Author: Mbeya Yetu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuimarisha ustahimilivu wa Taifa dhidi ya majanga, kupitia utekelezaji wa sera, sheria, mikakati na miradi mbalimbali

Amesema kuwa hatua hiyo itasaidia kuendelea katika kujenga ustahimilivu wa jamii dhidi ya maafa, tutaokoa maisha, mali, na rasilimali za taifa letu.

Amesema hayo leo Jumatatu (Oktoba 13, 2025) wakati alipotoa tamko katika maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Kupunguza madhara ya maafa, katika ukumbi wa mikutano wa City Park Garden jijini Mbeya.

Read More

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Patrobas Katambi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Sera na Uratibu Zanzibar Hamza Hassan Juma wameimwagia pongezi Benki ya NMB kwa kuendelea kushirikiana kwa karibu na serikali kwa kutoa elimu ya kifedha kwa vijana ili kujikwamua kiuchumi. Wameyasema hayo walipotembelea Banda la NMB kwenye maadhimisho ya wiki ya Vijana yanayoendelea viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya. “Mmekuwa na sapoti kubwa kwa serikali kusaidia elimu ya kifedha kwa vijana, Vijana wengi kwa sasa wamejikwamua kiuchumi kutoka na elimu mnayotoa” alisema Waziri…

Read More

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na baadhi ya Wadhamini wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yaliyozinduliwa Oktoba 10,2025 akiwemo Meneja Mahusiano Mwandamizi wa NMB Josephine Kulwa wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Vijana katika Soko la Uhindini jijini Mbeya. Baadhi ya wanafunzi na wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Oktoba 10,2025 katika Viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya wakifuatilia kwa karibu hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi. Wanafunzi wa shule ya Sekondari wasichana Loleza waliotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.…

Read More

Mgombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Ipyana Samson Njiku, ameendelea na kampeni zake za mguu kwa mguu kwa  wananchi wa Jimbo la Uyole, ambapo leo ametembelea maeneo ya Kata ya Itezi na Igawilo akiwahamasisha wananchi kujiandaa kwa mabadiliko chanya kupitia uongozi makini na wenye dira ya maendeleo. Akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali , Njiku amesema kuwa endapo atapata ridhaa ya wananchi wa Uyole, ataweka kipaumbele katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo: Ujenzi wa Soko la Kisasa na Kimataifa litakalowezesha wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao ndani na nje ya nchi…

Read More