni mkakati wake wa kuboresha sekta ya usafiri wa anga ikiwemo kuweka mazingira rafiki kabla na baada ya abiria kusafiri kutoka na kwenda nchi mbalimbali.

Akitoa taarifa kwa kamati ya siasa ya halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mbeya vijijini (Kichama) kwenye ukaguzi wa mradi huo Kaimu Meneja wa wakala wa barabara Tanzania TANROADS Mhandisi Joel Samwel Mwabungu alisema ujenzi huo unatekelezwa na serikali kwa gharama ya zaidi ya Shilingi Bilioni 14 na wanatarajia kukamilisha jengo hilo kufikia march 2023.

Kuhusu uwekaji taa za kuongozea ndege kiongozi huyo alisema tayari zilishakamilika na zinatumika vizuri hivyo ndege zinaweza kutua na kuanza safari usiku na mchana.

Wajumbe wa kamati ya siasa akiwemo Danieli Kapusi, Willium Simwali na Subiraga Mwangoka walieleza kuridhishwa kwao na utekelezwaji miradi mbalimbali kwenye uwanja huo katika kupanua wigo wa kuwahudumia wasafiri.

Michael Ngailo ni Diwani wa Kata ya Bonde la Songwe ulipo uwanja wa ndege wa Songwe alisema uwanja huo umekuwa na faida kwa jamii isipokuwa changamoto ni wanafunzi wa eneo la Iwejele kuzuiliwa kupita kwenye eneo la uwanja kwenda shuleni baada ya mamlaka kujenga uzio kuzunguka uwanja huo na kuiomba serikali kupitia wizara ya uchukuzi kutekeleza ahadi zao kwa wananchi wa Kata ya Bonde la Songwe Mbeya vijijini.

Msafara wa Kamati ya siasa uliongozwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mbeya vijijini Akimu Sebastian Mwalupindi ambapo baada ya kamati kukagua mfumo wa taa za kuongozea ndege uwanjani hapo na baadaye kukagua jengo la abiria alisema utekelezaji wa ilani ya chama hicho ni wa kiwango cha juu na kinachoridhisha.

Pamoja na hayo CCM wilaya ya Mbeya vijijini kupitia Mwenyekiti Mwalupindi imetumia ziara hiyo ya kikazi kumpongeza Rais Dkt. Samia kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Mwenyekiti wa Chama (CCM) Taifa katika uchaguzi wa hivi karibuni.

Pia imempongeza Rais Samia kwa kuendelea kusimamia ipasavyo utekelezwaji miradi mbalimbali nchini katika kuwatumikia wananchi hususani katika sekta za miundombinu ya usafiri, Maji, Afya, Kilimo na Elimu.

Jengo hilo la abiria linajengwa kwa thamani kwa zaidi ya shilingi bilioni 14 na kampuni ya Kichina ambapo pamoja na miradi mingine ya uwanja wa ndege ya Run Ways na taa za kuongozea ndege jumla yake ni zaidi ya shilingi bilioni 30 zitakazotumika katika miradi hiyo.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

VIAZI MVIRINGO VYATAJWA KUHARIBU SOKO LA PARETO,PCT YATOA SOMO KWA MAWAKALA WA UNUNUZI NA WAKULIMA

May 9, 2025

MVUA ILIVYOATHIRI BARABARA MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA SAUTI ,MDAU AJITOKEZA KUTOA SAPOTI

May 7, 2025

MVUA ILIVYOATHIRI MIUNDO MBINU MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA KILIO

May 6, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024169

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202481

DKT. TULIA ATOA MSAADA WA VIPAZA SAUTI MSIKITI WA MASJID BI FATMA NZOVWE JIJINI MBEYA

March 29, 202457

MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI MBEYA YAANZA,WANAHABARI WATEMBELEA MIRADI

March 16, 202444
Don't Miss
Video Mpya

VIAZI MVIRINGO VYATAJWA KUHARIBU SOKO LA PARETO,PCT YATOA SOMO KWA MAWAKALA WA UNUNUZI NA WAKULIMA

By Mbeya YetuMay 9, 20250

#mbeyayetutv

MVUA ILIVYOATHIRI BARABARA MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA SAUTI ,MDAU AJITOKEZA KUTOA SAPOTI

May 7, 2025

MVUA ILIVYOATHIRI MIUNDO MBINU MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA KILIO

May 6, 2025

KUSUASUA KWA UJENZI BARABARA NJIA NNE JIJINI MBEYA WANANCHI WATOA MAONI YAO

May 5, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

VIAZI MVIRINGO VYATAJWA KUHARIBU SOKO LA PARETO,PCT YATOA SOMO KWA MAWAKALA WA UNUNUZI NA WAKULIMA

May 9, 2025

MVUA ILIVYOATHIRI BARABARA MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA SAUTI ,MDAU AJITOKEZA KUTOA SAPOTI

May 7, 2025

MVUA ILIVYOATHIRI MIUNDO MBINU MITAANI ITEZI MBEYA WANANCHI WAPAAZA KILIO

May 6, 2025
Most Popular

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024169

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202481

DKT. TULIA ATOA MSAADA WA VIPAZA SAUTI MSIKITI WA MASJID BI FATMA NZOVWE JIJINI MBEYA

March 29, 202457
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.