Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi- Arusha
Ikiwa leo ni Machi 08,2024 kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani, Mtaandao wa
Polisi Wanawake Mkoa wa Arusha wameunga na wanawake wengine Mkoani humo huku
Mtandao huo wakiitumia siku hiyo kuwawekea akiba ya fedha katika mfuko wa uwekezaji (UTT)
kwa Watoto wawili wa askari wanandoa waliofariki kwa ajali ya gari.
Akiongea katika Viwanja vya Ngarenaro Complex Jijini Arusha Mwenyekiti wa Mtandao huo
Mkoa wa Arusha Mrakibu mwandamizi wa Polisi SSP Zauda Mohamed amesema mtaandao huo
katika kuelekea kilele hicho ulianza mapema kutoa elimu maeneo mbalimbali Pamoja na
kufanya ibada ya kuwaombea marehemu.
SSP Zauda ameongeza kuwa katika kuadhimisha siku hiyo waliona vyema kuunga na
kuwawekea akiba ya fedha kwa Watoto wa askari wanandoa waliofariki katika ajali ya gari
ambapo amebainisha kuwa fedha hizo zitawasaidia Watoto hao katika swala la elimu na
mahitaji mengine ya kibinadamu.
Aidha ametoa wito kwa wanawake wengine Mkoani humo kufanya kazi kwa bidii,nidhamu na
kutenda haki ili ustawi bora na wajikwamue kiuchumi na maendeleo ya Taifa kwa Ujumla.
Nae mrakibu msaidizi wa Polisi Lucy Teesa kutoka Makao Makuu ya kikosi cha Kuzuia wizi wa
Mifugo STPU amewaomba wanaweka wenzake kushiriki vyema katika mapambano dhidi
uhalifu ambapo amewaomba kutoa taarifa za uhalifu na kujikitaa katika malezi bora ya Watoto
ili kujenga Jamii iliyostarabika.
Kwa upande wake Mkuu wa kituo cha Polisi Wilaya ya Kipolisi Murieti Mrakibu msaidizi wa Polisi
ASP Tausi Mbalamwezi amewaomba wanawake wenzake kujiamini na kujituma katika
kutekeleza majukumu yao huku akiwaomba kuumuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuliinua taifa kiuchumi.
Trending
- Dkt. Tulia Aongoza kwa Vitendo, Apiga Kura na Kuhamasisha Ushindi wa CCM Uyole
- DKT MARY MWANJELWA AUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA AHAMASISHA KUJITOKEZA KWA WINGI AMANI IMETAWALA
- Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu
- MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”
- “Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo
- Nilivyomfanya Mtu Aliyenidharau Kuniheshimu na Kunitegemea Kwa Mambo Mengi
- NABII MPANJI AUTANGAZIA UMMA, WAKRISTO WASISHIRIKI MAANDAMANO WAJITOKEZE KWA WINGI KUPIGA KURA
- Nilivyookoa Biashara Yangu Baada ya Wateja Wote Kupotea Ghafla

