Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Nilivyopata Amani Baada ya Miaka ya Kukosa Usingizi na Huzuni Usiku Kila Usiku
- Nilivyopata Furaha Baada ya Kuachana na Marafiki Walionivuta Chini
- Child Support Tanzania Yashirikiana na Madiwani Kuimarisha Elimu Jumuishi Mbeya
- Child Support Tanzania Yawawezesha Madiwani Mbeya Kuhusu Elimu Jumuishi
- MAKALA: PARADISE MISSION BUSTANI YA TAALUMA KWA WANAFUNZI NCHINI NDELE MWASELELA AONESHA UWEZO WAKE
- Nilivyorejesha Uhuru Wangu Kitandani Baada ya Miaka ya Kuishi Bila Hamu Wala Hisia
- Nilivyopambana na Baby Mama Aliyenigeuza Mfadhili Pekee Bila Haki, Mpaka Hatimaye Nikaweza Kuwa Karibu na Watoto Wangu Tena
- NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya
Browsing: Video Mpya
Child Support Tanzania imeendesha kikao na madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya kupitia Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa Elimu Jumuishi, hususan kwa watoto na watu wenye ulemavu.
Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Child Support Tanzania, Bi. Noela Msuya Shawa, amesema kupitia mradi wa Sauti Zetu unaofadhiliwa na Oxfam na kutekelezwa kwa ushirikiano na AkiElimu, madiwani wamepatiwa mafunzo kuhusu Mpango Mkakati wa Taifa wa Elimu Jumuishi, miongozo yake na wajibu wao katika kuhakikisha utekelezaji wake kwa ubora katika shule za kata zao.
Kwa upande wao, madiwani wamesema mafunzo hayo yamewajengea uelewa mpana kuhusu masuala ya watoto na watu wenye ulemavu. Mh. Juma Samson Simbeange, Diwani wa Kata ya Nsoho, amesema atahakikisha masuala ya watoto yanapewa kipaumbele wakati wa kupitisha bajeti za Halmashauri ili kuwasaidia watoto wanaohitaji msaada maalum.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Mhe. Patali Shida Patali, amesema Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 250 kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Igyoma–Ilambo (takribani km 9), ambapo mkandarasi tayari ameanza kazi ili kuwezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za kiuchumi.
Amesema pia fedha zimetolewa kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya Isionje–Kikondo ambayo imekuwa na changamoto kubwa wakati wa mvua, huku mkandarasi akiwa tayari eneo la kazi na hali ya barabara ikionekana kuimarika ikilinganishwa na miaka iliyopita.
Akizungumzia changamoto ya barabara iliyo karibu na Shule ya Maadilisho Irambo, Mhe. Patali amesema hakuna mgogoro bali kuna taratibu za kisheria zinazohitajika kufuatwa baada ya barabara hiyo kuhamishwa kutoka TARURA kwenda TANROADS, na kuomba mamlaka husika kuharakisha mchakato huo kwa manufaa ya wananchi.
Kauli hiyo ilitolewa wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, katika Shule ya Maadilisho Irambo mkoani Mbeya.
Wazee wanaoishi katika Makazi ya Wazee na wasiojiweza Bukumbi, wilayani Misungwi mkoani Mwanza, wameishukuru Serikali kwa kuimarisha huduma za ustawi wao, wakisema hatua hiyo imeleta faraja, heshima na matumaini mapya katika maisha yao ya uzeeni.
Mwenyekiti wa Wazee kituoni hapo, Mzee John Nguku amesema wazee wanathamini jitihada Serikali za kuwapatia huduma muhimu kwa wakati.
“Kwa niaba ya wazee wenzangu, tunaishukuru Serikali kwa kutukumbuka tunaishi kwa amani, tunahudumiwa kwa heshima na tunahisi bado tuna thamani katika jamii, tunaomba uangalizi huu uendelee ili wazee wengi zaidi wanufaike maana uzee siyo mzigo bali ni neema”. amesema Mzee John
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali inawatambua wazee kama tunu muhimu ya Taifa na itaendelea kuimarisha huduma za ustawi na ulinzi wao.
Mhe. Mahundi amesema pamoja na jitihada za Serikali, jamii ina wajibu wa msingi wa kuwatunza wazee, huku akiwataka vijana kutowasahau wazazi wao wanapofikia uzee na kuhakikisha wanapata upendo, heshima na msaada unaostahili.
“Nawasihi vijana na jamii kwa ujumla, msije mkawasahau wazazi wenu wanapofikia uzee. Kuwatunza wazee ni wajibu wa familia na ni sehemu ya maadili yetu ya Kitanzania, Serikali itaendelea kuhakikisha wazee wanathaminiwa, wanalindwa na wanapata huduma stahiki bila kubaguliwa. Tunazitaka familia, vijana na jamii kwa ujumla kutambua kuwa kuwajali wazee ni wajibu wa kimaadili na msingi wa ustawi wa Taifa letu” amesema Mhe. Mahundi.
Kwa upande wake, Mfawidhi wa Makazi ya Wazee na wasiojiweza Bukumbi, Vivian Kaiza amesema uangalizi wa Serikali na ushirikiano wa wadau umeendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wazee waliopo kituoni hapo, Makazi yanaendelea kusimamiwa kwa weledi na kujali maslahi ya wazee, huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki na kuishi kwa amani.
Ziara hiyo ni mwendelezo wa dhamira ya Serikali katika kuimarisha ustawi wa wazee, huku jamii ikihimizwa kushirikiana na Serikali katika kuwatunza wazee ili waishi maisha yenye heshima, upendo na matumaini.
