Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026

February 26, 2026

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
  • MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
  • WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI
  • SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA
  • INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO
  • INEC YAWAPIGA MSASA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA PERAMIHO, SHIWINGA
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
Biashara na Uchumi

Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 26, 2026No Comments3 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Mfumo wa kidigitali wa utoaji wa Vyeti vya Uasili kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP) unaopatikana kupitia tovuti ya tcp.tncc.or.tz unatarajiwa kuanza kutumika rasmi kuanzia Machi 2, 2026, hatua inayolenga kurahisisha na kuharakisha huduma za biashara za kimataifa nchini.

Akizungumza mkoani Mbeya wakati wa mafunzo kwa wasafirishaji wa bidhaa kwenda nje (exporters), Makamu wa Rais Kilimo wa Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC), Bw. Swallah Swallah, amewahimiza wafanyabiashara kujiandaa na kuutumia kikamilifu mfumo huo kwa kujisajili na kuwasilisha maombi yao kupitia tcp.tncc.or.tz, ili kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku.

Alisema kuanza kwa kutumika kwa mfumo huo wa kidigitali wa utoaji wa Vyeti vya Uasili (Certificate of Origin) kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP) ni hatua muhimu itakayoongeza uwazi, kasi na ufanisi katika mchakato wa kupata nyaraka muhimu za biashara za kimataifa kwa njia ya mtandao.

“Kuanzia Machi 2, 2026, tunafungua ukurasa mpya wa utoaji wa Vyeti vya Uasili kwa njia ya kidigitali kupitia tcp.tncc.or.tz.

Mfumo huu utaondoa urasimu, kupunguza muda wa kusubiri na kuongeza ushindani wa wafanyabiashara wetu katika masoko ya nje,” alisema Bw. Swallah.

Alifafanua kuwa mafunzo hayo yaliyoratibiwa na TNCC yamefanyika katika mikoa 14 ikiwemo Mbeya, Rukwa, Katavi, Ruvuma, Songwe, Dodoma, Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara, Singida, Kigoma na Tabora, kwa lengo la kuwajengea uwezo viongozi wa Chemba na wafanyabiashara ili waweze kutumia mfumo huo kwa ufanisi tangu siku ya kwanza ya utekelezaji wake.

Kwa upande wake, mfanyabiashara anayesafirisha mahindi na mchele nje ya nchi, Bi. Felister Mutalemwa, alisema mfumo huo utapunguza gharama na muda wa kushughulikia nyaraka za usafirishaji kwa kuwa huduma zote zitapatikana mtandaoni kupitia tcp.tncc.or.tz.

“Kwetu sisi tunaosafirisha mazao ya kilimo, mfumo huu utarahisisha upatikanaji wa Vyeti vya Uasili bila kulazimika kufuatilia kwa muda mrefu au kusafiri umbali mrefu.

Hii itaongeza ushindani wetu katika masoko ya nje na kupunguza ucheleweshaji wa mizigo,” alisema Bi. Mutalemwa.

Alitoa wito kwa Serikali kuendelea kuimarisha mifumo ya kidigitali na kuhakikisha inawafikia wafanyabiashara wa maeneo yote ya nchi, huku akiwahimiza wafanyabiashara wengine kujitokeza kujifunza, kujisajili na kutumia mfumo huo kikamilifu kupitia tovuti hiyo.

Warsha hiyo inafanyika kwa udhamini wa TradeMark Africa kwa kushirikiana na Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuifanya Tanzania kuwa na mazingira bora na rafiki kwa biashara za kikanda na kimataifa.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.

February 11, 2026

KIKWETE AIPONGEZA BENKI YA NMB

October 8, 2025

Ujenzi barabara ya Lupeta-Wimba-Izumbwe kuinua Uchumi wa wananchi Mbeya.

January 12, 2024

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025356

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Biashara na Uchumi

Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026

By Mbeya YetuFebruary 26, 20263

Mfumo wa kidigitali wa utoaji wa Vyeti vya Uasili kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP) unaopatikana…

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026

February 26, 2026

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya

February 25, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025356

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.