Sharif Abdul Afisa Mwandamizi kitengo cha mahusiano Jamii na ujirani mwema hifadhi ya Taifa Ruaha amesema kupitia mradi wa REGROW wameandaa Muongozo rafiki wa kupokea na kushughulikia malalamiko kutoka kwa wananchi wanaozunguka hifadhi.
Amesema kupitia mradi wa REGROW viongozi na kamati za kushughulikia malalamiko kuanzia ngazi ya Kijiji mpaka mkoa wamejengewa uwezo kwa kupewa elimu namna ya kutumia muongozo huo ili kupokea na kushughulikia malalamiko ya wananchi. Lengo nikuhakikisha wananchi wanaoathirika na shughuli za hifadhi au Mradi wa REGROW wanawasilisha malalamiko yao na yanashughulikiwa kwa utaratibu unaofahamika.
Aidha Abdul amewasihi wananchi wenye malalamiko wafike ofisi za Serikali ya Kijiji nakuwasilisha malalamiko yao au wapige simu ya bure moja kwa moja kwa Hifadhi ya Taifa Ruaha namba 0800110801 na Wizara ya Maliasili na Utalii namba 0800110804 endapo lalamiko linahusu Hifadhi au Mradi wa REGROW. Malalamiko yote yatashughulikiwa kwa usiri na mlalamikaji atalindwa na sheria na tararibu za nchi.
Trending
- *TANI ZA MBOLEA ZAMWAGWA MBEYA RC HOMERA NA SILINDE WATOA YA MOYONI*
- REGROW Yatoa Muongozo Mpya wa Kupokea na Kushughulikia Malalamiko ya Wananchi Wanaozunguka Hifadhi
- Mh Mahundi Aanza Ujenzi wa Nyumba ya Katibu wa UWT Mkoa wa Mbeya Kwa Gharama ya Zaidi ya Milioni 70
- Jinsi ya Kufikisha Malalamiko Kuhusu Mradi wa REGROW na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha
- Serikali yagawa vishikwambi 350 kwa maafisa ugani Mkoani Mbeya
- RC. Homera azindua zahanati ya Sinai Kata ya Iwambi Jijini Mbeya
- MHE. MHESHIMIWA MHANDISI MAHUNDI AHITIMISHA ZIARA YA SIKU 3 KUTEMBELEA WATOA HUDUMA ZA MAWASILIANO
- MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA KERO NA KUPOKEA USHAURI KWA WATEJA WA MBEYA WSSA