Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
- Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
- VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII
- TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
- Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
- MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
- Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
- Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Author: Mbeya Yetu
Mbunge Mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Mh. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amezindua kampeni za CCM Kata ya Mbugani, Wilaya ya Chunya, ambapo aliwaomba wananchi kumpa kura za heshima Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Ubunge Jimbo la Lupa Masache Kasaka na Mgombea Udiwani Bosco Mwanginde. Mahundi alisema Dkt. Samia ni kiongozi shupavu aliyeendeleza miradi ya awamu ya tano na kuanzisha mipya kwa manufaa ya wananchi. Naye Bosco Mwanginde aliwashukuru wanachama kwa kumchagua na kuwataka kushirikiana naye katika kuwaletea maendeleo.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Septemba 21, 2025 ametembelea Halmashauri ya Mji wa Mafinga Wilayani Mufindi Mkoani Iringa ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambapo pamoja na mambo mengine alipokea taarifa ya Mji huo kutoka kwa wasimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025 na kisha kukagua vifaa ambavyo tayari vimepokelewa katika Halmashauri hiyo. Jaji Mwambegele yupo Mkoani Iringa kukagua maandalizi hayo na kutazama kampeni za wagombea katika majimbo ya Mkoa…
Stephen Samuel Langeni, Mkurugenzi wa Maranatha Pharmacy na Maranatha Hospitali, ambaye pia ni Mwakilishi wa Wafanyabiashara Mkoa wa Mbeya, ametoa rai kwa viongozi na wananchi wa mkoa huo kushirikiana kulinda na kutunza rasilimali za kijani ambazo ndiyo fahari ya Mbeya. Akizungumza katika kikao maalum, Langeni alisema jina la Mbeya limekuwa likihusishwa moja kwa moja na mandhari ya kijani, lakini hali hiyo ipo hatarini kupotea kutokana na changamoto za ukataji miti holela pamoja na mwamko mdogo wa upandaji miti. “Mbeya imekuwa ikitambulika kama fahari ya kijani, lakini sasa sifa hii inaondoka kwa kasi kubwa. Kila siku miti mingi inakatwa, na hatua…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele Septemba 19, 2025 ametembelea Halmashauri ya Jiji la Mbeya katika Majimbo ya Uchaguzi ya Mbeya Mjini na Uyole na kupokea taarifa ya mkoa kutoka kwa wasimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mbeya kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025 na kisha kukagua vifaa ambavyo tayari vimepokelewa katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya. Jaji Mwambegele pia alipata fursa ya kutembelea kampeni za wagombea Ubunge wa chama cha CUF na CCM katika majimbo hayo. Kwa mujibu…
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, ametangaza kuwa Mkoa wa Mbeya umepewa heshima kubwa ya kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mhe. Malisa amesema maandalizi yote ya sherehe hizo yanaendelea kwa kasi ili kuhakikisha Mkoa wa Mbeya unakuwa mwenyeji bora na unatimiza matarajio ya kitaifa.
Amesema sambamba na sherehe hizo, Mkoa wa Mbeya utakuwa na matukio mbalimbali ikiwemo:
Maonyesho ya Wiki ya Vijana yatakayofanyika kuanzia tarehe 08 – 13 Oktoba, 2025 katika Uwanja wa Soko la zamani Uhindini.
Misa Maalum ya Kumbukumbu ya Baba wa Taifa, Mwl. Julius Kambarage Nyerere itakayoadhimishwa tarehe 14 Oktoba, 2025 katika Kanisa Katoliki la Mwanjelwa.
Kupokelewa kwa Mwenge wa Uhuru utakaopokelewa na Mkoa wa Mbeya kutoka Mkoa wa Songwe kuanzia tarehe 07 – 13 Oktoba, 2025.
Sherehe za Kilele cha Kitaifa cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, zitakazofanyika tarehe 14 Oktoba, 2025.
Wito kwa Wananchi na Wadau
Mhe. Malisa ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kujitokeza kwa wingi kushiriki sherehe hizo muhimu za kitaifa, hususan wakati Mwenge wa Uhuru unapita katika maeneo mbalimbali ya Mkoa.
Ameeleza kuwa ni muhimu wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kilele ili kuujaza uwanja na kusherehekea tukio hilo la kihistoria.
Vilevile, ameyataka vyombo vya habari kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi ili kudumisha mshikamano, amani na umoja katika Mkoa wa Mbeya na taifa kwa ujumla.
Aidha, amewataka wamiliki wa hoteli na nyumba za kulala wageni kuandaa maeneo ya malazi ya kutosha kwa wageni wote watakaoshiriki, huku akiwataka kutoongeza gharama za huduma hizo.
Wafanyabiashara wa vyakula na usafirishaji pia wamehimizwa kujipanga kwa ajili ya kutoa huduma bora kutokana na wingi wa wageni watakaofika Mbeya kwa ajili ya sherehe hizo.
Hitimisho
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, amesisitiza kuwa Mkoa wa Mbeya umejipanga kikamilifu na upo tayari kwa heshima ya kuandaa kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025.
“Mbeya ipo tayari kwa ajili ya kilele,” amehitimisha.
