Author: Mbeya Yetu

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Eng Maryprisca Mahundi (Mb.) alikuwa mgeni rasmi katika Hafla ya siku ya Kimataifa ya Wasichana katika TEHAMA, 2024. Hafla hiyo ilikuwa imeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Hafla hiyo ilishirikisha wanafunzi wa kike kuanzia ngazi ya Awali, Msingi, Sekondari, Vyuo vya Kati na Vyuo Vikuu kutoka Tanzania bara, Unguja na Pemba. Naibu Waziri Mahundi aliipongeza TCRA kwa kuhamasisha ushiriki wa Wasichana katika masuala ya TEHAMA kwa kuwa ni muhimu sana katika kipindi hiki ambapo nchi inaelekea katika Uchumi wa Kidijitali. Aidha, Mhe Naibu Waziri Mahundi alisisitiza watoto wa kike…

Read More

#mbeyayetutv
Mke mkubwa wa Mbunge mstaafu wa jimbo la Mbeya mjini Obel Benson Mwamfupe,Bi Sosisyo Kalasya Mwamfupe amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90 na kuzikwa nyumbani kwake Lugombo Mwakaleli wilayani Rungwe.

Mwamfupe alipata kuwa Mbunge jimbo la Mbeya mjini kati ya mwaka 1985-1995.

Mtoto mkubwa wa marehemu ambaye ni Meya wa Jiji la Dodoma Prof Davis Obel Mwamfupe amemzungumzia marehemu Mama yake Sosisyo Kalasya Mwamfupe kwamba ukarimu wake ulisababisha nyumbani kwake Lugombo kutopungua wageni mara kwa mara.

Naye Binti wa marehemu Irene Mwamfupe alisema kuwa mama yake mbali ya kuwa ni mzazi wake alikuwa rafiki na msiri wake mkubwa ambaye alikuwa kiunganishi kikubwa cha watoto na familia nzima ya marehemu Obel Mwamfupe.

Read More

Leo tarehe 25/4/2024, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Dustan Kyobya na Mkurugenzi wa Ifakara Mji Zahara Michuzi wamefika eneo la kingo za mto lumemo ambao umejaa sana kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na kuleta mafuriko kwenye makazi na taasisi za umma na binafsi. Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi kuchukua tahadhari mapema na kuondoka maeneo yote yaliyojaa maji. Baadhi ya shule zimelazimika kufungwa kwa muda mpaka maji yatakapopungua Timu za uokoaji zimepata boti kutoka TAWA na zinaendelea na doria ya nyumba kwa nyumba kuokoa wananchi. Nyumba nyingi bado zimezungukwa na maji, hivyo timu za uokoaji zikiongozwa na kamanda wa zima…

Read More

Makanisa mbalimbali nchini yamekutana Jijini Mbeya kwa lengo la kujadiliana namna ya kuimarisha mahusiano kati ya makanisa na Israel kupitia matukizi ya Teknolojia na utaalamu wa miradi mikubwa ya mazao. Akitoa taarifa kwa wanahabari Mwangalizi Mkuu wa WAPO MISSION INTERNATINAL Profesa Sylvester Gamanywa amesema mradi umeona kuwashirikisha wafanyabiashara Wakristo kutoka Tanzanian katika biashara hizi, kawapa fursa za ubia zinazowiana na dhamira yetu ya kukuza uchumi na maendeleo endelevu. Katika hatua nyingine Gamanywa amesema lengo ni kuunga mkono serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan sanjari na kutoa ajira kwa vijana nchini. Kwa upande…

Read More

aasisi ya Tulia Trust imetoa msaada wa vyakula kwa wahanga wa mafuriko yaliyotokea Wilayani Kyela Mkoani Mbeya kutokana na mvua zinazoendelea Kunyesha hapa nchini.

Vyakula vilivyotolewa na kukabidhiwa kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Josephine Manase ni mchele Kg 300, maharage Kg 50, sukari Kg 75 pamoja na unga wa ugali Kg 125.

Tulia Trust chini ya mkurugenzi wake ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Mhe.Dkt. Tulia Ackson inatoa pole kwa wale wote waliokumbwa na Janga hilo la mafuriko.

Read More

Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Profesa Hamis Malebo Na Mwandishi Wetu Maalum ,Marekani Nchi ya Tanzania umetoa ujumbe wake Kwa Umoja wa Mataifa kuwa haitishi wala kukandamiza raia wake Ujumbe huo umetolewa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO Profesa Hamis Malebo kwenye mkutano Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) ulionza Aprili 15 na kuhitimishwa Aprili 26 unaofanyika nchini Marekani Prof. Malebo ameueleza mkutano huo wa Umoja wa Mataifa kuwa Tanzania nchi inayofuata misingi ya sheria katika mifumo ya kiutawala. “Inasikitikisha kwamba kongamano hilo linatumiwa vibaya kwa…

Read More

Taasisi ya Tulia Trust imeanza ujenzi wa nyumba ya Bi. Eliza Yongo Mwaifwani mkazi wa mtaa wa Ilolo kata ya Ruanda Mbeya Mjini kupitia mpango wa Tulia Trust Mtaani Kwetu. Bi.Mwaifwani anaishi na familia yake ya watoto sita katika mazingira magumu na atakabidhiwa nyumba hiyo mapema mwezi Mei mwaka huu. Sambamba na ujenzi huo Tulia Trust inayoongozwa na Mkurugenzi wake ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe.Dr.Tulia Ackson wametoa vifaa vya Shule (Daftari na Sare za Shule) kwa Watoto watatu wa familia hiyo ili…

Read More

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera emewataka wananchi wa mkoa wa Mbeya kutambua kuwa mafanikio yaliyopo mkoani Mbeya yanatokana na jitihada zinazofanywa na Rais wa Awamu ya Sita, Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye ni zao la Muungano. Mhe. Homera ametoa rai hiyo mapema leo tarehe 22 Aprili, 2024 eneo la Uhindini lilipokuwa soko la zamani wakati wa dua ya kuliombea Taifa ikiwa ni sehemu yamaadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ulioasisiwa na Rais wa Kwanza wa Tanzania Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Sheikh Abeid…

Read More