Author: Mbeya Yetu

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Vunja nazi, Omary Mngwali kutoka Wilayani Mafia mkoani Pwani  akimuonesha Mwenyekiti wa Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele orodha yawatu wasio stahili kuwepo kwenye Daftari.  Mwenyekiti wa Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akitazama Mwandikishaji Msaidizi katika Kituo cha Kata ya Kilindoni kilichopo Shule ya Msingi Kilimani akichukua taarifa za watu waliopoteza sifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa Vunja nazi, Omary Mngwali wakati Mwenyekiti wa Tume alipotembelea vituo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mkoani Pwani leo Mei 16, 2025…

Read More

Na Woinde Shizza, Arusha Serikali imepiga kengele ya tahadhari kufuatia ongezeko la madai feki ya bima yanayodaiwa kuisababishia nchi hasara ya mabilioni, huku ikiweka wazi kuwa asilimia 10 hadi 15 ya madai hayo duniani yana chembechembe za udanganyifu. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Dk. Sada Mkuya, amesema hali hiyo imeifanya sekta ya bima kupoteza uaminifu wa umma na kuathiri utoaji wa huduma kwa wateja wa kweli wanaohitaji msaada halali. Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, wakati wa mkutano wa wataalamu wa udhibiti wa udanganyifu wa bima (IASIU), Dk. Sada alisema baadhi…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza na Watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ambayo yanahusisha waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki kutoka Kata zote za Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani. Zoezi la uboreshaji awamu ya pili linataraji kuanza Mei 16 hadi 22, 2025 sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la Wapiga Kura na vituo vitafunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 12:00 jioni.  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.…

Read More

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amesema kuwa Wizara inaendelea kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Polisi katika kukabiliana na vitendo vya utapeli mtandaoni, hasa vinavyofanyika kupitia huduma za simu na miamala ya kifedha (SimBanking). Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Fakharia Shomari Khamisi (Mb.), katika kikao cha Bunge kilichofanyika jijini Dodoma, Mhandisi Mahundi alisema ongezeko la matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) limeleta manufaa makubwa kwa taifa katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa, huku pia likizua changamoto mbalimbali ikiwemo uhalifu wa mtandaoni. Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka…

Read More