Browsing: Video Mpya

DKT TULIA ACKSON:”Kwanza kabisa nichukue fursa hii kutoa pole kwa dhati. Sisi ni sehemu ya wananchi ambao tuliathirika na tukio lililotokea, na kama ilivyoelezwa vizuri na Sheikh wa Mkoa, sitarudia kwa kirefu. Lakini nitoe pole zangu za dhati kwa wananchi wenzangu wa Mbeya, Uyole, na Watanzania wote kwa ujumla, kufuatia tukio lililolikumba Taifa letu tarehe 29 Oktoba”.

”Wakati huohuo, baada ya dua na maelezo yaliyotolewa, nitoe pole pia kwa wananchi wenzetu waliopoteza maisha, na niwatakie uponaji wa haraka wale wote waliojeruhiwa.

Nichukue fursa hii pia, Mheshimiwa Waziri Mkuu, kukukaribisha mkoani Mbeya, lakini kwa ziara hii maalum, nitoe pole kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa changamoto iliyotokea, ambayo pia imekupa fursa ya kutembelea miundombinu mbalimbali ya umma na mali za wananchi zilizopata athari”.

*DKT. MWIGULU AMBANA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KITAI-RUANDA*

_Aaagiza kukamatwa kwa hati yake ya kusafiria hadi atakapokamilisha ujenzi_

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kumsimamia vema mkandarasi anayejenga barabara ya Kitai hadi Ruanda ili aweze kuendana na kasi iliyotarajiwa.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema tayari Serikali ilikwishalipa fedha za ujenzi wa barabara hiyo kwa kutambua umuhimu wake kwenye uchumi wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla.

📍Songea-Tanzania
🗓️Desemba 16, 2025

kuu wa Mkoa wa Mbeya, Benno Malisa, amewataka watumishi wa taasisi za serikali Nyanda za Juu Kusini kulinda kwa wivu rasilimali za taifa kwa kutumia ipasavyo maendeleo ya teknolojia, ili kutimiza adhima ya serikali ya kupata thamani halisi ya fedha katika manunuzi ya umma.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Mfumo wa NesT, yanayojumuisha moduli mpya za majadiliano, uandaji na usimamizi wa mikataba, Malisa amesema usimamizi usioridhisha wa mikataba ni miongoni mwa changamoto kubwa zinazokwamisha upatikanaji wa thamani ya fedha katika ununuzi wa umma.

Amesisitiza kuwa matumizi sahihi ya mifumo ya kidijitali yataongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika michakato ya ununuzi, sambamba na kupunguza mianya ya upotevu wa fedha za umma.

Kwa upande wake, Meneja wa PPRA Nyanda za Juu Kusini, Pascal Manono, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuweka uwazi katika hatua zote za ununuzi, kuanzia mchakato wa zabuni hadi usimamizi wa mikataba, kwa kutumia moduli mpya zilizoboreshwa ndani ya mfumo wa NesT.

Nao washiriki na wawezeshaji wa mafunzo hayo wamesema kuwa uelewa walioupata kuhusu matumizi ya moduli mpya utawasaidia kuboresha utendaji kazi wao na kutoa huduma kwa wananchi kwa weledi, ufanisi na kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji.