Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Maelfu ya wana CCM Mbeya Wamiminika Songwe Kumlaki Dkt. Samia—Wavutiwa na Uongozi Wake wa Kipekee
- Nilivamiwa na Uchawi Kila Usiku Hadi Nilipopata Kinga Iliyowafanya Wachawi Washindwe Kunitazama Machoni
- TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA YA NYAKASUNGWA JIMBO LA BUCHOSA
- RC Malisa Azindua Wodi ya Watoto Wachanga Hospitali ya Meta Mbeya kwa Ushirikiano wa IHI na NEST360 Tanzania
- Nilivyolipizwa Kisasi na Aliyeniumiza Baada ya Kunitendea Vibaya, Sasa Anaomba Msamaha Kila Siku
- Nilivyomrudisha Mume Wangu Baada ya Miaka Mitatu ya Kuachana, Sasa Hachoki Kuniambia ‘You’re My Destiny
- Madaktari Walishangaa Nilivyopona Maradhi Ambayo Walikuwa Wamesema Hayatibiki
- Nilivyomfanya Mume Wangu Kusema ‘Baby Siwezi Tena’
Author: Mbeya Yetu
Mgombea Udiwani Kata ya Chokaa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya Joshua Mlambalala amefikisha maombi ya minara ya mawasiliano kwa Kijiji cha Mapogolo Kata ya Chokaa mbele ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi Mbunge mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya kutokana na umuhimu mkubwa kibiashara hasa Wachimbaji wa madini ya dhahabu eneo hilo.
Mlambalala amefikisha kilio hicho kwenye kampeni za Urais, Ubunge na Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) zilizofanyika Kata ya Chokaa mgeni rasmi akiwa ni Mhandisi Maryprisca Mahundi.
Akijibu maombi hayo Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema suala hilo lipo ndani ya uwezo wake hivyo anawaagiza wataalam haraka iwezekanavyo ili kuwaondolea kadhia wananchi wa Mapogolo.
Akiomba kura Urais, Ubunge na Udiwani Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan imefanya maendeleo makubwa hivyo kuna kila sababu ya kukipa kura Chama Cha Mapinduzi.
Aidha amesema wananchi wajitokeze kupiga kura kumchagua Masache Kasaka nafasi ya Ubunge na Joshua Mlambalala nafasi ya Udiwani ili kutimiza mafiga matatu kwa maendeleo ya Kata,Wilaya na nchi kwa ujumla.
Uchaguzi mkuu utatamatisha oktoba 29 mwaka huu ambapo Mhandisi Maryprisca Mahundi ameendelea kuomba kura maeneo mbalimbali nchini.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi ( CCM) Dkt. Tulia Ackson, ameendelea na Kampeni Zake za Kuomba ridhaa kwa Wananchi wa Jimbo hilo kumchagua kwa kura nyingi kwa nafasi yake ya Ubunge na kura nyingi kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya Urais katika Uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 ili wakaendelee kutatua Changamoto zinazowakabili ikiwemo upatikanaji wa Soko la Kisasa ndani ya Mtaa wa Ituha Kata ya Ilomba. Akizungumza mbele ya Wananchi wa kata ya Ilomba Katika Mitaa wa Ituha leo tarehe 23 Septemba, 2025 , Dkt. Tulia amesema Chama Cha Mapinduzi…
Mgombea Ubunge Jimbo la Uyole kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Tulia Ackson, leo Septemba 23, 2025 amefanya mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Ndugunya (Isoso) vilivyopo Kata ya Mwasanga, Jijini Mbeya. Katika mkutano huo uliovuta mamia ya wananchi, Dkt. Tulia amenadi sera za Chama Cha Mapinduzi huku akisisitiza mshikamano, mshikikiano na mshirikiano katika utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2025 – 2030. Amewataka wananchi wa Kata ya Mwasanga na Jimbo zima la Uyole kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi ifikapo Oktoba 29, 2025 kushiriki uchaguzi mkuu kwa kuwapigia kura wagombea wote wa CCM kuanzia ngazi ya Udiwani, Ubunge hadi…
Mbunge mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ameibukia Soko la Uhindini lililopo Kata ya Chokaa Wilaya ya Chunya Mkoani kwa lengo la kukutana na Wanawake wajasiriamali wanaofanya biashara katika Soko hilo.
Aidha amewatia moyo na kuwahimiza kumiliki uchumi wao sanjari na kujiunga pamoja ili waweze kunufaika na mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri.
Aidha Mahundi ametumia fursa hiyo kuzisaka kura za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, Mbunge na Diwani ili kuendeleza maendeleo nchini.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Uyole, Dkt. Tulia Ackson, amewaomba wananchi wa Uyole kumpigia kura za kishindo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 ili aweze kuwaletea maendeleo ya haraka. Dkt. Tulia ametoa ombi hilo leo tarehe 22 Septemba, 2025 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Nsalaga mkoani Mbeya katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Itezi kwa lengo la kunadi sera za CCM kuelekea Uchaguzi mkuu. Amesema kuwa Jimbo la Uyole linayo mahitaji mengi ya msingi ambayo watu pekee na sahihi…
Leo nimekuja mbele yenu nikiwa na ari na msisimko wa kweli. Nitumieni nikafanye kazi kwa ajili yenu na kwa ajili ya maendeleo ya Jimbo la Mbeya Mjini.
Nataka tushirikiane kubadilisha Mkoa wa Mbeya – tubebe pamoja ajenda ya maendeleo kwa tabasamu na mshikamano. Nina afya, nina nguvu, nina ujuzi na ubunifu. Nina dhamira thabiti ya kusimamia na kulinda maslahi ya wananchi wa Mbeya.
Nikiwa mgombea wa Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), naomba tushirikiane katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29. Naomba kura zenu kwa ajili ya Rais wetu mpendwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kura kwa ajili yangu kuwa Mbunge wenu, na kura kwa Diwani wa CCM.
Tukiwa pamoja, tutaendelea kusonga mbele. Nitumieni nikafanye kazi.
Asanteni sana.
Mbunge Mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Mh. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amezindua kampeni za CCM Kata ya Mbugani, Wilaya ya Chunya, ambapo aliwaomba wananchi kumpa kura za heshima Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Ubunge Jimbo la Lupa Masache Kasaka na Mgombea Udiwani Bosco Mwanginde. Mahundi alisema Dkt. Samia ni kiongozi shupavu aliyeendeleza miradi ya awamu ya tano na kuanzisha mipya kwa manufaa ya wananchi. Naye Bosco Mwanginde aliwashukuru wanachama kwa kumchagua na kuwataka kushirikiana naye katika kuwaletea maendeleo.