Browsing: Video Mpya

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Furaha Mwile Nyelele, mkazi
wa Kijiji cha Shilanga kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wa jirani yake
aliyekuwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Shilanga darasa la saba
aitwaye Boniventure Elia Lazaro [12] mkazi wa Shilanga.
Awali kabla ya tukio hilo tarehe 21.12.2025 saa 10:15 jioni huko Kijiji cha
Shilanga, Kata ya Ilembo, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Mbeya Vijijini
mtuhumiwa Furaha Mwile Nyelele alimpiga kwa kipande cha mti kichwani
mtoto Boniventure Elia Lazaro [12] ambaye kwa sasa ni marehemu na
kumsababishia jeraha ambapo alikimbizwa katika Hospitali Teule ya Ifisi
kwa matibabu.
Tarehe 22.12.2025 saa 6:30 mchana akiwa anaendelea kupatiwa matibabu
katika Hospitali Teule ya Ifisi alifariki dunia. Uchunguzi wa awali umebaini
kuwa chanzo cha tukio hili ni kujichukulia sheria mkononi baada ya
mtuhumiwa kumtuhumu mtoto kuiba mayai ya kuku.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa kwa jamii kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi ili kuepuka madhara. Aidha, wazazi na walezi
wanakumbushwa kuzingatia suala la ulinzi na usalama wa mtoto kwa
kuhakikisha haki za mtoto zinaheshimiwa na kulindwa.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.

Mbunge wa Jimbo la Uyole, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson (@tulia.ackson), ameendelea kutoa sadaka kwa familia zisizo na uwezo katika kipindi cha kuelekea sikukuu ya Krismasi kwa kutoa chakula na fedha.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Dkt. Tulia amesema ushirikiano mzuri kati ya viongozi wa mitaa na wananchi ndiyo umefanikisha kuwatambua walengwa sahihi, akibainisha kuwa leo ilikuwa zamu ya Kata ya Ilemi, ambapo kaya 13 zimenufaika, huku jumla ya kaya 130 zikitarajiwa kupata msaada huo katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Uyole.

Ameongeza kuwa zoezi hilo ni endelevu na litaendelea katika kata nyingine kadri ratiba itakavyoruhusu, kwa lengo la kuwafikia wananchi wenye uhitaji mkubwa zaidi.

Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Mathew Kundo ametembelea chanzo cha maji mto Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya ambacho kimefikia asililimia tisini na nane huku akisema zaidi ya shilingi bilioni nne zimetolewa na Serikali kuendeleza mradi huo pamoja na kutoa wito kwa wananchi kutunza chanzo cha maji ili mradi uweze kufanya kazi kwa muda mrefu. Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYAUWSA) amesema mradi huo utakuwa na ujenzi wa chanzo cha maji, bwawa la kutibu maji,utandazaji wa mabomba na tanki la kusambazia maji.

Website: https://sabbysabs.com/
Patreon: https://www.patreon.com/SabrinaSalvati
PayPal: https://paypal.me/sabbysabspodcast?locale.x=en_US
Merch: https://www.bonfire.com/store/sabby-sabs/
Newsletter: https://sabbysabs.substack.com/
Sabby Sabs Discord: https://discord.gg/bZaB7SJz5E
Rokfin: https://www.rokfin.com/SabbySabs
Odysee: https://odysee.com/@SabbySabs:e?order=new
Rumble: https://rumble.com/c/c-1572375
Ritual Network: http://ritualnetwork.com/
Anime Sabby artwork credit: By Diva’sDoodles by Yvonne J.
Intro Song: Sabby Sabs Intro – Do Bee Doo by Jesse Jett – Copyright ยฉ @Song Secure 2023.
Intro Video: Kesheev

Please LIKE and SUBSCRIBE!

Contact Me:
Business Inquiries: [email protected]
General contact: [email protected]

Follow me on Twitter: @SabbySabs2
Follow me on Telegram: https://t.me/boost/sabbysabspod
Follow me on Instagram! https://www.instagram.com/sabbysabs4u/
Spotify & iHeart Radio: Sabby Sabs
Facebook: Sabby Sabs Podcast

#mitscientist #sabbysabs #brownuniversitysuspect #kashpatel #gavinnewsomnews #katiemiller #chriscuomo #geopoliticsinconflict #trumpaddressingthenation