Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Dkt. Shein Awataka Wahitimu wa Mzumbe Mbeya Kujituma kwa Uadilifu na Kulitumikia Taifa
- Sasa chumba chao kimejaa mapenzi na furaha!
- Ingawa alikuwa msomi, alijisalimisha ili apate kazi
- Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
- WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA
- *DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*
- WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI
- Karejesha tabasamu la uso wake na ndoa yake
Author: Mbeya Yetu
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameelekeza Jeshi la Polisi na Uhamiaji kuhakikisha wanamkamata na kuzuia hati ya kusafiria ya mkandarasi anayejenga mradi wa Kituo cha ukaguzi cha Pamoja kilichopo Muhalala mkoani Singida. Dkt. Mwigulu amesema kuwa mkandarasi huyo aliaminiwa na Serikali kwa kupewa ujenzi wa mradi huo wa kimkakati uliosimama kwa zaidi ya miaka nane tangu mwaka 2016. Mradi huo unaojengwa na kampuni ya Impresa di Costruzioni Ing. E. Mantovani S.p.A ulipaswa kukamilika mwaka 2018. Ametoa agizo hilo leo Ijumaa tarehe 21 Novemba, 2025 wakati alipokagua mradi huo katika ziara yake ya kikazi mkoani…
Diwani wa Kata ya Ilomba, Ndg. Noah Edson Mwakisu, leo amerejesha fomu za kuwania Umeya wa Jiji la Mbeya kupitia CCM. Akizungumza katika Ofisi za CCM Mbeya Mjini, Mwakisu alisema anagombea nafasi hiyo ili kulipa jiji mwelekeo mpya wa maendeleo, akisisitiza umuhimu wa uongozi wenye maono, ushirikiano na uwajibikaji.
Mwakisu alisema Mbeya ina fursa kubwa za kimaendeleo kutokana na mazingira na jiografia yake, hivyo inahitaji kiongozi anayeendana na mahitaji ya kizazi cha sasa, hususan vijana ambao ndio nguvu ya uchumi wa jiji. Aliomba sapoti na baraka za wananchi, akiahidi kulifanya jiji hilo mfano wa kuigwa endapo atapewa dhamana.
Kurejesha fomu hizo kunamweka rasmi katika kinyang’anyiro cha ndani ya CCM cha kuwania Umeya wa Jiji la Mbeya mwaka huu.
#mbeyayetutv
Mvua iliyonyesha kwa takribani saa moja Novemba 20 2025 Mtaa wa Lumbila Kata ya Iwambi Jijini Mbeya imeathiri makazi ya watu kutokana na mitaro kujaa maji kuingia kwenye makazi ya watu na baadhi ya sehemu za biashara.
Kijana Golden Kidumba, maarufu kama DON. G, amewagusa watoto wa mitaani kwa kuwapatia chakula, kuwanunulia nguo na kutumia muda wa siku nzima akiwa nao, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kuikumbuka jamii aliyotokea.
Golden, mzaliwa na mkazi wa zamani wa Njombe, anasema maisha magumu aliyoyapitia utotoni ndiyo yamemfanya kuwa na moyo wa huruma na kujitoa kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.
“Nimekulia kwenye maisha magumu sana. Lakini namshukuru Mungu kwa kunibariki na kunifanya niweze kuwakumbuka hawa wadogo zangu wa mitaani. Nimekula nao, nimesherehekea nao na pia nimewanunulia nguo ili wajisikie wanathaminiwa kama watoto wengine,” amesema DON. G.
Amesema kusaidia watoto wa mitaani si tukio la leo pekee, bali ni jambo alilolianza miaka kadhaa iliyopita, ikiwemo kutembelea hospitali na kuwasaidia watu wenye uhitaji.
Golden ameweka wazi kuwa ndoto yake ya baadaye ni kuanzisha taasisi ya msaada na hata kujenga shule maalum kwa ajili ya watoto hao, ili kuwapa elimu, malezi na fursa za kuanza maisha mapya.
Baadhi ya watoto wa mitaani waliopokea msaada huo wameeleza machungu ya maisha yao, ikiwemo vipigo, njaa, manyanyaso na mara nyingi kudharauliwa kama wahalifu bila kujua historia zao.
Kijana Brian Edwin, anayelelewa katika kituo cha Mtama, amesema:
“Maisha ya mitaani ni magumu. Tunapigwa, tunanyanyaswa na tunaishi bila uhakika. Lakini leo tumepata faraja kubwa kutoka kwa DON. G. Mungu ambariki.”
Wengine kama Anody Nyondo na Gifty wameeleza jinsi walivyokimbia nyumbani kutokana na migogoro ya kifamilia na manyanyaso, hali iliyowalazimu kuingia mitaani.
Watoto hao wameiomba jamii na serikali kutowatenga, bali kuwaona kama watoto wanaohitaji msaada na si wahalifu.
Golden ameendelea kutoa wito huo huo:
“Tusishikilie mali bila sababu. Tukiondoka duniani, hatuchukui chochote. Tuwakumbuke watoto wa mitaani; wanahitaji upendo na msaada wetu.”
Rais Dkt Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri Naibu Mawaziri Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu
Rais Dkt. Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu, tarehe 19 Novemba, 2025, Ikulu Chamwino, Dodoma.
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba leo Novemba 17, 2025 amekabidhiwa Ofisi na Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa, Mlimwa Jijini Dodoma Novemba 17, 2025.
Viongozi waliohudhuria hafla ni pamoja na Naibu Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Doto Biteko, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi, Wakuu wa Idara na watumishi wengine wa Ofisi ya Waziri Mkuu.
Taasisi ya Tulia Trust iliyo chini ya Mbunge wa jimbo la Uyole jijini Mbeya Dkt Tulia Ackson, wameanza ujenzi wa nyumba ya famikia ya mzee Anyomwisye Mwalyaje mkazi wa mtaa wa Mwafute kata ya Ilemi iliyoteketea kwa moto usiku wa September 5 kutokana na hitilafu kwenye mfumo wa Umeme.
Ujenzi huo umeanza baada ya Mbunge wa jimbo la Uyole kutoa ahadi ya kumjengea nyumba mzee Anyomwisye Mwalyaje alipomtembelea kutokana na kadhia ya nyumba yake kuteketea kwa moto pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani.
Afisa kutoka taasisi ya Tulia Trust kitendo cha habari Addi Kalinjila amesema ujenzi wa nyumba hiyo unaanza maramoja baada ya vifaa kufika eneo la ujenzi ili kurejesha maisha ya familia hiyo kama yalivyokua hapo awali.
