Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira

December 15, 2025

WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI

December 15, 2025

MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA

December 15, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira
  • WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA
  • Suzi alivyomrejesha mpenzi wake na wakafunga ndoa
  • Jinsi unavyoweza kuibadilisha biashara yako na kukupa faida
  • RAIS DKT. SAMIA AKIWASILI SKUA (TANGA) KWA KIKAO CHA NDANI NA VIONGOZI WA JWTZ
  • WAZIRI MKUU- WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA▪️Ahimiza matumizi ya mbolea na mbegu za mazao
  • Ndipo akashinda Sh13 milioni kupitia betting
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TAKUKURU Mbeya Yaokoa Milioni 47 na Kuongeza Mapato ya Halmashauri Zaidi ya Milioni 200
Habari za Kitaifa

TAKUKURU Mbeya Yaokoa Milioni 47 na Kuongeza Mapato ya Halmashauri Zaidi ya Milioni 200

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 19, 2025Updated:August 19, 2025No Comments58 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Mbeya, Agosti 2025 – Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mbeya imetangaza kufanikisha uokoaji wa zaidi ya shilingi milioni 47 na kuziwezesha Halmashauri kuongeza mapato ya ndani kwa zaidi ya shilingi milioni 200 kupitia ufuatiliaji na udhibiti wa mianya ya rushwa na upotevu wa fedha za umma.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mbeya, Maghela P. Ndimbo, mafanikio hayo yametokana na kazi za ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo, uchambuzi wa mifumo ya ukusanyaji mapato, na kudhibiti matumizi yasiyo sahihi ya fedha katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2025.

Miradi ya Maendeleo na Huduma

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, TAKUKURU ilibaini ubadhirifu wa shilingi milioni 30 zilizotolewa kwa kikundi cha mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Fedha hizo zilielekezwa kwa matumizi mengine kinyume cha taratibu, lakini baada ya ufuatiliaji, kiasi hicho kilirejeshwa kikamilifu kwenye akaunti ya Halmashauri.

Vilevile, uchunguzi ulifanyika kwenye miradi 24 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 8.7 bilioni katika sekta za elimu, afya, barabara na miundombinu. Uchunguzi huo uliibua mapungufu ya utunzaji wa vifaa vya ujenzi na kusababisha upotevu wa mali, hatua zilizochukuliwa zikiwemo uchunguzi maalum na usimamizi zaidi.

Uboreshaji wa Mapato ya Halmashauri

Kupitia uchambuzi wa mifumo ya mapato, TAKUKURU Wilaya ya Mbarali iliwezesha Halmashauri kuongeza mapato kwa shilingi 214,337,401.2. Utafiti ulionyesha mianya ya rushwa katika ulipaji wa ushuru wa huduma, leseni za biashara na kodi za vibanda, ambapo baadhi ya wafanyabiashara walikuwa hawalipi ipasavyo kutokana na ukosefu wa ufuatiliaji.

FEDHA ZA MICHANGO YA WANAFUNZI

TAKUKURU imeokoa shilingi 17,023,750/= ambazo ni fedha za wanafunzi wa chuq ambao walizidisha katika kulipa ada stahiki kwa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya – MUST.

  • Ilibainika kuwa jumla ya wanafunzi 57 kwa kipindi cha Januari hadi Juni, 2025 walikua wakidai malipo ya fedha kiasi cha shilingi 17,023,750/= walizokuwa wamelipa zaidi kwenye akaunti ya chuo kipindi walipokuwa wanafunzi wa chuo

Baada ya kubaini hayo hatua zifuatazo zilichukuliwa;

  • Kuitisha kikao vya majadiliano na Uongozi wa Chuo cha MUST na kuweka mikakati ya namna ya kulipa fedha za wanafunzi
  • Hadi kufikia Juni 26, 2025 wanafunzi wote 57 walilipwa madai yao waliyokuwa wakikidai chuo

.

Uelimishaji na Mapambano Dhidi ya Rushwa

TAKUKURU iliendelea na programu za elimu kwa wananchi kupitia klabu za wapinga rushwa, semina 34, mikutano ya hadhara 36, vipindi vya redio 4 na makala mbalimbali. Pia ilitekeleza programu ya TAKUKURU-Rafiki kwa kushughulikia kero 63 kutoka kata 14.

Wito kwa Wananchi

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mbeya, Maghela P. Ndimbo, ametoa wito kwa wananchi kushirikiana kikamilifu katika kutoa taarifa za vitendo vya rushwa hasa kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025. Amesisitiza kuwa mapambano dhidi ya rushwa ni jukumu la kila mmoja kwa manufaa ya Taifa.


👉 TAKUKURU inakumbusha wananchi wote:
Kuzuia rushwa ni jukumu lako na langu; tutimize wajibu wetu.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Suzi alivyomrejesha mpenzi wake na wakafunga ndoa

December 15, 2025

Jinsi unavyoweza kuibadilisha biashara yako na kukupa faida

December 15, 2025

Ndipo akashinda Sh13 milioni kupitia betting

December 14, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025257

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025235

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024208

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025130
Don't Miss
Video Mpya

Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira

By Mbeya YetuDecember 15, 20250

WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI

December 15, 2025

MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA

December 15, 2025

Suzi alivyomrejesha mpenzi wake na wakafunga ndoa

December 15, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira

December 15, 2025

WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI

December 15, 2025

MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA

December 15, 2025
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025257

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025235

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024208
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.