Mratibu wa Kambi ya Madktari bingwa wa rais samia kutoka wizara ya afya Bi. Jackline Ndeshau ameeleza kuwa wamejipanga kuhudumia wananchi wote watakaojitokeza kipindi cha siku 5 za kambi hii mkoani songwe katika maeneo 5 na kutoa rai kwa wananchi kujitokeza kutumia fursa hiyo ambapo lengo lake ni kusogeza huduma za afya karibu na jamii, kuongezea ujuzi wataalamu wa afya waliopo katika vituo husika vilevile kupunguza gharama za kwa wananchi kuzifwata huduma hizo za kibingwa nje ya kituo husika.
Amesema kambi ya madaktari bingwa na bobezi wa Rais Samia wanategemea kutoa huduma za afya kwa watoto na watoto wachanga, huduma za upasuaji, huduma za afya ya uzazi, wajawazito na magonjwa ya wanawake, huduma za ganzi na usingizi na huduma ya magonjwa ya ndani mkoani songwe kwa siku tano katika hospitali za wilaya ya Tunduma, Itumba, Vwawa, Momba na hospitali ya halmashauri wilaya ya Songwe
Trending
- Hii ndiyo Shule ya Sekondari Mbeya DAY!! inazidi kung’ara
- Viziwi waipongeza Serikali huduma za Afya, waomba alama itakayowatambulisha katika usafiri
- KAILIMA: WENGI WAJITOKEZA KUBORESHA AU KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTARIO LA KUDUMU LA WAPIGA KURA
- Bodi ya TASAC yaridhishwa utekelezaji wa maagizo kwa TPA
- TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM (2020-2025) MBUNGE VITI MAALUM MKOA WA MBEYA – MH. MAHUNDI
- Tulia Traditional Dances Festival 2024 Kurundima Mkoani Mbeya
- Uvumi kifo cha Muimbaji wa Injili Bonny Mwaitege Wazazi Waiomba Serikali kuchukua hatua
- Mtoto adaiwa kumuua baba yake mzazi kwa shambulio la mwili