Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025

MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”

October 27, 2025

“Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo

October 27, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu
  • MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”
  • “Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo
  • Nilivyomfanya Mtu Aliyenidharau Kuniheshimu na Kunitegemea Kwa Mambo Mengi
  • NABII MPANJI AUTANGAZIA UMMA, WAKRISTO WASISHIRIKI MAANDAMANO WAJITOKEZE KWA WINGI KUPIGA KURA
  • Nilivyookoa Biashara Yangu Baada ya Wateja Wote Kupotea Ghafla
  • DED Yegella: Ahamasisha Upigaji Kura, Kamanda Kuzaga Asema Jeshi la Polisi Lipo Tayari Kulinda Amani
  • RC Malisa Atoa Wito wa Kulipa Leseni Wakati Akikabidhi Madawati 1,000 kwa Shule 15 Jijini Mbeya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TUME YA UCHAGUZI YAPONGEZWA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU 2025
Uncategorized

TUME YA UCHAGUZI YAPONGEZWA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU 2025

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJune 9, 2025No Comments13 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kilichokutana Mjini Unguja Zanzibar leo Juni 9,2025.

 
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume akizungumza mapema kabla ya ufunguzi wa kikao hicho.

 

 

 

 

 

Wajumbe wa Baraza hilo wakifuatilia mada katika Mkutano huo.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume, Ramadhani Kailima,  wakati Katibu Mkuu huyo alipofika kufungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Mjini Unguja, Zanzibar leo Juni 9,2025.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz (kushoto)  na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume, Ramadhani Kailima,  pamoja na wajumbe wa baraza la Wafanyakazi la Tume wakiimba wimbo wa wafanyakazi wakati kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Wafanyakazi  Mjini Unguja, Zanzibar leo Juni 9,2025. 

Na. Mwandishi Wetu, Zanzibar

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge
na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz ameipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa
kukamilisha zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na
kuendelea vyema na maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Dkt. Yonazi ametoa pongezi hizo leo tarehe 09
Juni, 2025 Kisiwani Unguja, Zanzibar wakati wa kufungua kikao cha Baraza la
Wafanyakazi la INEC,  ambapo imewaasa
viongozi wa Tume kuendelea kuwa imara na kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano
ili kuhakikisha kuwa uchaguzi unakwenda vizuri.

“Kwanza niwapongeze sana kwa kukutekeleza
jukumu hili kubwa ambalo mmekabidhiwa na Taifa letu na kwa namna ya pekee
kabisa Mwenyekiti wa Baraza unifikishie salamu za pongezi kwa Mwenyekiti wa
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele pamoja na
wajumbe wa Tume kwa kazi kubwa ambayo mmeifanya katika kuhakikisha kuwa
shughuli za uchaguzi nchini kwetu zinakwenda vizuri,” amesema Dkt. Yonazi.

Ameeleza kuridhishwa na jinsi Tume ilivyotekeleza
kwa ufanisi zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuongeza
kuwa ni matarajio ya Serikali kuwa utendaji huo mzuri wa Tume utaendelea kwa
viwango vya juu kwa mujibu wa katiba, sheria na taratibu mbalimbali ambazo zimewekwa.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti
wa Baraza la Wafanyakazi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya
Taifa ya Uchaguzi, Ndugu. Kailima Ramadhan amesema tayari Tume imekamilisha
awamu ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambapo kwa
sasa inaendelea na uboreshaji wa awamu ya pili.

“Tume imeshakamilisha uboreshaji wa awamu ya
kwanza na imeshachakata na kutoa daftari la awali na imeshakamilisha uboreshaji
wa awamu ya pili mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili. Tunategemea kuanzia
tarehe 28 mwezi huu (tarehe 28 Juni, 2025) tutaanza mzunguko wa tatu wa
uboreshaji katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar na Magereza Tanzania Bara
kwa wanafunzi na wafungwa waliohukumiwa kifungo chini ya miezi sita,” amesema
Kailima.

Katibu huyo wa Baraza amesema mzunguko huo wa
tatu utahusisha vituo 140 vya kuandikisha wapiga kura ambapo 130 vipo kwenye
magereza Tanzania Bara na vituo 10 vipo kwenye vyuo vya mafunzo Tanzania
Zanzibar. Zoezi hilo linatarajiwa kufanyika kwa siku saba hadi tarehe 04 Julai,
2025.

Ameongeza kuwa Tume imekamilisha maandalizi
ya nyaraka mbalimbli kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni pamoja
na Kanuni za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025, Kanuni za
Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025 na maelekezo
mbalimbali kwa ajili ya watendaji wa uchaguzi na wadau wa uchaguzi kupata
miongozo kwa ajili ya utekelezaji wa uchaguzi.

Alimkumbusha mgeni rasmi kuwa tayari Tume
imekamilisha zoezi la ugawaji wa majimbo na kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa
mwaka 2025 kutakuwa na jumla ya majimbo 272 yatakayofanya uchaguzi wa wabunge
katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kata 3960 kwa ajili ya uchaguzi wa
madiwani kwa Tanzania Bara.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025

Nilivyomfanya Mtu Aliyenidharau Kuniheshimu na Kunitegemea Kwa Mambo Mengi

October 27, 2025

Nilivyookoa Biashara Yangu Baada ya Wateja Wote Kupotea Ghafla

October 26, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025200

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025126
Don't Miss

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

By Mbeya YetuOctober 27, 20251

Ndoa yangu ilifika hatua ya kutisha. Kila usiku tulikuwa tukilumbana kuhusu kitu kipya, hasa pesa…

MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”

October 27, 2025

“Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo

October 27, 2025

Nilivyomfanya Mtu Aliyenidharau Kuniheshimu na Kunitegemea Kwa Mambo Mengi

October 27, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025

MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”

October 27, 2025

“Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo

October 27, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025200

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.