Author: Mbeya Yetu

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amesema kuwa ni wajibu wa kila mtanzania kuhakikisha anailinda kwa wivu wote tunu ya Muungano iliyoanzishwa na waasisi wa taifa hilo. Dkt. Tulia ameyasema hayo leo tarehe 25 Aprili 2025 wakati akizungumza na wananchi wa wa Mkoa wa Pwani wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika stendi ya Kibaha ikiwa ni sehemu ya shughuli za Maadhimisho ya Miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mara baada ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyofanyika katika mkoa huo. Kiupekee, Dkt.…

Read More

Umoja wa Machinga wa eneo la Old Airport katika Jiji la Mbeya wamemchangia Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson, kiasi cha shilingi milioni moja (1,000,000/=) ili aweze kuchukua fomu ya kugombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kufuatia chama hicho kutangaza tarehe rasmi za kuchukua fomu.

Fedha hizo zimekabidhiwa kwa Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Dormohamed Issa, ambaye alimwakilisha Dkt. Tulia katika hafla hiyo ya makabidhiano.

Read More

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYAUWSA) imefuta madeni ya wateja wa kata ya Mwasenkwa waliokuwa wakitumia mradi wa maji wa kijiji na kushindwa kulipa ankara kwa muda mrefu.

Uamuzi huo umetangazwa wakati wa uzinduzi wa mradi mpya wa kisima kirefu chenye uwezo wa kuzalisha lita 720,000 za maji kwa siku, utakaohudumia wakazi zaidi ya 2,800. Mradi huu unaleta huduma ya maji kwa masaa 24.

Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson, alizindua mradi huo na kuhimiza wananchi kupanda miti rafiki kwa vyanzo vya maji ili kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka.

Read More