Kaimu Kaimu Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya UNESCO Tanzania Fatuma Mrope wa kwanza kutoka kulia akikabidhiwa baadhi ya taarifa na Mnufaifaika wa Ufadhili wa Masomo nchini Poland George Kato wa tatu kutoka kushoto katika makabidhiano yaliyofanyika katika Ofisi ya Tume hiyo jijini Dar es Salaam
UNESCO Tanzania yataka vijana kuchangamkia fursa za ufadhili wa masomo nje ya nchi -Kaimu Katibu Mtendaji Mkuu Fatuma
*Miradi ya Kimkakati ni fursa ya kwenda kupata ufadhili na kuongeza maarifa
Na Mwandishi wetu
Vijana nchini wametakiwa kuchangamkia fursa za kusoma nchi nchi zinazotolewa Tume ya Taifa ya UNESCO kutoka nchi wafadhili.
Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania imekuwa inapata ufadhili wa vijana katika kusoma nchi mbalimbali lakini changamoto iliyopo ni vijana kutoomba nafasi hizo za kusoma.
Hayo ameyasema Kaimu Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume Fatuma Mrope amesema kuwa nafasi zipo nyingi za kusoma katika nchi za Poland ,China na nchi nyingine.
Amesema Teknolojia zinabadilika kila siku katika program za kusoma ambapo nchi ambazo zinatoa ufadhili zimefika mbalimbali ambapo kwenye miradi ya kimkakati inayofanyika nchini wanaweza kutumika kuliko kutafuta nje ya nchi hizo zilizoweza kuwa Teknolojia hizo na zikatoa ufadhili.
Kaimu huyo Fatma amesema kazi ya UNESCO ni kutafuta nchi zenye utayari wa kutoa ufadhili kwa vijana nchi za Afrika katika shahada ya kwanza,Shahada ya pili pamoja na shahada Uzamivu (PhD) na kuzitangaza kwa watanzania ili waweze kuomba na kunufaika nazo.
Akielezea utaratibu ulivyo Afisa Program wa UNESCO Tanzania Adrian Hyera amesema ufadhili unaotolewa ni bure na kazi kubwa kwa wanahitaji ni kuomba kwenye tovuti za Tume ya Taifa UNESCO Tanzania.
“Nchi nyingi fursa ufadhili wa kusoma wanazitumia zikifika Tanzania vijana hawaombi hadi program za nchi zilitoa ufadhili zinaisha”amesema Hyera
Aidha amesema kuwa ufadhili huo licha ya kuwa bure ni bure kwa kipindi unachokuwa unasoma na gharama zinazomhusu kama mwanafunzi ni kusoma tu.
Hyera amesema kuwa vijana wanaotaka kupata ufadhili nafasi ziko za kutosha kwani idadi wakati mwingine wanatakiwa 10 nchi lakini Tanzania unakuta hata kijana mmoja hajaenda.
Mmoja wa Wanufaika George Kato aliyekwenda kusoma utalii wa Miamba nchini Poland amesema kuwa kwa Tanzania alikuwa pekee yake huku baadhi ya nchi zikiwa zina zaidi ya watano.
Kato amesema kuwa haoni sababu ya vijana kushindwa kutumia fursa wakati kwao inaongeza utaalam wa kufanya kuingia katika ushindani wa soko la ajira.
Amesema kuwa wakati alipoenda ofisi za Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania alipata msaada mkubwa hadi kukamilisha taratibu na kwenda kusoma katika nchi hiyo.
Trending
- Haya tena Dkt. Tulia Huyoooo
- Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amehudhuria hafla ya kuadhimisha miaka 135 ya Bunge la Hungary,
- Sierra Leone wafika Ludewa kujifunza kwa TARURA matengenezo ya barabara
- Wananchi walia na gharama kubwa ya matibabu Wajawazito watozwa Fedha Hospitali ya wilaya Chunya
- RAIS SAMIA ANATAKA TUONGEZE MAPATO YA UTALII- WAZIRI CHANA
- TRA WAMLIZA MBUNGE MASACHE
- FULL VIDEO : MKUTANO MKUU WA 149 WA IPU UKIONGOZWA NA DKT. TULIA
- MADEREVA WANAOTUMIA LUGHA CHECHEFU KWA ABIRIA WAONYWA