Author: Mbeya Yetu

Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya ( MBEYAUWSA) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Bi Edina Mwaigomole imetembelea Kambi ya waathirika wa maporomoko mlima Kawetere iliyopo shule ya msingi Tambuka reli Kata ya Itezi Jijini Mbeya na kutoa msaada wa vyakula kwa lengo la kuwatia moyo.Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya CPA Gilbert Kayange amesema amesema ujio wao ni ishara ya upendo na kuwatia moyo waathirika wa tukio hilo huku akiwapongeza Viongozi mbalimbali ambao wamelichukua suala hilo kwa uzito mkubwa.CPA Gilbert Kayange amesema vyakula vilivyotolewa ni pamoja na kilo mia nne…

Read More

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Jerry Silaa ameagiza kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Mwanjelwa aliyejulikana kwa jina la Brayan Mwakalukwa na Ezekiel Mwanje mwakilishi wa mmiliki wa anayedaiwa kuuziwa Nyumba ambayo ni mali halali ya Li Shi Cai ambaye ni mwekezaji raia wa China wakidhani amekufa na Korona.

Waziri Silaa amaeagiza kutafutwa mtu mwingine mmoja anayefahamika kwa jina la Nida ili aweze kueleza jinsi alivyozibeba milioni 80 ambazo ni pesa za mauzo ya nyumba ya Li Shi Cai.

Read More

Katibu wa Umoja wa Wanawake ambaye pia ni Mkurugenzi wa Raslimali watu Miriam Msalale amesema wamechangishana ili kupata fedha hizo kupitia mishahara,posho na biashara zao.Watumishi Wanawake vitengo mbalimbali Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kupitia umoja wao wamekaa   kitanda cha kisasa kwa ajili ya upasuaji chenye thamani ya shilingi milioni thelathini na saba.Mwenyekiti wa Umoja huo Stellah Nkwama amesema lengo ni kuungana na Wanawake wengine katika maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani inayofanyika mwezi machi kila mwaka. Katibu wa Umoja wa Wanawake ambaye pia ni Mkurugenzi wa Raslimali watu Miriam Msalale amesema wamechangishana ili kupata fedha hizo kupitia mishahara,posho na…

Read More

Ibada ya Mbaraka kwa Askofu Mteule Robert Pangani wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi itafanyika Juni 2,2024 Viwanja vya Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji Jijini Mbeya.
Akitoa taarifa kwa Wanahabari Makamu Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania Askofu Kenani Panja amesema mgeni Rasmi katika hafla hiyo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Israel Mwakilasa amesema mbali ya Rais wageni mbalimbali wa ndani na nje ya nchi wamealikwa kuhudhuria hafla hiyo.

Askofu Mteule Robert Pangani atakuwa Askofu wa tatu kushika nafasi hiyo baada ya watangulizi Askofu Yohana Wavenza na Askofu Alinikisa Cheyo.

Read More

Maandiko matakatifu katika kitabu cha Biblia Yakobo 1:27 yanasema Dini safi ni kuwaona yatima,wajane na watu wenye uhitaji wakati Korani takatifu Sura ya 4 aya ya 36 inasema thawabu kwa Waislam ni kutoa sadaka kwa watu walio katika dhiki.
Hivi ndivyo Taasisi ya Maryprisca Women Empowerment Foundation(MWEF)inayoongozwa Mhandisi Maryprisca Mahundi Naibu Waziri wa Habari Teknolojia ya Mawasiliano na Habari Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya ambaye ndiye Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Mhandisi Maryprisca Mahundi ilivyojitokeza kutoa msaada kwa waathirika wa maporomoko ya mlima Kawetere Kata ya Itezi Jijini Mbeya.

Baraka Mlonga ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Maryprisca Women Empowerment Foundation(MWEF)amesema Mkurugenzi wake Mhandisi Maryprisca Mahundi alitamani kuwepo lakini yupo nje ya nchi hivyo wapokee msaada huo na uwe faraja kwa waathirika.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Itezi Sambwee Shitambala mbali ya kushukuru kupokea msaada huo ameomba wasisisite kurudi tena kwani bado msaada unahitajika zaidi

Read More

Na. Catherine Sungura-Dodoma Katika mwaka 2024/25, Ofisi ya Rais – TAMISEMI imepanga kutumia shilingi bilioni 841.19 kwa ajili ya ujenzi, matengenezo na ukarabati wa miundombinu ya barabara za wilaya. Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 257.03 ni za Mfuko wa Barabara, shilingi bilioni 127.50 Mfuko Mkuu wa Serikali, shilingi bilioni 325.77 ni za tozo ya mafuta (shilingi 100 kwa lita), shilingi bilioni 4.03 za mapato ya ndani kupitia Wakala ya Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam na shilingi bilioni 126.85 ni fedha za nje. Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, OR-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na…

Read More