Author: Mbeya Yetu

Madaktari Bingwa wa Mifupa na Magonjwa yanayohusiana na Ajali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya leo wameanza kutoa huduma ya uchunguzi na matibabu ya kibingwa mkoani Manyara katika kambi maalumu ya Madaktari Bingwa ya Mifupa, Macho, pua, koo na masikio iliyoandaliwa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara, inayolenga kusogeza na kuboresha huduma kibingwa za afya kwa wananchi wa mkoa wa huo. Kwa upande wake, Dkt Baraka Mponda, Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Mifupa kutoka Rufaa ya Kanda Mbeya, amesema kuwa juhudi hizo ni sehemu ya mkakati wa Serikali na Wadau wa afya wa kuhakikisha huduma za matibabu…

Read More

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ametoa vifaa vya kusomea kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum wa Shule ya Msingi Nsalala, Halmashauri ya Mbeya. Vifaa hivyo vikiwemo kompyuta mpakato na rekoda za sauti vinalenga kuboresha mazingira ya ujifunzaji na kuhakikisha elimu bora kwa usawa. Akikabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Bi. Erica Yegera, amesema ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika utekelezaji wa sera ya elimu jumuishi.

Read More

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, ametembelea Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru mkoani Arusha na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa chuoni hapo, ikiwemo ujenzi wa jengo la Utawala, kituo cha uhifadhi wa machapisho yanayohusu wanawake, mabweni ya wanafunzi pamoja na Kituo cha Ubunifu wa Kidigitali na Huduma Tandaa (JODIC). Akizungumza mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la Utawala, Mhe. Mahundi amesema serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya vyuo vya maendeleo ya jamii ili kuimarisha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia, sambamba na kuongeza ufanisi…

Read More

Mkazi wa eneo la Soweto, jijini Mbeya, Rashidi Mkwinda, ambaye ni mwandishi wa habari wa Mbeya Yetu Online TV, amesimulia tukio la kuvamiwa na kupigwa kichwani na watu wanaodhaniwa kuwa vibaka majira ya saa sita usiku.

Amesema alikuwa akirejea nyumbani baada ya kudownload faili kwenye kompyuta, ndipo alipofuatwa na watu hao na kushambuliwa wakati akifungua geti la nyumba yake. Katika tukio hilo alipigwa mara kadhaa kichwani, akaanguka chini na kupoteza fahamu kwa muda, kisha kuibiwa simu ya mkononi pamoja na fedha.

Baada ya kupata msaada kutoka kwa majirani, alikimbizwa hospitalini ambako alishonwa majeraha sehemu mbalimbali za mwili na kufanyiwa kipimo cha CT Scan, huku majibu yakitarajiwa kutoka leo.

Mkwinda ametoa wito kwa mamlaka husika kuchukua hatua madhubuti dhidi ya vitendo vya kihalifu vinavyoendelea kushamiri mitaani.

Read More

Kijana dereva wa bodaboda Brown Anthony amevunja rekodi baada ya kusafiri kutoka Mbeya hadi Dar es Salaam kwa saa 10 tu akitumia pikipiki aina ya Boxer 150 HD (MC 473 FKT).

Safari hii ilianza kama ubishani wa kawaida kati yake na bodaboda mwenzake Alex Ndile tarehe 14 Januari 2026, wakibishana kama inawezekana kufika Dar ndani ya masaa 13. Ubishi ukawekwa kwenye makubaliano rasmi, na Brown akaamua kuthibitisha kwa vitendo.

Read More

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge, ameanza kutatua kero ya barabara katika Kata ya Iyela, mitaa ya Iyela na Pambogo, kwa kuagiza kumwagwa kwa vifusi kufuatia malalamiko ya muda mrefu ya wakazi wa maeneo hayo. Hatua hiyo inalenga kuboresha hali ya barabara na kurahisisha shughuli za kijamii na kiuchumi za wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mbunge, Katibu wa Mbunge Hakimu Edward alisema zoezi la kumwaga vifusi ni utekelezaji wa maelekezo ya moja kwa moja ya Mbunge Mwalunenge, ikiwa ni sehemu ya ahadi zake za kisiasa na mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa vitendo.

Read More