Author: Mbeya Yetu

Na Mwandishi Wetu, JAB Serikali imesema vitambulisho vya Uandishi wa Habari (Press Card), vitaanza kutolewa wakati wowote baada ya siku saba kuanzia leo Mei 3, 2025 baada ya Waandishi wa Habari kuanza kujisajili rasmi kwenye mfumo wa TAI-Habari. Mwandishi wa Habari ataanza kujisajili kupitia kiunganishi cha https://taihabari.jab.go.tz kisha kufuata maelekezo yaliyotolewa ili kukamilisha kujaza fomu yake kwenye mfumo huo wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari. Kauli hiyo imetolewa tarehe 03 Mei, 2025 na Katibu Mkuu wa Wizara Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa, katika Kijiji cha Sayu mkoani Shinyanga wakati akizungumza…

Read More

Katika shamrashamra za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi, yaliyofanyika katika Uwanja wa Nguzo Nane wilayani Maswa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Comrade Kenani Kihongosi, alikabidhi cheti cha heshima kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bi. Zahara Muhidin Michuzi, kwa kutambua mchango wake mkubwa kama mfanyakazi hodari na mwenye weledi. Bi. Zahara alihamishiwa wilayani Meatu mwishoni mwa mwezi Januari mwaka huu, akitokea Wilaya ya Kilombero Halmashauri ya Mji Ifakara mkoani Morogoro, ambako pia alihudumu kama Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji huo. Kabla ya hapo, alikuwa Mkurugenzi wa Mji Geita katika Wilaya ya Geita, Mkoa…

Read More

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Mwaselela, amekabidhi vyerehani viwili kwa vijana wa Hamasa wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Mbeya Mjini ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha kiuchumi na kuhamasisha uzalishaji wa ndani.

Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano, MNEC Mwaselela alieleza kuwa msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya chama ya kujenga vijana waadilifu, wachapakazi na wenye kujitegemea. Alisisitiza kuwa uwezeshaji wa vitendea kazi ni kichocheo muhimu katika kuleta maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Viongozi wa UVCCM pamoja na wanachama walitoa shukrani kwa mchango huo na kuahidi kuvitumia vyerehani hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa.

Read More

Wananchi wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa. Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025 unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali.  Wananchi wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa katika kiuo…

Read More

Mwemyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na watendaji wa uboreshaji ngazi ya Kata na Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Biometriki kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa leo Aprili 29,2025 wakati alipotembelea mafunzo hayo ikiwa ni maandalizi ya awamu ya pili mzunguko wa kwanza wa uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaoanza Mei Mosi hadi Mei 07, 2025 katika mikoa 15. Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume. Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.   Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa…

Read More