Kuelekea Maadhimisho ya siku maalum ya familia ya Polisi Mbeya, 2026, Benki ya CRDB Mbeya imetoa msaada wa vifaa vya michezo kwa Jeshi la Polisi Mbeya.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Meneja wa CRDB Mbeya ndugu Harrison Andrew amesema kuwa wao kama CRDB wanatekeleza kauli mbiu yao ya “ULIPO TUPO” kwa kuungana na jamii katika shughuli au matukio mbalimbali.
Aliongeza kuwa, wanashirikiana katika mambo mbalimbali na Jeshi la Polisi ikiwemo jitihada za kuzuia na kutokomeza uhalifu hivyo kuelekea sikukuu maalum ya familia ya Polisi Mbeya watakuwepo kuungana na jamii.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga ameshukuru kwa msaada wa jezi za michezo (mpira wa miguu na riadha) zilizotolewa na Benki hiyo.
Aidha, Kamanda Kuzaga amewakaribisha wakazi wa Mkoa wa Mbeya kuungana na Jeshi hilo katika Maadhimisho ya siku maalum ya familia ya Polisi Mbeya itakayojumuisha michezo mbalimbali, burudani na utoaji wa elimu ya masuala ya ulinzi na usalama.
Siku Maalum ya Familia ya Polisi uadhimishwa kila mwaka ambapo kwa mwaka huu itaadhimishwa siku ya jumamosi Februari 14, 2026 kama sehemu ya Jeshi hilo kufanya tathmini ya utendaji kazi, kutoa zawadi kwa Askari waliofanya vizuri zaidi katika utendaji kazi, kuungana na wadau mbalimbali wa ulinzi na usalama pamoja na Wananchi.

