Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Badili upepo wa Biashara Yako Hadi Mafanikio
- Watumishi wazembe hawatakuwa na nafasi-Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba
- Dkt. Mwigulu: “Mabasi ya Esther Yamechomwa Wakidhani Ni Yangu”
- Mama Dkt. Samia Atua Arusha atoa neno
- Mbinu ya kupata faida katika biashara ya samaki, uvuvi
- WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUZUIA HATI YAKE
- Mgombea Umeya Jiji la Mbeya, Noah Mwakisu Arejesha Fomu; Aahidi “Ukombozi wa Jiji”
- MVUA ILIYONYESHA LUMBILA IWAMBI MBEYA MITARO YAFURIKA MAKAZI YA WATU YAJAA MAJI BIASHARA ZASIMAMA
Browsing: Video Mpya
MAMIA WAMPOKEA DKT. SAMIA ARUSHA, ASISITIZA UMUHIMU WA AMANI NCHINI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amewashukuru wananchi wa Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kwa imani kubwa waliyompatia katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akiahidi kurejea tena Mkoani Arusha kutoa shukrani zake kwa wananchi.
Dkt. Samia amebainisha hayo leo Ijumaa Novemba 21, 2025 alipotua katika Uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) na kuzungumza na mamia ya wananchi waliofika uwanjani hapo Kumpokea, akianza ziara yake ya siku mbili Mkoani Arusha.
Katika salamu zake Rais Samia amesisitiza kuhusu umuhimu wa amani kwa ustawi na maendeleo ya Watanzania, akisisitiza wananchi kutotoa fursa katika kuharibu amani na kuwasihi Wazazi na walezi kuzungumza na Vijana wao pia kuhusu umuhimu wa kutunza amani ya Tanzania.
“Niwashukuru sana kwa kuendelea kuiweka mikoa hii kuwa salama. Usalama upo, kazi zinaendelea na mambo yetu yote yanaendelea. Niwaombe sana amani pekee ndiyo tumaini letu, uhai wetu ni amani yetu sasa niwaombe sana tusitoe fursa ya kuharibu amani yetu.” Amesema Rais Samia.
Rais Samia pia ametoa wito kwa wazazi na walezi kuzungumza na watoto wao kuhusu amani, akisema anafahamu kuwa matukio ya uvunjifu wa amani ya Oktoba 29, 2025 Vijana wengi walifuata mikumbo, akisema ni muhimu kuilinda amani kwani masuala ya uvunjifu wa amani si masuala ya kufanyia majaribio nchini.
Rais Samia yupo Mkoani kwa ziara ya siku mbili ambapo kesho Jumamosi Novemba 22, 2025 anatarajiwa kutunuku Kamisheni na Shahada ya Sayansi ya Kijeshi kwa Maafisa wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli Mkoani Arusha.
Diwani wa Kata ya Ilomba, Ndg. Noah Edson Mwakisu, leo amerejesha fomu za kuwania Umeya wa Jiji la Mbeya kupitia CCM. Akizungumza katika Ofisi za CCM Mbeya Mjini, Mwakisu alisema anagombea nafasi hiyo ili kulipa jiji mwelekeo mpya wa maendeleo, akisisitiza umuhimu wa uongozi wenye maono, ushirikiano na uwajibikaji.
Mwakisu alisema Mbeya ina fursa kubwa za kimaendeleo kutokana na mazingira na jiografia yake, hivyo inahitaji kiongozi anayeendana na mahitaji ya kizazi cha sasa, hususan vijana ambao ndio nguvu ya uchumi wa jiji. Aliomba sapoti na baraka za wananchi, akiahidi kulifanya jiji hilo mfano wa kuigwa endapo atapewa dhamana.
Kurejesha fomu hizo kunamweka rasmi katika kinyang’anyiro cha ndani ya CCM cha kuwania Umeya wa Jiji la Mbeya mwaka huu.
#mbeyayetutv
Mvua iliyonyesha kwa takribani saa moja Novemba 20 2025 Mtaa wa Lumbila Kata ya Iwambi Jijini Mbeya imeathiri makazi ya watu kutokana na mitaro kujaa maji kuingia kwenye makazi ya watu na baadhi ya sehemu za biashara.
Kijana Golden Kidumba, maarufu kama DON. G, amewagusa watoto wa mitaani kwa kuwapatia chakula, kuwanunulia nguo na kutumia muda wa siku nzima akiwa nao, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kuikumbuka jamii aliyotokea.
Golden, mzaliwa na mkazi wa zamani wa Njombe, anasema maisha magumu aliyoyapitia utotoni ndiyo yamemfanya kuwa na moyo wa huruma na kujitoa kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.
“Nimekulia kwenye maisha magumu sana. Lakini namshukuru Mungu kwa kunibariki na kunifanya niweze kuwakumbuka hawa wadogo zangu wa mitaani. Nimekula nao, nimesherehekea nao na pia nimewanunulia nguo ili wajisikie wanathaminiwa kama watoto wengine,” amesema DON. G.
Amesema kusaidia watoto wa mitaani si tukio la leo pekee, bali ni jambo alilolianza miaka kadhaa iliyopita, ikiwemo kutembelea hospitali na kuwasaidia watu wenye uhitaji.
Golden ameweka wazi kuwa ndoto yake ya baadaye ni kuanzisha taasisi ya msaada na hata kujenga shule maalum kwa ajili ya watoto hao, ili kuwapa elimu, malezi na fursa za kuanza maisha mapya.
Baadhi ya watoto wa mitaani waliopokea msaada huo wameeleza machungu ya maisha yao, ikiwemo vipigo, njaa, manyanyaso na mara nyingi kudharauliwa kama wahalifu bila kujua historia zao.
Kijana Brian Edwin, anayelelewa katika kituo cha Mtama, amesema:
“Maisha ya mitaani ni magumu. Tunapigwa, tunanyanyaswa na tunaishi bila uhakika. Lakini leo tumepata faraja kubwa kutoka kwa DON. G. Mungu ambariki.”
Wengine kama Anody Nyondo na Gifty wameeleza jinsi walivyokimbia nyumbani kutokana na migogoro ya kifamilia na manyanyaso, hali iliyowalazimu kuingia mitaani.
Watoto hao wameiomba jamii na serikali kutowatenga, bali kuwaona kama watoto wanaohitaji msaada na si wahalifu.
Golden ameendelea kutoa wito huo huo:
“Tusishikilie mali bila sababu. Tukiondoka duniani, hatuchukui chochote. Tuwakumbuke watoto wa mitaani; wanahitaji upendo na msaada wetu.”
Rais Dkt Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri Naibu Mawaziri Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu
Rais Dkt. Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu, tarehe 19 Novemba, 2025, Ikulu Chamwino, Dodoma.
