Author: Mbeya Yetu

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Cde: Juma Z .Homera Amesema Serikali Iko tayari kuwapatia Viwanja 21 Waathirika ambao kaya zao zilifukiwa na Udongo mzito uliotokana na Kupasuka kwa Mlima Kawetere ulioko Kata ya Itezi Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Ameyasema hayo Leo alipoupokea Ugeni maalumu Kutoka Ofisi ya Rais Ikulu ukiongozwa na Mshauri wa Rais Maswala ya Siasa na Uhusiano wa Jamii Mh: Wilium Lukuvi(Mb) uliokuja Kutoa Msaada kama Salamu za pole kwa Waathirika hao ambapo Msaada huo umepokelewa na Dkt: Tulia Ackson Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini.

Katika Salamu zake RC Homera Amesema Mh:Rais Dkt:Samia Suluhu Hassan amempa Maagizo hayo kupitia kwa Mshauri wake(Mh: Lukuvi) ambapo naye ameiagiza Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuhakikisha Zoezi hilo linafanyika haraka iwezekanavyo.

Read More

#mbeyayetutv
Kundi la baadhi ya Wafanyabishara wakubwa Jijini Mbeya wanaofahamika kwa jina la Mbeya Real Friends wameguswa na tukio la mafuriko lililoukumba mtaa wa Maanga Veta Kata ya Ilemi Jijini Mbeya na kuchangia msaada wa chakula wenye thamani ya Shilingi milioni 2 kwa Waathirika 23 wa maeneo hayo.

Msaada huo umewasilishwa na Mwenyekiti wa Kundi hilo Francis Msae na kupokelewa na Diwani wa Kata ya Ilemi Angelo Magoma kwa niaba ya wananchi wa maeneo hayo.

Read More

Mwenyekiti wa Wanawake Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya Aminael Julias ameongoza wanawake wenzie kutoa faraja Kambi shule ya msingi Tambuka reli Kata ya Itezi Jijini Mbeya kwa waathirika wa maporomoko mlima Kawetere yalitokea aprili 14,2024.

Aminael amesema wao kama Wanawake wameguswa na tukio hilo zito hivyo wamekabidhi nguo za kike,taulo za kike,pampas,vyakula na mipira kwa ajili ya kuchezea watoto.

Mwakilishi kutoka ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha maafa amewashukuru Wanawake hao kwa namna walivyoguswa kutoa msaada kwani serikali peke yake isingeweza kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa baadhi ya waathirika hawakuweza kuokoa chochote katika nyumba zao.

Read More

Mwenyekiti wa Wanawake Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya Aminael Julias ameongoza wanawake wenzie kutoa faraja Kambi shule ya msingi Tambuka reli Kata ya Itezi Jijini Mbeya kwa waathirika wa maporomoko mlima Kawetere yalitokea aprili 14,2024.Aminael amesema wao kama Wanawake wameguswa na tukio hilo zito hivyo wamekabidhi nguo za kike,taulo za kike,pampas,vyakula na mipira kwa ajili ya kuchezea watoto. Mwakilishi kutoka ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha maafa amewashukuru Wanawake hao kwa namna walivyoguswa kutoa msaada kwani serikali peke yake isingeweza kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa baadhi ya waathirika hawakuweza kuokoa chochote katika nyumba zao. Ziara…

Read More

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya CPA Gilbert Kayange amesema Mamlaka yake ina dhamana ya kutoa huduma ya maji Safi na Usafi wa Mazingira kwa wananchi wanaoshi Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi., Katika kutoa huduma za maji safi na usafi wa mazingira mamlaka inazingatia malengo yake na Taifa mwaka 2020 kuwa ifikapo mwaka 2025 kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)kuhakikisha huduma za maji zinapatikana kwa asilimia 95. Ameyasema hayo baada ya kutembelea maendeleo ya ujenzi wa tanki mradi mkubwa wa kimkakati Kiwira linalojengwa Forest mpya Jijini Mbeya. CPA Kayange amefurafishwa na…

Read More

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya CPA Gilbert Kayange amesema Mamlaka yake ina dhamana ya kutoa huduma ya maji Safi na Usafi wa Mazingira kwa wananchi wanaoshi Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi.

Katika kutoa huduma za maji safi na usafi wa mazingira mamlaka inazingatia malengo yake na Taifa mwaka 2020 kuwa ifikapo mwaka 2025 kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)kuhakikisha huduma za maji zinapatikana kwa asilimia 95.

Ameyasema hayo baada ya kutembelea maendeleo ya ujenzi wa tanki mradi mkubwa wa kimkakati Kiwira linalojengwa Forest mpya Jijini Mbeya.

CPA Kayange amefurafishwa na maendeleo ya ujenzi wa mradi huo unaotarajiwa kukamilika mwezi machi 31,2025 uwe umekamilika.

Aidha ametaka ushirikiano baina ya Mamlaka, Mhandisi Mshauri na Mkandarasi kuhakikisha kazi inafanyika Kwa Kasi na ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake Mhandisi Barnabas Konga msimamizi wa mradi huo amesema usanifu wa mradi umekamilika ambapo utatakelezwa kwa kipindi cha miaka miwili na kwamba mradi utakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Naye Mhandisi Colman Ngainayo Mshauri katika mradi huo amesema vifaa vingi vimesogezwa eneo la mradi na kazi itakwenda kwa kasi kama ilivyokusudiwa.

Naye Mhandisi msaidizi Hendrick Munuo Mkandarasi anayetekeleza mradi huo amesema kwa sasa mradi unatekelezwa kwenye banio,tanki la kusafishia maji na tanki lenye uwezo wa kupokea lita milioni tano za maji lililopo Forest mpya Jijini Mbeya ambapo kazi zote hizo zinakwenda vizuri.

Kukamilika kwa mradi wa maji Kiwira mbali ya Mamlaka kuongeza mapato utamaliza kabisa changamoto ya maji Jijini Mbeya na Wilaya jirani.

Read More