Author: Mbeya Yetu

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Edith Swebe Machi 30,2024 ameshiriki katika kongamano la Pasaka la Ushirika wa Kikristo wa Wanafunzi Tanzania (UKWATA) wa Shule za Sekondari Mkoa wa Simiyu ambalo limefanyika katika shule ya Sekondari Itilima iliyopo Wilaya ya Itilima.

Kamanda Swebe alipata fursa ya kuongea na vijana hao wa UKWATA Mkoa wa Simiyu na kuwahasa kujiepusha na matumizi mabaya ya Mitandao ya kijamii kwa kuangalia picha zisizo na maadili kitendo ambacho kinaweza kusababishia madhara ya afya ya akili na badala yake watumie mitandao ya kijamii kwa lengo la kujifunza.

Read More

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mbeya limefanikiwa kuopoa mwili wa mtu jinsi ya kiume daraja la mto Magege Mtaa wa Masewe Kata ya Ilemi Jijini Mbeya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka thelathini na nane hadi arobaini.Akitoa taarifa eneo la tukio Askari wa zamu Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Sajini Abdalah Sebombo amesema tukio limetokea majira ya saa mbili kasorobo asubuhi machi 30,2024.Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa wa Maswe Japhet Mahinya amesema alipata taarifa kutoka kwa mwananchi naye baada ya kufika eneo la tukio na kitoa taarifa Polisi,Polisi walipofika waliona mwili ukiwa korongo la mto hivyo ikawalazimu kuwasilana na…

Read More

Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Rais wa Mabunge Duniani Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt Tulia Ackson imetoa msaada wa vyombo vya kuhubiria Msikiti wa Masjid Bi Fatma Nzovwe Jijini Mbeya.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Dkt Tulia Ackson Afisa Habari wa Taasisi hiyo Joshua Mwakanolo amesema lengo ni kutekeleza ombi la Msikiti huo kwa Mbunge ambapo waliomba vipaza sauti kwa ajili ya ibada.

Kwa niaba ya Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mbeya msemaji wake Shekhe Ibrahim Bombo mbali ya kushukuru amewaomba waumini kumuombea dua ya heri huku akitaka vyombo hivyo vitunzwe kwa uangalifu.

Naye Hemed Kipengele kwa niaba ya Waumini ametoa neno la shukurani akimshukuru Mbunge kwa kutoa vifaa hivyo bila kujali itikadi za Kidini.

Aidha Justin Kayuni Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Ndanyela ameipongeza Taasisi ya Tulia Trust kwa kutoa vifaa hivyo kwani vitasaidia kueneza neno la Mungu.

Hatimaye Abdalah Yundu Shekhe Mkuu wa Wilaya ya Mbeya ameongoza dua ya kumuombea Dkt Tulia Ackson katika kazi zake za kila siku.

Dkt Tulia amekuwa akitoa misaada mbalimbali bila kujali itikadi za Kidini na Kisiasa ambapo hivi karibuni amefanikisha ujenzi wa Misikiti ya Tukuyu Mjini,Kiwira Wilayani Rungwe na Uyole Jijini Mbeya.

Read More

Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Rais wa Mabunge Duniani Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt Tulia Ackson imetoa msaada wa vyombo vya kuhubiria Msikiti wa Masjid Bi Fatma Nzovwe Jijini Mbeya.Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Dkt Tulia Ackson Afisa Habari wa Taasisi hiyo Joshua Mwakanolo amesema lengo ni kutekeleza ombi la Msikiti huo kwa Mbunge ambapo waliomba vipaza sauti kwa ajili ya ibada.Kwa niaba ya Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mbeya msemaji wake Shekhe Ibrahim Bombo mbali ya kushukuru amewaomba waumini kumuombea dua ya heri huku akitaka…

Read More

Timida Mpoki Fyandomo Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana Taifa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Mkoa wa Mbeya ameahidi kutoa godoro kwa mjane Singwava Mwanyanje mwenye watoto sita mkazi wa Itanji Kata ya Iganjo Jijini Mbeya anayejengewa nyumba na Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Rais wa Mabunge Duniani Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini.Clemence Mwandemba Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Mbeya amesema Dkt Tulia amekuwa akifanya mambo makubwa nchini kwa kuwagusa watu wenye uhitaji.Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Itanji Javin Shaha amesema mama huyo anapitia kipindi kigumu hivyo anahitaji…

Read More

Zaidi ya bilioni kumi na Moja zimetumika kukamilisha ujenzi wa miradi mbalimbali katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya ndani ya miaka mitatu tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassani kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita kutokana na aliekuwa rais wa awamu ya Tano kufariki Dunia mwanzoni mwa mwaka 2022 Hayati Dkt.Pombe Joseph Magufuri.

Hayo yamebainishwa na Mganga mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya Dkt.Abdallah Mmbaga wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya hali ilivyo tangu Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwepo madarakani.

Baadhi ya wananchi waliopo Mkoani Mbeya wamezungumzia hali ya huduma ilivyo katika hospitali hiyo wakisema maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali yamefanya hospitali hiyo kuwa kimbilio la haraka kwao huku wakiwapongeza watumishi wa hospitali hiyo kuwa na lugha nzuri kwa wagonjwa tofauti na zamani.

Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya huhudumia wakazi wa Wilaya za Mbeya,Kyela,Chunya,Mbarali na Rungwe.

Read More

Jeshi la Polisi Nchini limesema Machi 20, 2024 lilitoa taarifa kuhusiana na kifo cha Omary Saimon Msamo kilichotokea huko Wilayani Karatu Mkoa wa Arusha Machi 16, 2024.

Akitoa taarifa hiyo leo machi 26,2024 Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime amesema Jeshi hilo lilieleza mazingira ya tukio hilo ambapo amebainisha kuwa ilibidi kushirikisha wataalam mbalimbali wakiwepo wachunguzi wa matukio ya vifo.

DCP Misime aliendelea kueleza kuwa Timu ya uchunguzi wa tukio hilo ilipofanya uchunguzi wa tukio hilo ilibaini kuwa kifo chake hakikuwa cha kawaida bali ilikuwa ni Mauaji.

Aidha Msemaji wa Jeshi hilo alisema Baada ya kubaini hivyo Jeshi hilo lilianza uchunguzi wa mauaji hayo ambapo lilibaini waliohusika wa mauaji hayo.

Sambamba na hilo amebainisha kuwa uchunguzi umebaini kuwa malengo yalikuwa ni kumpora Omary Saimon Masamo chochote kile watakacho mkuta nacho.

Misime ameviambia vyombo vya habari kuwa Waliohusika na mauaji hayo tayari wamekamatwa na wamekutwa wakiwa na simu ya marehemu huku fedha walizompora kiasi cha Shilingi 200,000/= wakiwa tayari wameshagawana na kuzitumia.

Waliokamatwa ni Anthony Paskali ambaye anajulikana kwa jina maarufu Lulu na Emmanuel Godwin Jeseph anayejulikana kwa jina maarufu la Emma wote wakiwa ni wakazi wa Wilaya ya Karatu.

Taratibu zilizobaki za kiuchunguzi zinakamilishwa ili hatua nyingine za kisheria ziweze kufuata.

Pia DCP Misime amesema Jeshi la Polisi linaendelea kutoa tahadhari kwa baadhi ya watu kuacha kueneza taarifa za uwongo, chuki na uzushi dhidi ya mtu mwingine au taasisi kwa ajili ya malengo yao binafsi kwani kwakufanya hivyo watakuwa wanaukaribisha mkono wa sheria uweze kuwafikia na kuchukuliwa hatua.

Read More

Taasisi ya Tulia Trust imetoa mifuko mia nne kwa shule tatu za msingi na sekondari Jijini Mbeya kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya madarasa katika shule hizo. Shule zilizonufaika na msaada huo ni pamoja na Shule ya Msingi Mlimani iliyopo Kata ya Sinde,Sekondari ya wasichana ya Dkt Tulia ilioyopo Kata ya Iyunga na Sekondari ya Itende inayomilikiwa na Jumuia ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)iliyopo Kata ya Itende Jijini Mbeya. Shule ya msingi ya Mlimani iliyopo Kata ya Sinde Jijini Mbeya imepokea msaada wa mifuko mia mbili kutoka Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Dkt Tulia Ackson Rais wa Mabunge Duniani Spika…

Read More

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali watu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Miriam Mmbaga amefungua Kikao cha Baraza Dogo la Wafanyakazi Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini Kikao kilichofanyika Jijini Mbeya akiwataka wafanyakazi kufanya kazi kwa uadilifu na kufika kwa wakati eneo la tukio. Kamishina Utawala na Fedha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mbaraka Semwanza amesema Jeshi la Zimamoto limeendelea kufanya maboresho mbalimbali pamoja na kutoa elimu kwa jamii ambapo serikali imewaongezea vifaa vya kukabiliana na matukio ya ajali kwa kuwapatia magari kumi na mbili ya Zimamoto ambayo yatagawiwa kwenye mikoa mbalimbali. Charo Mangare Kaimu Kamishina wa Opesheni ambaye amesema wamepokea…

Read More