Author: Mbeya Yetu

Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi- Arusha
Ikiwa leo ni Machi 08,2024 kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani, Mtaandao wa
Polisi Wanawake Mkoa wa Arusha wameunga na wanawake wengine Mkoani humo huku
Mtandao huo wakiitumia siku hiyo kuwawekea akiba ya fedha katika mfuko wa uwekezaji (UTT)
kwa Watoto wawili wa askari wanandoa waliofariki kwa ajali ya gari.
Akiongea katika Viwanja vya Ngarenaro Complex Jijini Arusha Mwenyekiti wa Mtandao huo
Mkoa wa Arusha Mrakibu mwandamizi wa Polisi SSP Zauda Mohamed amesema mtaandao huo
katika kuelekea kilele hicho ulianza mapema kutoa elimu maeneo mbalimbali Pamoja na
kufanya ibada ya kuwaombea marehemu.
SSP Zauda ameongeza kuwa katika kuadhimisha siku hiyo waliona vyema kuunga na
kuwawekea akiba ya fedha kwa Watoto wa askari wanandoa waliofariki katika ajali ya gari
ambapo amebainisha kuwa fedha hizo zitawasaidia Watoto hao katika swala la elimu na
mahitaji mengine ya kibinadamu.
Aidha ametoa wito kwa wanawake wengine Mkoani humo kufanya kazi kwa bidii,nidhamu na
kutenda haki ili ustawi bora na wajikwamue kiuchumi na maendeleo ya Taifa kwa Ujumla.
Nae mrakibu msaidizi wa Polisi Lucy Teesa kutoka Makao Makuu ya kikosi cha Kuzuia wizi wa
Mifugo STPU amewaomba wanaweka wenzake kushiriki vyema katika mapambano dhidi
uhalifu ambapo amewaomba kutoa taarifa za uhalifu na kujikitaa katika malezi bora ya Watoto
ili kujenga Jamii iliyostarabika.
Kwa upande wake Mkuu wa kituo cha Polisi Wilaya ya Kipolisi Murieti Mrakibu msaidizi wa Polisi
ASP Tausi Mbalamwezi amewaomba wanawake wenzake kujiamini na kujituma katika
kutekeleza majukumu yao huku akiwaomba kuumuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuliinua taifa kiuchumi.

Read More

Naibu Waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya Mhandisi Maryprisca Mahundi amezidi kuyafikia makundi mbalimbali kwa lengo la kuwakwamua kiuchumi. Miongoni mwa kikundi kilichofikiwa na mkono wa kheri ni kikundi cha Mwanamke Shujaa cha Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ambacho kimechangiwa shilingi milioni tano kwa ajili ya ujenzi wa mabanda ya kufugia mifugo mbalimbali yeye akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika Kiwilaya Tukuyu mjini lengo ni kupata 20m kufanikisha malengo. MAHUNDI ACHANGIA 5M KIKUNDI CHA MWANAMKE SHUJAA RUNGWE Naibu Waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum…

Read More

#mbeyayetutv

Miaka 8 ya Jumuiya ya Maridhiano na Amani JMAT ilivyoadhimisha Wilayani Kyela.

Mkuu wa Wilaya ya Kyela Josephine Manase amesema Wilaya ya Kyela imeadhimisha Kitaifa Maridhiano Day kwa kuendesha ligi Maalumu ya Kombe la (Samia Maridhiano Cup)ambalo limefikia kilele kwa michuano ya soka.

DC Manase amesema michezo hiyo ya Samia Maridhiano Amani Cup limeacha ujumbe wa amani na ushirikiano kwa wakazi wa wilaya ya Kyela.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano ya Amani Tanzania JMAT Dkt Sheikh Alhad Mussa Salum amesema kombe hilo limechochea ushirikiano wa kijamii kwa kuwahusisha viongozi wa madhehebu ya dini zote.

Read More

Kampuni kubwa zinazojishughulisha na masuala ya utalii duniani zimevutiwa kuwekeza nchini Tanzania katika huduma za malazi, usafirishaji na utangazaji utalii. Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika Maonesho ya Utalii ya ITB yanayoendelea jijini Berlin Ujerumani. “Nimefurahi kukutana na kampuni kubwa ya TUI (TUI Group) yenye Makao Makuu nchini Ujerumani ambayo ina hoteli zaidi ya 400 duniani, meli za kitalii 16, mashirika ya ndege matano na zaidi Mashirika 1,200 ya usafiri” Mhe. Kairuki amesisitiza. Na Mwandishi Wetu-Berlin Kampuni kubwa zinazojishughulisha na masuala ya utalii duniani zimevutiwa kuwekeza nchini Tanzania katika huduma za malazi, usafirishaji…

Read More

Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi- Arusha.

Mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Arusha TPF-Net katika kuelekea siku ya wanawake Duniani leo wamefanya ibada maalumu kwa ajili ya kuwaombea Askari Polisi wanandoa waliofariki Dunia kwa ajali ya gari siku mbili baada ya kufunga ndoa.

Akiongea mara baada ya ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Theresia Jijini Arusha Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoani humo Mrakibu Msaidizi wa Polisi ASP Happiness Temu amesema mtandao huo umekuwa na utaratibu wa kuyakumbuka makundi mbalimbali yenye uhitaji katika jamii ambapo kwa mwaka huu waliona ni vyema kuwakumbuka Askari waliofariki kwa ajali.

ASP Temu amebainisha kuwa wameamua kufanya Ibada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuwaombea marehemu hao ambao walikua wanafanya nao kazi Mkoani humo kabla kupatwa na umauti Disemba 20, 2022 ambapo pia katika ibada hiyo wamewaombea Watoto wawili ambao waliachwa na marehemu.

Nao baadhi ya askari wa mtaandao huo waliofanya kazi kwa Karibu na marehemu wamebainisha Pamoja na kuwaombea marehemu, pia wametumia ibada hiyo kumshukuru Mungu kwa kuendelea kuwalinda katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kwa upande wake Mrakibu wa Polisi SP Asia Matauka ambaye anafanya kazi katika Mkoa wa Kilimanjaro amesema mara baada kusikia juu ya uwepo wa ibada hiyo aliona ni vyema kuungana na mtaandao huo kuwaombea marehemu.

Askari waliofariki na kufanyiwa ibada leo ni Konstebo Noah Simfukwe na Agness Martin.

Read More

Mkurugenzi wa kampuni ya usambazaji mbolea ya Bens Patrick Mwalunenge ameahidi kutekeleza ahadi yake ya kutoa shilingi milioni kumi endapo Tanzania Prisons itazifunga timu za Simba na Yanga.

Akitoa taarifa kwa Waandishi wa habari meneja wa Bens Israel Mwampondele baada ya Tanzania Prisons kufanikiwa kuifunga Simba mabao 2-1 katika uwanja wa Jamhuri Morogoro jumatano machi 6,2024 Mwalunenge ameahidi kuikabidhi timu hiyo pindi itakaporejea Mbeya baada ya kumaliza michezo ya ugenini.

Mbali ya ahadi hiyo Mwalunenge ameahidi kumjengea nyumba mchezaji bora baada ya kutamatika ligi ya NBC.

Read More

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Mkoa wa Mbeya Patrick Mwalunenge amechangia shilingi milioni kumi kwa ajili ya ukarabati wa Uwanja wa Sokoine ikiwa ni utekelezaji wa agizo la TFF.

Katibu Mwenezi na Siasa Mkoa wa Mbeya Christopher Uhagile amemshukuru Mwalunenge kwa hatua alizozichukua vinginevyo uwanja ungefungiwa.

Aidha Meneja wa Bens inayosambaza mbolea Israel Mwampondele ambao ni wadhamini wa Tanzania Prisons amesema uwanja utakarabatiwa uzio,jukwaa kuu na uwanja wa kuchezea mpira wa miguu.

Meneja wa uwanja Modestus Mwaluka amepongeza juhudi zinazofanywa na viongozi ili kuuboresha uwanja wa Sokoine.

Read More

#mbeyayetutv
MBUNGE KINANASI AAHIDI KUJENGA UWANJA WA KISASA WA MPIRA WILAYANI KYELA
Mbunge wa Jimbo la Kyela Ally Jumbe Kinanasi ameahidi kujenga uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu na shughuli mbalimbali za kijamii Wilayani Kyela.

Ameyasema hayo wakati wa kilele cha mashindano ya kuwania Kombe la Samia Maridhiano Cup yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Maridhiano ya Amani Tanzania JMAT yaliyozikutanisha timu za Kasala Fc na Iteya FC ambapo timu ya Kasala ilishinda kwa jumla ya magoli 3-1 na kujitwalia Kombe na kitita cha Shilingi Laki Nane ambapo mshindi wa pili Iteya FC alijinyakulia kiasi cha Shilingi Laki Tano wakati viongozi wa Jumuiya hiyo walipozindua kombe la michuano hiyo wilayani Kyela.

Read More

#mbeyayetutv
RAIS SAMIA AMEONDOSHA VIKWAZO,MAANDAMANO NA MIKUTANO YA KISASA ITALETA MARIDHIANO KWA WANASIASA JMAT

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Maridhiano ya Amani Tanzania JMAT Dkt Sheikh Alhad Mussa Salum amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta maridhiano ya kisiasa yaliyoondoa vikwazo vya kisiasa katika mfumo wa demokrasia ya vyama vingi na kuvifanya vyama vya kisiasa kuwa na Uhuru wa kufanya siasa kwa kufanya maandamano na mikutano ya kisiasa jambo ambalo halikuwepo hapo awali.

Sheikh Alhad amesema hayo wilayani Rungwe wakati alipokutana na baadhi ya wananchi katika muendelezo wa Maridhiano Day ambayo inawahusisha viongozi wa madhehebu mbalimbali ya kidini na viongozi wa kimila ambayo yamefanyika kitaifa Jijini Mbeya.

Read More