Browsing: Video Mpya

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba leo Novemba 17, 2025 amekabidhiwa Ofisi na Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa, Mlimwa Jijini Dodoma Novemba 17, 2025.

Viongozi waliohudhuria hafla ni pamoja na Naibu Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Doto Biteko, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi, Wakuu wa Idara na watumishi wengine wa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Taasisi ya Tulia Trust iliyo chini ya Mbunge wa jimbo la Uyole jijini Mbeya Dkt Tulia Ackson, wameanza ujenzi wa nyumba ya famikia ya mzee Anyomwisye Mwalyaje mkazi wa mtaa wa Mwafute kata ya Ilemi iliyoteketea kwa moto usiku wa September 5 kutokana na hitilafu kwenye mfumo wa Umeme.

Ujenzi huo umeanza baada ya Mbunge wa jimbo la Uyole kutoa ahadi ya kumjengea nyumba mzee Anyomwisye Mwalyaje alipomtembelea kutokana na kadhia ya nyumba yake kuteketea kwa moto pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani.

Afisa kutoka taasisi ya Tulia Trust kitendo cha habari Addi Kalinjila amesema ujenzi wa nyumba hiyo unaanza maramoja baada ya vifaa kufika eneo la ujenzi ili kurejesha maisha ya familia hiyo kama yalivyokua hapo awali.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 15, 2025 amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. “ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, kama duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.”

Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.

Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. “Ujauzito sio suala la dharura vifaa kama ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.”

Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya.