Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Dkt. Tulia: Michezo Ni Fursa ya Ajira kwa Vijana

September 5, 2025

Mwantona: Mama Samia Ni Shujaa wa Wakulima, Tumpe Kura za Historia

September 5, 2025

Nilijaribu Kuacha Ulevi Kwa Miaka 10 Lakini Siku Nilipopata Dawa Nilifunga Pombe Milele

September 5, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Dkt. Tulia: Michezo Ni Fursa ya Ajira kwa Vijana
  • Mwantona: Mama Samia Ni Shujaa wa Wakulima, Tumpe Kura za Historia
  • Nilijaribu Kuacha Ulevi Kwa Miaka 10 Lakini Siku Nilipopata Dawa Nilifunga Pombe Milele
  • ahati Ndingo: “Historia ya Dkt. Samia Wana Mbarali Tutaandika kwa Wino wa Dhahabu”
  • “Suma Fyandomo: Dkt. Samia Ni Dhahabu, Lulu na Tunu Ya Taifa Letu” tumpe kura za kishindo
  • Kwa Mara ya Kwanza, Patali S. Patali Atikisa Jukwaa kwa Kumwombea Kura Samia
  • Sophia Mwakagenda: Dkt. Samia Ameonyesha Uwezo wa Mwanamke Kuongoza Taifa
  • Fyandomo Ampongeza Dkt. Samia Miradi Mikubwa Mbeya Ni Ushahidi kura zote ni kwako
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LINDI, MTWARA, RUVUMA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI
Habari za Kitaifa

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LINDI, MTWARA, RUVUMA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJanuary 19, 2025Updated:January 19, 2025No Comments0 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu, Asina Omari akizungumza hii leo Januari 18, 2025 wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ngazi ya mkoa, mkoani Lindi ambapo amewataka watendaji hao  kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni, maelekezo na miongozo itakayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.  Dkt. Zakia Mohamed Abubakar akizungumza hii leo Januari 18, 2025 wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ngazi ya mkoa, mkoani Mtwara ambapo amewahimiza watendaji hao kuhakikisha wanahamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao.

 

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Magdalena Rwebangira akizungumza hii leo Januari 18, 2025 wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ngazi ya mkoa, mkoani Ruvuma kwa Watendaji wa Halmashauri za Madaba, Namtumbo na Tunduru ambapo amewataka kuwa makini katika kila eneo la usambazaji na utunzaji wa vifaa, mafunzo yote na muda sahihi wa ufunguaji na ufungaji wa vituo vya kuandikishia wapiga kura.
*******
Na. Mwandishi Wetu
Watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu
la Wapiga Kura katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma wametakiwa kutekeleza
majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni, maelekezo na miongozo itakayotolewa
na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
 
Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Tume ambaye
pia ni Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Asina Omar leo tarehe 18 Januari, 2025 wakati
akifunga mafunzo ya watendaji wa uboreshaji wa Daftari ngazi ya mkoa, Mkoani Lindi
ikiwa ni maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
 
“mnapaswa kutekeleza majukumu mliyopewa kwa
kuzingatia sheria, kanuni, maelekezo na miongozo itakayotolewa na Tume,”
amesema Jaji Asina.
 
Amewaasa watendaji hao kutambua uzito na
umuhimu wa zoezi la uboreshaji wa Daftari na kwamba elimu na ujuzi walioupata
vitawasaidia kutekeleza kwa nadharia na vitendo yale yote waliyofundishwa.
 
“Mnapaswa kutambua uzito na umuhimu wa zoezi
hili la kitaifa na kwamba baada ya ninyi kufundishwa na kuelekezwa ipasavyo
katika mafunzo haya, elimu na ujuzi mliopata vitawasaidia kutekeleza kwa
nadharia na vitendo yale yote mliyofundishwa,” amesema.
 
Akifunga mafunzo kama hayo mkaoni Mtwara,
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.
Dkt. Zakia Mohamed Abubakar amewahimiza watendaji hao kuhakikisha wanahamasisha
wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba
itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao.
 
“Ni matarajio ya Tume kuwa, mara baada ya
zoezi hili kukamilika watu watakaokuwa wamepatiwa kadi watakuwa ni wapiga kura
halali.
 
 Jukumu
la uhamasishaji linawahusu moja kwa moja ninyi watendaji, kwa kushirikiana na
wadau wengine katika maeneo yenu kupitia nyenzo mlizo nazo,” amesema Mhe.
Zakia.
 
Mkoani Ruvuma mafunzo hayo yamefungwa na
Mjumbe wa Tume, Mhe. Magdalena Rwebangira ambaye aliwakumbusha watendaji hao
kuwa makini katika kila eneo la usambazaji na utunzaji wa vifaa, mafunzo yote
na muda sahihi wa ufunguaji na ufungaji wa vituo vya kuandikishia wapiga kura.
 

Mafunzo hayo yamefanyika
ikiwa ni maandalizi ya uboreshaji wa Daftari mkoani Mtwara, Lindi na mkoa wa Ruvuma
kwenye Halmashauri za Wilaya ya Madaba, Namtumbo na Tunduri  ambapo uboreshaji utafanyika kwa siku saba
kuanzia tarehe 28 Januari, 2025 hadi tarehe 03 Februari, 2025 na vituo
vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.

 

Mwenyekiti wa Mafunzo Mkoani Mtwara, Ndg. George Mbogo akizungumza.

 

 
Meza kuu Mkoani Lindi 

 

Watendaji mkoani Mtwara wakifuatilia hotuba ya kufunga mafunzo.

 

Mafunzo kwa vitendo mkoani Mtwara

 

 

Watendaji Mkoani Ruvuma wakimsikiliza mgeni rasmi akifunga mafunzo hayo. 

 

Watendaji Mkoani Lindi wakimsikiliza mgeni rasmi akifunga mafunzo hayo. 

 

 

Watendaji Mkoani Lindi wakifanya mafunzo kwa vitendo.

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TUME YATOA MWALIKO KWA WAANDISHI WA HABARI WENYE NIA YA KURIPOTI MATUKIO WAKATI WA UCHAGUZI

September 3, 2025

Mbeya Yatikisika! Dkt. Tulia Achukua Fomu Ubunge Jimbo Jipya la Uyole

August 25, 2025

TAKUKURU Mbeya Yaokoa Milioni 47 na Kuongeza Mapato ya Halmashauri Zaidi ya Milioni 200

August 19, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025206

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025123

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025102
Don't Miss
Video Mpya

Dkt. Tulia: Michezo Ni Fursa ya Ajira kwa Vijana

By Mbeya YetuSeptember 5, 20250

Mbeya, Septemba 5, 2025 — Spika wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson, ametoa wito kwa vijana nchini kutumia michezo, hususan mpira wa miguu, kama njia ya kujipatia ajira na kuboresha maisha yao.

Dkt. Tulia alitoa kauli hiyo leo wakati wa tamati ya mashindano ya Tulia Trust Uyole Super Cup yaliyofanyika mkoani Mbeya, ambapo alikuwa mgeni rasmi.

Amesema michezo ni sekta yenye fursa nyingi, ikiwemo ajira, na hivyo vijana wanapaswa kujituma, kuwa na nidhamu, na kuendeleza vipaji vyao ili kufanikisha malengo yao.

Aidha, Dkt. Tulia amethibitisha kuwa taasisi yake ya Tulia Trust itaendelea kudhamini mashindano hayo kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo, kwa lengo la kuibua na kukuza vipaji vya vijana pamoja na kuendeleza michezo nchini.

Mwantona: Mama Samia Ni Shujaa wa Wakulima, Tumpe Kura za Historia

September 5, 2025

Nilijaribu Kuacha Ulevi Kwa Miaka 10 Lakini Siku Nilipopata Dawa Nilifunga Pombe Milele

September 5, 2025

ahati Ndingo: “Historia ya Dkt. Samia Wana Mbarali Tutaandika kwa Wino wa Dhahabu”

September 5, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Dkt. Tulia: Michezo Ni Fursa ya Ajira kwa Vijana

September 5, 2025

Mwantona: Mama Samia Ni Shujaa wa Wakulima, Tumpe Kura za Historia

September 5, 2025

Nilijaribu Kuacha Ulevi Kwa Miaka 10 Lakini Siku Nilipopata Dawa Nilifunga Pombe Milele

September 5, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025206

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025123
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.