Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba kutoka wizara ya Afya Dkt. Hamad Nyembea ametoa wito kwa Waganga Wafawidhi wa Hospitali za rufaa za mikoa Tanzania Bara kwenda kuongeza Ubunifu wa kuanzisha huduma mpya za Kibingwa katika hospitali zao ili wananchi wapate huduma bora za Afya Dkt Nyembea ametoa wito huo leo tarehe 20 Septemba, 2024 jijini Mbeya katika kuhitimisha kikao kazi cha Waganga Wafawidhi, Wauguzi Wafawidhi, Makatibu wa Hospitali na Waratibu wa Ubora wa Huduma(QI) wa Hospitali za Rufaa za Mikoa ya Tanzania bara.“Niwaelekeze Kupitia kikao hiki kahakikisheni mnakwenda kuboresha huduma kwa kuanzisha angalau huduma mpya za kubingwa nane katika Hospitali zenu ili kuendelea kuongeza imani kwa wananchi.”Pia Dkt. Nyembea amewataka wafawidhi kuboresheni stahiki za madaktari Bingwa ili kuwezesha madaktari hao wasifikiri kuhama (retantion) kwa kuwawekea mazingira wezeshi yatakayonfanya Daktari Bingwa abaki kwenye Kituo chako, na kuwashirikisha katika mipango ili nao waweze kuchangia katika kuboresha huduma za kibingwa katika Hospitali zetu.“Kama wizara tumejiwekea malengo kuwa itakapofikia mwaka 2026 huduma nane za kibingwa katika hospitali zote za rufaa za mikoa ikiwemo huduma za utengemao ambapo ni hospitali Saba mpka sasa ambazo zinatoa huduma za utengema.”Kwa upande wake Mwenyekiti wa Waganga wafawidhi Dkt. Bahati Msaki ambae ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sekotoure amewashukuru viongozi wa Wizara ya Afya kwa kufanikisha kikao hicho kwani kimekuwa kikao kizuri kwa kujitathimini kuona changamoto zilizopo na namna ya kuzikabili na kuwaahidi viongozi hao kwenda kuboresha katika Hospitali zao.”
Trending
- ONGEZENI UBUNIFU KATIKA HUDUMA MPYA MNAZOTOA
- Mbunge wa Mbeya Vijijini Aendeleza Ziara ya Kusikiliza Kero na Kukagua Miradi ya Maendeleo
- KERO ZAENDELEA KUTATULIWA MBEYA VIJIJINI, WANANCHI WATAKA MWENDELEZO.
- WAANDISHI WASAIDIZI KATA MKOA WA SINGIDA WAPIGWA MSASA
- *TANI ZA MBOLEA ZAMWAGWA MBEYA RC HOMERA NA SILINDE WATOA YA MOYONI*
- REGROW Yatoa Muongozo Mpya wa Kupokea na Kushughulikia Malalamiko ya Wananchi Wanaozunguka Hifadhi
- Mh Mahundi Aanza Ujenzi wa Nyumba ya Katibu wa UWT Mkoa wa Mbeya Kwa Gharama ya Zaidi ya Milioni 70
- Jinsi ya Kufikisha Malalamiko Kuhusu Mradi wa REGROW na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha