Mratibu wa Kambi ya Madktari bingwa wa rais samia kutoka wizara ya afya Bi. Jackline Ndeshau ameeleza kuwa wamejipanga kuhudumia wananchi wote watakaojitokeza kipindi cha siku 5 za kambi hii mkoani songwe katika maeneo 5 na kutoa rai kwa wananchi kujitokeza kutumia fursa hiyo ambapo lengo lake ni kusogeza huduma za afya karibu na jamii, kuongezea ujuzi wataalamu wa afya waliopo katika vituo husika vilevile kupunguza gharama za kwa wananchi kuzifwata huduma hizo za kibingwa nje ya kituo husika.
Amesema kambi ya madaktari bingwa na bobezi wa Rais Samia wanategemea kutoa huduma za afya kwa watoto na watoto wachanga, huduma za upasuaji, huduma za afya ya uzazi, wajawazito na magonjwa ya wanawake, huduma za ganzi na usingizi na huduma ya magonjwa ya ndani mkoani songwe kwa siku tano katika hospitali za wilaya ya Tunduma, Itumba, Vwawa, Momba na hospitali ya halmashauri wilaya ya Songwe
Trending
- TUME YAWAPIGA MSASA MAOFISA WA POLISI KUHUSU SHERIA ZA UCHAGUZI
- Haya tena Dkt. Tulia Huyoooo
- Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amehudhuria hafla ya kuadhimisha miaka 135 ya Bunge la Hungary,
- Sierra Leone wafika Ludewa kujifunza kwa TARURA matengenezo ya barabara
- Wananchi walia na gharama kubwa ya matibabu Wajawazito watozwa Fedha Hospitali ya wilaya Chunya
- RAIS SAMIA ANATAKA TUONGEZE MAPATO YA UTALII- WAZIRI CHANA
- TRA WAMLIZA MBUNGE MASACHE
- FULL VIDEO : MKUTANO MKUU WA 149 WA IPU UKIONGOZWA NA DKT. TULIA