Browsing: Video Mpya

KAULI MPYA KUTOKA CCM KYELA,FEDHA ZIMETOKA AU ZIMEUNGUA ,UCHUNGUZI UNAENDELEA.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya Bw.Elias Mwanjala amejitokeza hadhara kwa mara nyingine na kutoa kauli juu ya fedha ambazo alidai kuwa zimeteketea kwa moto wakati jengo la chama hicho lilipochomwa.

Bw.Mwanjala amesema kuwa ukweli wa fedha hizo kama zimeteketea kwa moto au kuchukuliwa na yeyote wameliachia vyombo vya ulinzi na usalama liendelee na uchunguzi.

Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (Mbeya UWSA), ikiongozwa na Mwenyekiti wake Bi. Edna Mwaigomole, leo tarehe 03/12/2025 imefanya kikao cha dharula cha Kamati ya Bodi ya Fedha na Mipango kwa ajili ya kupokea na kujadili Mpango Mkakati wa Mamlaka wa mwaka 2025/2026–2029/2030 na Mpango wa Biashara wa mwaka 2025/2026–2029/2030.

Pamoja na kujadili masuala mengine ya kiutendaji ya Mamlaka, Kamati imepokea taarifa ya ununuzi wa gari maalumu kwa ajili ya shughuli za uondoshaji wa majitaka kwa wateja ambao hawajajiunga na mtandao wa majitaka.

Akitoa taarifa hiyo, CPA. Gilbert Kayange Mkurugenzi Mtendaji wa Mbeya UWSA amesema, Mamlaka ina jukumu la kutoa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira kwa Wananchi ambapo kwa upande wa usafi wa mazingira Mamlaka ilikuwa haijawafikia wateja ambao hawajajiunga katika mfumo rasmi wa majitaka. Hivyo ununuzi wa gari la kuondosha majitaka majumbani utaboresha hali ya usafi wa mazingira katika jamii.

Aidha, alieleza kuwa, Mamlaka imenunua gari aina ya Isuzu FVR34P lenye thamani ya Shilingi 497,000,400 ambalo lina uwezo wa kubeba maji lita 10,000.

Bi. Cynthia Hilda Ngoye Mwenyekiti wa Kamati ya Bodi ya Fedha na Mipango , ameeleza kuwa anafurahishwa na utendaji kazi wa Menejimenti na Watumishi wa Mamlaka kwani mipango mingi inayowekwa inatekelezwa.

Akizindua gari hilo, Bi. Edna ameeleza kuwa fedha zilizotumika kununua gari hilo ni fedha za umma, hivyo ni wajibu wa Watumishi kutoa huduma bora kwa Wananchi.

Mbeya UWSA inaendelea kutekeleza maboresho ya huduma kwa lengo la kuongeza ufanisi, usalama wa mazingira na ustawi wa wananchi wa Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kwa namna moja au nyingine kuna baadhi ya taasisi za dini zimejiingiza kwenye mkumbo ambao unaendelea wenye nia ovu ndani yake. Akieleza juu ya uongozi wa nchi katika kufuata misingi ya katiba na sheria, Rais Dkt. Samia amesema Tanzania haina dini lakini Watanzania wana dini za madhehebu mbalimbali huku akisisitiza kuwa kikatiba na sheria za nchi hakuna dini na dhehebu lolote lenye uwezo wa’kuover ride’ madhehebu mengine. Akizungumza na Wazee wa mkoa wa Dar es salaam leo tarehe 2 Disemba 2025, Rais DKt. Samia ameyasema na kuyasisitizia haya kuhusu taasisi za dini nchini “Viongozi wa dini msijivishe majoho ya kwamba nyinyi ndio mnaweza ‘kuover run’ nchi hii, hakuna. Tutakwenda kwa kwa Katiba na Sheria ya Nchi hii.” “Hatutaendeshwa na madhehebu yoyote ya dini, madhehebu ya dini na wafuasi wao” “ubora wa dini upo miyoyoni kwetu, wale wanaoamini ndio wanajua ubora wa dini yao..” “hakuna ‘over riding’ hapa! Kwamba “mimi dini yangu ndio itaover ride Tanzania na tamko nikilitoa ndio hilo hilo”. “…hata wenyewe wanatofautiana, mimi toka nimekaa matamko 8 yametolewa na TEC, lakini ukienda chini chini wenyewe wanapingana, matamko yale hayafanyi kazi…waliosimama kwenye mstari wa haki wanaona ni batili iliyofanyika..hawaungani nao..” “Tanzania yetu ni nchi ya umoja na mshikamano, amani na utulivu ndio ngazo zetu, tusivurugwe ndugu zangu