Author: Mbeya Yetu

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima Ramadhani akimkabidhi kadi ya Mpiga Kura, Bi. Hanifa Chija mkazi wa Mtaa wa Boma Kata ya Kimobwa, Wilayani Kasulu mkoani Kigoma baada ya kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura katika kituo cha Ofisi ya Mkuu wa Wilaya tarehe 21 Julai, 2024. Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora limeanza Julai 20 na litafikia ukomo Julai 26 mwaka huu. ****** Zoezi la Uboreshaji la Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora…

Read More

Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Mohamed Salum alieleza kuhusiana na mipango ya mkakati katika Bandari ya Nyamisati katika kutoa huduma za Usafiri kwa Vyombo Vidogo vya Majini. Mwenyekiti wa Bodi ya TASAC Nahodha Mussa Mandia akizungumza katika Bandari ya Nyamisati wakati Bodi hiyo ilipofanya ziara Bandari hapo. Meneja wa Bandari ya Nyamisati Issa Unemba akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na utendaji wa Bandari hiyo pamoja na maboresho yaliyofanyika wakati Bodi ya TASAC ilipotembelea Bandari ya Nyamisati wilayani Kibiti mkoani Pwani. *Mkurugenzi Mkuu TASAC asema zaidi ya Bilioni Mbili kununua boti za Uokozi Na Mwandishi Wetu ,Kibiti Bodi ya Shirika…

Read More

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Juma Homera ameagiza kukamatwa na kichunguzwa viongozi wa chama kikuu cha ushirika wilayani Kyela (KYECU) Kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kupelekea upotevu wa zaidi ya millioni 440 za wakulima, baada ya magunia zaidi ya 200 kutoonekana baada ya mnada namba tatu wa zao la cocoa uliofanyika jumatatu July 15 wilayani humo.

Pamoja na kukamatwa viongozi hao akiwemo mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika wilayani Kyela (KYECU) Evance Mwaipopo pamoja na Meneja wa chama hicho Julius Mwankenja, Homera ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Mkoa wa Mbeya, kuchunguza chama hicho mifumo yao ya kifedha huku akisitisha taratibu zote za manunuzi Hadi pale kamati ya ulinzi na usalama itakapo jiridhiaha.

Awali akiwasilisha taarifa Kwa mkuu wa Mkoa, mkuu wa Wilaya ya Kyela Mhe Josephine Manasi, amesema hasara hiyo imeonekana baada ya mnunuzi aliyeshinda mnada namba tatu kubaini magunia zaidi ya 200 hayopo kwenye maghara kati ya magunia 1,915 yaliyoshindanishwa kwenye mnada huo.

Read More