Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo
- TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya
- New Asante Mbeya Yapongeza TAKUKURU Mbeya kwa Elimu ya Uadilifu na Kufungua Uelewa wa Wanachama
- Utengule Usangu Yapata Jezi, Majiko ya Gesi na Msaada wa Kijamii Kutoka kwa Mbunge Ndingo
- Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Aga Khan Zaanzisha Ushirikiano wa Kuboresha Huduma za Afya
- Shule ya Sekondari Utengule Usangu, H
- Mradi wa Barabara Mlima Nyoka Wamfikisha MCC ASAS, Ataka Kero za Wananchi Zitokomee
- Mradi wa Soko la Matola Wakwama, Meya na MNEC Wakanusha Kukamilika Mei
Author: Mbeya Yetu
Serikali imesema haina haja ya kuweka sharti la kisheria linalowalazimisha watoto kuwahudumia wazazi wao wasiojiweza, ikieleza kuwa suala hilo tayari linashughulikiwa kupitia misingi ya kifamilia na kijamii. Kauli hiyo imetolewa bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa kinondoni Mhe. Tarimba Gulam Abbas lililohoji “Je Serikali haioni haja ya kuweka sharti la kisheria la watoto wakubwa kutunza wazazi wao wasiojiweza”? Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inatambua umuhimu wa familia na jamii katika kuchukua jukumu la kulea na kuwahudumia wazee, akisisitiza kuwa huo…
Baraza la Wazee Mkoa wa Dodoma limeshirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum katika upandaji Miti ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Dkt. Samia aliamua kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo kwa kupanda mti ikiwa na lengo la kulinda na kihifadhi mazingira. Wakizungumza mara baada ya zoezi hilo Wazee hao qwamempongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Uongozi wake mahiri na thabiti katika kuliongoza taifa kwa misingi ya amani na utulivu. “Tunampongeza Rais Samia kwa hatua yake…
Wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya wameadhimisha siku ya kuzaliwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kukata keki kama ishara ya mshikamano na pongezi. Maadhimisho hayo yaliongozwa na Diwani wa Kata ya Nsalala, Mhe. Festo Mbilike, aliyempongeza Rais Samia kwa kuwaamini na kuwawezesha vijana kupitia fursa za ajira na mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri. Sherehe hizo zilifanyika Mji Mdogo wa Mbalizi, zikianza na maandamano ya amani ya vijana na bodaboda.
Madaktari Bingwa wa Mifupa na Magonjwa yanayohusiana na Ajali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya leo wameanza kutoa huduma ya uchunguzi na matibabu ya kibingwa mkoani Manyara katika kambi maalumu ya Madaktari Bingwa ya Mifupa, Macho, pua, koo na masikio iliyoandaliwa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara, inayolenga kusogeza na kuboresha huduma kibingwa za afya kwa wananchi wa mkoa wa huo. Kwa upande wake, Dkt Baraka Mponda, Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Mifupa kutoka Rufaa ya Kanda Mbeya, amesema kuwa juhudi hizo ni sehemu ya mkakati wa Serikali na Wadau wa afya wa kuhakikisha huduma za matibabu…
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ametoa vifaa vya kusomea kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum wa Shule ya Msingi Nsalala, Halmashauri ya Mbeya. Vifaa hivyo vikiwemo kompyuta mpakato na rekoda za sauti vinalenga kuboresha mazingira ya ujifunzaji na kuhakikisha elimu bora kwa usawa. Akikabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Bi. Erica Yegera, amesema ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika utekelezaji wa sera ya elimu jumuishi.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru mkoani Arusha na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa chuoni hapo, ikiwemo ujenzi wa jengo la Utawala, kituo cha uhifadhi wa machapisho yanayohusu wanawake, mabweni ya wanafunzi pamoja na Kituo cha Ubunifu wa Kidigitali na Huduma Tandaa (JODIC). Akizungumza mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la Utawala, Mhe. Mahundi amesema serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya vyuo vya maendeleo ya jamii ili kuimarisha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia, sambamba na kuongeza ufanisi…
Mkazi wa eneo la Soweto, jijini Mbeya, Rashidi Mkwinda, ambaye ni mwandishi wa habari wa Mbeya Yetu Online TV, amesimulia tukio la kuvamiwa na kupigwa kichwani na watu wanaodhaniwa kuwa vibaka majira ya saa sita usiku.
Amesema alikuwa akirejea nyumbani baada ya kudownload faili kwenye kompyuta, ndipo alipofuatwa na watu hao na kushambuliwa wakati akifungua geti la nyumba yake. Katika tukio hilo alipigwa mara kadhaa kichwani, akaanguka chini na kupoteza fahamu kwa muda, kisha kuibiwa simu ya mkononi pamoja na fedha.
Baada ya kupata msaada kutoka kwa majirani, alikimbizwa hospitalini ambako alishonwa majeraha sehemu mbalimbali za mwili na kufanyiwa kipimo cha CT Scan, huku majibu yakitarajiwa kutoka leo.
Mkwinda ametoa wito kwa mamlaka husika kuchukua hatua madhubuti dhidi ya vitendo vya kihalifu vinavyoendelea kushamiri mitaani.
Kijana dereva wa bodaboda Brown Anthony amevunja rekodi baada ya kusafiri kutoka Mbeya hadi Dar es Salaam kwa saa 10 tu akitumia pikipiki aina ya Boxer 150 HD (MC 473 FKT).
Safari hii ilianza kama ubishani wa kawaida kati yake na bodaboda mwenzake Alex Ndile tarehe 14 Januari 2026, wakibishana kama inawezekana kufika Dar ndani ya masaa 13. Ubishi ukawekwa kwenye makubaliano rasmi, na Brown akaamua kuthibitisha kwa vitendo.
