Author: Mbeya Yetu

Maandiko matakatifu katika kitabu cha Biblia Yakobo 1:27 yanasema Dini safi ni kuwaona yatima,wajane na watu wenye uhitaji wakati Korani takatifu Sura ya 4 aya ya 36 inasema thawabu kwa Waislam ni kutoa sadaka kwa watu walio katika dhiki. Hivi ndivyo Taasisi ya Maryprisca Women Empowerment Foundation(MWEF)inayoongozwa Mhandisi Maryprisca Mahundi Naibu Waziri wa Habari Teknolojia ya Mawasiliano na Habari Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya ambaye ndiye Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Mhandisi Maryprisca Mahundi ilivyojitokeza kutoa msaada kwa waathirika wa maporomoko ya mlima Kawetere Kata ya Itezi Baraka Mlonga ni Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Maryprisca Women Empowerment Foundation(MWEF)amesema…

Read More

Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amewasili na kupokelewa kwa shangwe na Wanachama, Wapenzi, Mashabiki na Wadau mbalimbali wa maendeleo katika ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya. Mapokezi hayo ni ishara njema ya bendera za CCM zenye rangi ya kijani na njano kuendelea kupeperushwa vema ndani ya Jiji la Mbeya na ni imani kubwa imeendelea kujengeka. Balozi Dkt. Nchimbi mara baada ya kupokelewa, ametoa salamu za upendo za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan #SamiaWaWatanzania🇹🇿 na kuwataka wana Mbeya kuendelea kuchapaka kazi kwa bidii. Huu ni muendeleo wa ziara yake ambapo ameambatana na Katibu wa NEC – Itikadi, Uenezi…

Read More

Rais wa chama cha walimu Tanzania CWT Leah Ulaya ameikumusha serikali juu ya upandishwaji wa madaraja kwa walimu kutokana na baadhi ya walimu nchini kukaa kwenye nafasi moja kwa muda mrefu hali ambayo inapunguza ufanisi wa ufanyaji kazi kitaaluma
Rai hiyo imetolewa mala baada ya ufunguzi wa mkutano mkuu wa 10 wa Mwaka ukiwahusisha umoja wa maafisa Elimu wa mikoa na Wilaya

Aidha katibu wa chama cha walimu CWT Joseph Msalaba amesema mara baada ya mafunzo wanayo yapata maafisa Elimu katika mkutano huo utakao dumu kwa muda wa siku 5 mafunzo yanayo fanyikia mkoani Mbeya utakuwa na manufaa makubwa yatakayo leta manufaa katika sekta ya Elimu nchini

Read More

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Cde Juma Z. Homera amefika Mlima Kawetele uliopolomoka Alfajiri ya Leo na Kusababisha Kufukiwa kwa Nyumba 20, Ng’ombe Wanne na Kuharibika kwa Miundombinu ya Shule ya Mary’s katika Mtaa wa Gombe Kata ya Itezi Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Akizungumza baada Kuwasili eneo la Tukio RC Homera amekanusha Uvumi unaozagaa Mtandaoni ukidai Kuna Maafa katika tukio hilo ambapo amesema zaidi ya hivyo vilivyotajwa Aya ya Kwanza hakuna Madhara mengine Wala Maafa kama inavyoripotiwa na Baadhi ya Watu.

Aidha Homera ameiagiza Halmashauri ya Jiji la Mbeya kufanya Tathimini juu ya Waathirika hasa wale wasio na Malazi ya Kulala wahakikishe wanapatiwa Sehemu hizo wakati huu ambao Serikali inaendelea kupambana kuhakikisha Hali inakuwa Sawa katika Maeneo hayo.

Pia amekiagiza Kitengo Cha Ardhi Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuacha kuwapimia Wananchi Viwanja eneo lenye Changamoto hasa ya Mkondo wa Maji kwa kufanya Kwao hivyo kutasababisha Matatizo kama hayo ambayo yangeweza kuzuilika.

Tukio hilo limetokea Alfajiri ya Kuamkia Leo ambapo chanzo Chake ni Mvua zinazoendelea Kunyesha Mfululizo na Matukio yanayofanana na haya yamekuwa yakitukia Mikoa Mbalimbali ikiwemo Mikoa ya Arusha na Lindi.

Read More

Wananchi wa kata ya Nzovwe na Mabatini jijini Mbeya wameiomba serikali kuwalipa fidia ya kuwasimamisha uendelezaji wa makazi yao na shughuli nyingine za kiuchumi kwa zaidi ya miaka kumi na mbili baada ya mabadiliko ya sheria ya hifadhi za barabara ya kuongeza mita saba mbele kutoka mita 22.5 za awali.

Wananchi wamepaza kilio hicho kwa serikali na kuiomba kuwalipa fidia baada ya kuwakataza kuendeleza makazi yao kwa ajiri ya hifadhi ya barabara ambapo wamedai walifanyiwa tathimini ya nyumba zao toka mwaka 2012 na kwa sasa hawana matumaini ya kulipwa kutokana na mabadiliko yaliyojitokeza.

Timu ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Patrick Mwalunenge kwa kushrikiana na ofisi ya Meneja wa TANROADs mkoa wa Mbeya wamefika eneo lenye mgogoro ili kujionea hali halisi na maelekezo ya chama kwa wananchi.

Read More

Timu ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya ikiongozwa na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya CPA Gilbert Kayange inapambana usiku na mchana kurejesha huduma ya maji katika maeneo ya Nzovwe,lyunga,Viwandani,lnyala,lkuti,Iwambi,TAZARA,Kalone,Itende na Sistila baada ya miundombinu ya mabomba katika chanzo cha Haji Halewa Kata ya Swaya kusombwa na maji machi 6,2024.Akitoa taarifa eneo la chanzo Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya CPA Gilbert Kayange amewatoa hofu wananchi kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na Mamlaka yake. Awali Kayange amesema wamefanikiwa kurejesha huduma chanzo cha lyela baada ya…

Read More

KATIBU Tawala Msaidizi wa Idara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mkoa wa Mbeya Bi. Anna Mwambene amewaasa wafanyabiashara wa Mkoa huo na Watanzania kwa ujumla kutumia Baraza la Ushindani (FCT) katika kutatua changamoto za kibiashara zinazotolewa maamuzi na Mamlaka za Udhibiti au Tume ya Ushindani zilizoanishwa katika Sheria ya Ushindani, 2003 kustawisha ushindani wa haki na kumlinda mlaji katika Soko.   Bi. Mwambene ameyasema hayo alipokuwa akifungua Semina ya elimu kwa Wadau Baraza la Ushindani (FCT) iliyofanyika hivi karibuni jijini Mbeya.Akiwa anatoa mafunzo hayo Mkuu wa Idara ya Uchumi katika Baraza hilo Bw. Kulwa Msogoti alieleza kuwa Baraza la Ushindani…

Read More

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasili Mkoani Arusha ambapo anatarajiwa kuwe Mgeni Rasmi, katika Misa maalum ya Kumbukumbu ya miaka 40 ya Kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine.Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, amepokelewa na Viongozi mbalimbali, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu, na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda.

Read More