Author: Mbeya Yetu

Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam Aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene, pamoja na mpiga picha wa zamani wa Rais, Ikulu, Fredrick Maro, wamekabidhiwa rasmi Vitambulisho vyao vya Uandishi wa Habari (Presscard) leo tarehe 07 Agosti 2025, baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria. Zoezi hilo limefanyika katika Ofisi za Bodi zilizopo Mtaa wa Jamhuri, jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula. Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi vitambulisho hivyo, Wakili Kipangula alibainisha kuwa Mwambene na Maro wamefuata utaratibu wa kisheria,  ikiwa ni pamoja na kujisajili,…

Read More

#Aipongeza kwa kuwafungulia barabara wakulima Dodoma Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Bi. Asia Messos ameipongeza Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa ujenzi wa miundombinu ambayo imeweza kuwasaidia wakulima kusafirisha mazao yao kwa wakati. Ameyasema hayo mara baada ya kutembelea banda la TARURA kwenye Maonesho ya NaneNane Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma. Amesema kwamba kazi kubwa imefanyika katika maeneo mengi na hivyo wameweza kuwarahisishia wakulima kusafirisha mazao yao kwa wakati na kufikisha kwenye masoko. “Niwapongeze sana TARURA kwa kazi kubwa mnayoifanya vijijini,sisi ni mashahidi katika maeneo yetu,wakulima wanaweza kusafirisha mazao na bidhaa zao…

Read More

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema kuwa zaidi ya wakulima 18,000 wanatarajiwa kunufaika moja kwa moja na Mpango wa Taifa wa Kilimomisitu ifikapo mwaka 2031, ambao unalenga kuhakikisha wakulima milioni 15 wanatumia teknolojia na mbinu bora za kilimomisitu nchini. Mkakati huo uliozinduliwa mwaka 2024 na Mhe Dkt. Philipo Isdori Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umejikita katika kuendeleza kilimomisitu nchini, ikiwa na dhima ya kukuza ufanisi wa mbinu za kilimomisitu na teknolojia zake ili ziweze kutumika na jamii ya wakulima kwa ajili ya kudumisha ustawi wa jamii, uchumi na mazingira. Akizungumza…

Read More

Ujumbe wa Bodi ya Shirika la Kimataifa la Helen Keller tarehe 5 Agosti, 2025 pamoja na masuala mengine ulifika Isman Wilaya ya Iringa kujionea kwa vitendo zoezi linaoendelea la kambi ya upasuaji wa ugonjwa wa macho ujulikanao kama mtoto wa jicho kambi itakayo toa huduma hiyo kwa siku saba. Akiongea wakati wa kikao kifupi ofisi ya mkuu wa mkoa mkoani Iringa kabla ya kutembelea kituo hicho, Rais wa shirika hilo Sarah Bochie amesema shirika hilo limeamua kutembelea mkoani Iringa ili kujionea na kujiridhisha huduma zinazotolewa kwa vitendo kwani shirika lake linafanya kazi kwa kanzi data na takwimu ili kutoa tathimini…

Read More