Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya
- CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.
- DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji
- KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA
- Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji
- Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo
- TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya
- New Asante Mbeya Yapongeza TAKUKURU Mbeya kwa Elimu ya Uadilifu na Kufungua Uelewa wa Wanachama
Author: Mbeya Yetu
Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjini imefanya matembezi ya amani leo, ikiwa ni sehemu ya ufunguzi rasmi wa maadhimisho ya miaka 49 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi, kilichoasisiwa Februari 5 mwaka 1977. Akizungumza mara baada ya matembezi hayo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mbeya Mjini, Emmanuel Mwalupindi, amewataka wanachama wa chama hicho kuondoa hofu na uoga katika kukitumikia chama chao, akisisitiza kuwa CCM ni chama chenye misingi imara na historia kubwa ya kulihudumia Taifa. Kwa upande wake, Katibu wa Shirikisho la Walimu wa CCM Mkoa wa Mbeya, Daud Siame, ametumia…
#mbeyayetutv
Wakazi wa wilaya ya Kyela mkoani Mbeya wamessimulia fursa zilizopo katika Ziwa Nyasa namna zinavyowanufaisha kiuchumi na kuwapatia kipato
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Bi. Erica Yegella, leo tarehe 29 Januari 2026 amekutana na waandishi wa habari na kutoa taarifa ya mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kipindi cha siku 100, ndani ya Halmashauri hiyo. Mkutano huo umefanyika katika Ofisi za Mbeya Press Club, eneo la Sokoine Jijini Mbeya, ukiwa na lengo la kuujulisha umma kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo na uboreshaji wa huduma za kijamii na kiuchumi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya. Fedha Zilizopokelewa Ndani ya Siku 100 Bi. Yegella amesema kuwa kwa kipindi cha Oktoba 2025 hadi Februari 2026, Halmashauri ya…
Taasisi za Picterus AS (Norway) na GOAL 3 (Uholanzi) pamoja wameshinda ruzuku ya Eurostars ya Euro milioni 1 (takribani Shilingi Bilioni 3 za Kitanzania) ili kuleta teknolojia mpya ya upimaji wa manjano katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini, kukiwa na uwezekano wa kusaidia mamilioni ya watoto kuzuia matatizo makubwa ya kiafya yanayosababishwa na manjano isiyotibiwa katika mazingira yenye rasilimali chache. Taasisi hizo za Picterus AS (Norway) na GOAL 3 (Uholanzi), zinazofanya kazi nchini Tanzania kuunga mkono juhudi za Serikali katika maboresho ya sekta ya afya, zimekusudia kuboresha huduma za afya ya watoto wachanga, hasa kupitia teknolojia kwa kuleta…
Serikali imesema haina haja ya kuweka sharti la kisheria linalowalazimisha watoto kuwahudumia wazazi wao wasiojiweza, ikieleza kuwa suala hilo tayari linashughulikiwa kupitia misingi ya kifamilia na kijamii. Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa kinondoni Mhe. Tarimba Gulam Abbas lililohoji “Je Serikali haioni haja ya kuweka sharti la kisheria la watoto wakubwa kutunza wazazi wao wasiojiweza”? Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inatambua umuhimu wa familia na jamii katika kuchukua jukumu la kulea na kuwahudumia wazee, akisisitiza kuwa huo…
Baraza la Wazee Mkoa wa Dodoma limeshirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum katika upandaji Miti ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Dkt. Samia aliamua kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo kwa kupanda mti ikiwa na lengo la kulinda na kihifadhi mazingira. Wakizungumza mara baada ya zoezi hilo Wazee hao qwamempongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Uongozi wake mahiri na thabiti katika kuliongoza taifa kwa misingi ya amani na utulivu. “Tunampongeza Rais Samia kwa hatua yake…
Wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya wameadhimisha siku ya kuzaliwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kukata keki kama ishara ya mshikamano na pongezi. Maadhimisho hayo yaliongozwa na Diwani wa Kata ya Nsalala, Mhe. Festo Mbilike, aliyempongeza Rais Samia kwa kuwaamini na kuwawezesha vijana kupitia fursa za ajira na mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri. Sherehe hizo zilifanyika Mji Mdogo wa Mbalizi, zikianza na maandamano ya amani ya vijana na bodaboda.
Madaktari Bingwa wa Mifupa na Magonjwa yanayohusiana na Ajali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya leo wameanza kutoa huduma ya uchunguzi na matibabu ya kibingwa mkoani Manyara katika kambi maalumu ya Madaktari Bingwa ya Mifupa, Macho, pua, koo na masikio iliyoandaliwa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara, inayolenga kusogeza na kuboresha huduma kibingwa za afya kwa wananchi wa mkoa wa huo. Kwa upande wake, Dkt Baraka Mponda, Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Mifupa kutoka Rufaa ya Kanda Mbeya, amesema kuwa juhudi hizo ni sehemu ya mkakati wa Serikali na Wadau wa afya wa kuhakikisha huduma za matibabu…
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ametoa vifaa vya kusomea kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum wa Shule ya Msingi Nsalala, Halmashauri ya Mbeya. Vifaa hivyo vikiwemo kompyuta mpakato na rekoda za sauti vinalenga kuboresha mazingira ya ujifunzaji na kuhakikisha elimu bora kwa usawa. Akikabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Bi. Erica Yegera, amesema ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika utekelezaji wa sera ya elimu jumuishi.
