Author: Mbeya Yetu

Mbunge Mteule wa Viti Maalumu wa Mkoa wa Mbeya Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewasihi
wananchi wa Jimbo la Lupa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya kujitokeza kupiga kura oktoba 29,2025 kuhakikisha wanakipa kura za heshima Chama Cha Mapinduzi(CCM)katika ngazi zote tatu yaani Urais, Ubunge na Udiwani.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa Kampeni Jimbo la Lupa Mhandisi Maryprisca Mahundi amewasihi wananchi kwenye Viwanja vya Itumbi Kata ya Matundasi kuwa ni vema wakakiamini Chama cha Mapinduzi huku ameweka bayana ajenda kuu zikiwa ni Barabara, Maji, Afya, Sekta ya Madini na Elimu.

Read More

Mbeya, Septemba 5, 2025 — Spika wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson, ametoa wito kwa vijana nchini kutumia michezo, hususan mpira wa miguu, kama njia ya kujipatia ajira na kuboresha maisha yao.

Dkt. Tulia alitoa kauli hiyo leo wakati wa tamati ya mashindano ya Tulia Trust Uyole Super Cup yaliyofanyika mkoani Mbeya, ambapo alikuwa mgeni rasmi.

Amesema michezo ni sekta yenye fursa nyingi, ikiwemo ajira, na hivyo vijana wanapaswa kujituma, kuwa na nidhamu, na kuendeleza vipaji vyao ili kufanikisha malengo yao.

Aidha, Dkt. Tulia amethibitisha kuwa taasisi yake ya Tulia Trust itaendelea kudhamini mashindano hayo kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo, kwa lengo la kuibua na kukuza vipaji vya vijana pamoja na kuendeleza michezo nchini.

Read More