Browsing: Video Mpya

Maafisa Usafirishaji maarufu kama Bodaboda Mkoani Iringa wamelaani kitendo cha baadhi ya vijana kukubali kushawika na kushiriki kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kisingizio cha kwamba ni maandamano ya amani.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 11, 2025 na kundi hilo la vijana ambapo wameonyesha kutofurahishwa na vitendo viovu ikiwemo uchomaji wa miundombinu mbalimbali jambo ambalo linapelekea kudhorota kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Meya wa Jiji la Mbeya, Dourmohamed Issa, ameonyesha kukerwa na kasi ndogo ya ujenzi wa soko la Tandale na stendi, akisema mradi umesimama licha ya mkandarasi kuongezewa muda mara kadhaa.

Amesema mradi huo ulipaswa kukamilika mwezi Agosti, lakini hadi sasa — Desemba — kazi haijaonyesha maendeleo, huku mkandarasi akitoa sababu dhaifu kama ukosefu wa vifaa.

Meya Issa amesema serikali tayari imetoa zaidi ya bilioni 12, hivyo hakutakiwi kuwe na visingizio, na ametaka kasi iongezeke mara moja vinginevyo hatua kali zitachukuliwa.