Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilipata Miscarriage Mara Tano Hadi Nikapoteza Ndoto Zangu Za Kuwa Mama Mpaka Nilipopata Usaidizi Usio na Madhara

January 25, 2026

Nilifanya Kazi Kwa Miaka Miwili Bila Kupata Promotion Ila Nilijitafutia Hiyo Promotion Mwenyewe

January 25, 2026

Ndoa Yangu Ilikuwa Karibu Kuvunjika Lakini Siri Hii ya Mwisho Iliokoa Mapenzi Yetu

January 24, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilipata Miscarriage Mara Tano Hadi Nikapoteza Ndoto Zangu Za Kuwa Mama Mpaka Nilipopata Usaidizi Usio na Madhara
  • Nilifanya Kazi Kwa Miaka Miwili Bila Kupata Promotion Ila Nilijitafutia Hiyo Promotion Mwenyewe
  • Ndoa Yangu Ilikuwa Karibu Kuvunjika Lakini Siri Hii ya Mwisho Iliokoa Mapenzi Yetu
  • Walidhani Ni Bahati Tu Lakini Ukweli Uliofichuka Ulishangaza Kila Mtu
  • NAIBU WAZIRI MAHUNDI AWASIHI WANAFUNZI TENGERU, KUTUMIA ELIMU KUTATUA CHANGAMOTO ZA JAMII
  • Aliiba Kila Siku Bila Kuonekana Siku Moja Hatua Moja Ilimrudisha Mwenyewe Akiwa Ametikisika
  • Nilianza Kudhoofika Bila Sababu Nilipogundua Nilikuwa Nachawiwa, Njia Hii Ilinilinda Milele
  • Vibaka Wamvamia Mwandishi Rashid Mkwinda wa Mbeya Yetu Ajeruhiwa Vibaya Kichwani na Kulazwa
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WAKULIMA 18,000 KUNUFAIKA NA KILIMO MISITU – WAZIRI CHANA
Utalii na Utamaduni

WAKULIMA 18,000 KUNUFAIKA NA KILIMO MISITU – WAZIRI CHANA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 6, 2025Updated:August 6, 2025No Comments4 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema kuwa zaidi ya wakulima 18,000 wanatarajiwa kunufaika moja kwa moja na Mpango wa Taifa wa Kilimomisitu ifikapo mwaka 2031, ambao unalenga kuhakikisha wakulima milioni 15 wanatumia teknolojia na mbinu bora za kilimomisitu nchini.

Mkakati huo uliozinduliwa mwaka 2024 na Mhe Dkt. Philipo Isdori Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umejikita katika kuendeleza kilimomisitu nchini, ikiwa na dhima ya kukuza ufanisi wa mbinu za kilimomisitu na teknolojia zake ili ziweze kutumika na jamii ya wakulima kwa ajili ya kudumisha ustawi wa jamii, uchumi na mazingira.

Akizungumza leo Agosti 6, 2025 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa ya Ushauri ya Kilimomisitu, Waziri Chana alisema kuwa Mkakati huo uliopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii na unalenga kukuza ufanisi wa matumizi ya teknolojia za kilimomisitu ili ziweze kutumiwa na jamii ya wakulima katika kuboresha ustawi wa jamii, uchumi na mazingira.

“Ili kuhakikisha utekelezaji wa mkakati huu unafanyika kwa ufanisi, Wizara imeunda Kamati ya Kitaifa ya Ushauri ambayo leo naizindua rasmi. Kamati hii itakuwa na jukumu la kushauri na kusimamia utekelezaji wa mkakati huu,” amesema Waziri Chana.

Alifafanua kuwa Tanzania ina jumla ya hekta milioni 48.1 za misitu, sawa na asilimia 55 ya eneo la nchi kavu, ambapo asilimia 93 ni misitu ya uoto wa Miombo na asilimia 7 ni misitu ya Uwanda wa Chini, Milimani, Mikoko na mashamba ya miti.

Hata hivyo, alionya kuwa misitu inakabiliwa na changamoto kubwa kama uvamizi, uchomaji mkaa, moto wa misituni na uchimbaji haramu wa madini. “Takwimu zinaonesha kuwa hekta 469,400 za misitu hupotea kila mwaka. Kiwango hiki ni kikubwa mno na kinapaswa kudhibitiwa,” alisisitiza.

Alibainisha kuwa wakulima ni wadau muhimu katika utekelezaji wa Mkakati wa Kilimomisitu kutokana na nafasi yao katika kilimo na uhifadhi wa mazingira, hivyo wataunganishwa katika minyororo ya thamani ya bidhaa za kilimomisitu ili kuongeza kipato na maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Misitu, Bw. Daniel Pancras, akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara, alisema kuwa Kamati hiyo inaundwa na wajumbe tisa kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo Wizara ya Maliasili na Utalii, Kilimo, Mifugo na Uvuvi, TAMISEMI, TFS, TAFORI, TARI-Tumbi, SHIWAKUTA, Bodi ya Kahawa na Vi-Agroforestry.

Naye Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, Prof. Dos Santos Silayo alisema kuwa kilimomisitu ni mbinu shirikishi ya kuchanganya miti na mazao ya chakula ili kuongeza uzalishaji, kuhifadhi mazingira na kusaidia katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

“Mkakati huu utawezesha upatikanaji wa mbegu na miche bora, kuimarisha uwezo wa kitaifa kusimamia mifumo ya kilimo mseto, kuongeza thamani ya mazao, kupanua masoko na kuchochea urejeshaji wa ardhi na uhakika wa chakula,” alisema Prof. Silayo.

Alisema kuwa mafanikio ya mkakati huo yatategemea ushirikiano wa wadau wote katika sekta za misitu na kilimo, na kuhimiza matumizi ya maarifa ya kisasa katika kilimo mseto ili kulinda mazingira na kukuza maendeleo endelevu.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MALIASILI, MAMBO YA NDANI ZATAKIWA KUSHIRIKIANA KUKUZA UTALII

January 24, 2025

WADAU WA UTALII DUNIANI WAVUTIWA KUWEKEZA NCHINI TANZANIA

March 7, 2024

TALII NA MAMA SAMIA HIFADHI YA TAIFA KITULO

December 19, 2023

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025312

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025244

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024220

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025136
Don't Miss
Uncategorized

Nilipata Miscarriage Mara Tano Hadi Nikapoteza Ndoto Zangu Za Kuwa Mama Mpaka Nilipopata Usaidizi Usio na Madhara

By Mbeya YetuJanuary 25, 20262

Ndoto yangu ya kuwa mama ilikuwa kitu nilichokiamini kwa moyo wangu wote. Tangu nikiwa msichana,…

Nilifanya Kazi Kwa Miaka Miwili Bila Kupata Promotion Ila Nilijitafutia Hiyo Promotion Mwenyewe

January 25, 2026

Ndoa Yangu Ilikuwa Karibu Kuvunjika Lakini Siri Hii ya Mwisho Iliokoa Mapenzi Yetu

January 24, 2026

Walidhani Ni Bahati Tu Lakini Ukweli Uliofichuka Ulishangaza Kila Mtu

January 24, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilipata Miscarriage Mara Tano Hadi Nikapoteza Ndoto Zangu Za Kuwa Mama Mpaka Nilipopata Usaidizi Usio na Madhara

January 25, 2026

Nilifanya Kazi Kwa Miaka Miwili Bila Kupata Promotion Ila Nilijitafutia Hiyo Promotion Mwenyewe

January 25, 2026

Ndoa Yangu Ilikuwa Karibu Kuvunjika Lakini Siri Hii ya Mwisho Iliokoa Mapenzi Yetu

January 24, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025312

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025244

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024220
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.