Author: Mbeya Yetu

Wananchi wa Jimbo la Mbeya vijijini hususani vijana wamehimizwa kujiandaa kushiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025 kwa maelezo kuwa ni haki yao kuchagua viongozi wanaowataka kwa mujibu wa katiba kwa maendeleo yao. Wito huo umetolewa na Gabriel Kilembe afisa kutoka ofisi ya Mbunge wa Mbeya vijijini Oran Njeza wakati akizungumza na wananchi hususani vijana katika kata ya Inyala waliokusanyika kwa ajili ya bonanza la michezo na kukutanisha vijiji ikiwemo vya Inyala na Darajani. Kilembe amewapongeza vijana kwa kuendelea kushirikiana na viongozi wao kuanzia ngazi ya vitongoji ambao wamekuwa chachu ya kusogeza huduma za maendeleo kwenye maeneo yao katika sekta mbalimbali.…

Read More

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imetunukiwa tuzo maalum ya ushirikishaji jamii katika ujenzi wa barabara yaani ” People Centered Design Approach”. Ushirikishaji huo ni kuhakikisha usanifu unajumuisha mawazo, mapendekezo na mahitaji maalum kwaajili ya jamii itakayohudumiwa na barabara husika baada ya kujengwa hususani maeneo ya shughuli za kijamii kama shule, masoko na huduma za afya (hospitali, vituo vya afya, zahanati na kliniki). Tuzo hiyo maalum imetolewa na Taasisi ya Kimataifa ya ‘FIA Foundation’ kwa kushirikiana na AMEND katika kongamano la Kikanda la Afrika lililofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam lililohudhuriwa na nchi mbalimbali…

Read More

MFUKO wa hifadhi ya Jamii PSSSF imefanya mkutano maalumu na Waandishi wa Habari kutoka Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mbeya, MBEYA PRESS CLUB ikiwa ni sehemu ya kuongeza wigo wa kujua utendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF. Mkutano huo maalumu umefanyika katika ukumbi wa Hotel ya Mgwasi Jijini Mbeya ambapo Waandishi wa Habari wamejengewa uwezo na kuwekewa mazingira mazuri ya kutambua umuhimu wa shughuli zinazofanywa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma PSSSF. Akizungumza katika mkutano huo Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma PSSSF Rehema…

Read More

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kilichokutana Mjini Unguja Zanzibar leo Juni 9,2025.   Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume akizungumza mapema kabla ya ufunguzi wa kikao hicho. Wajumbe wa Baraza hilo wakifuatilia mada katika Mkutano huo. Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi wa…

Read More