Author: Mbeya Yetu

Imeelezwa kuwa uuguzi na ukunga ni fani ya wito wa kipekee na inayohitaji si maarifa na ujuzi bali heshima, moyo wa kujitolea, maadili ya juu na upendo kwa binadamu. Hayo yamesemwa na Samwel Mwangoka Mkuu wa Chuo cha Uuguzi na Ukunga Tukuyu katika mahafali ya 14 ya kuhitimu mafunzo ya Stashahada ya uuguzi na ukunga chuoni hapo na kuwasihi kuzingatia maadili kila mahali watakapokwenda na kuwa mfano wa nidhamu, bidii na uadilifu katika kazi. “..mtakuwa na jukumu kubwa la kutoa huduma bora za afya kwa wananchi na mtakabiliana na changamoto mbalimbali na zinaendelea kubadilika, kuanzia kushughulikia matatizo ya afya ya…

Read More

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ndugu Kailima R.K, amefunga kikao cha siku mbili cha Tume na Vyama vya Siasa 18 vyenye usajili kamili na ambavyo vimependekeza wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania  na Makamu wa Rais, kwa lengo la kujadili na kupanga kwa pamoja ratiba ya kampeni za vyama hivyo.    Kikao hicho kilichoketi Agosti 25 na 26, 2025  kilishirikisha vyama vya Civic United Front (CUF), National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi), Union for Multiparty Democracy (UMD), Chama cha Mapinduzi (CCM), National League for Democracy (NLD), United Peoples’…

Read More

Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma Taifa, Ipyana Samson Njiku, leo Tarehe 25/08/2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia chama hicho.
Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.

Read More