Taasisi ya Tulia Trust iliyo chini ya Mbunge wa jimbo la Uyole jijini Mbeya Dkt Tulia Ackson, wameanza ujenzi wa nyumba ya famikia ya mzee Anyomwisye Mwalyaje mkazi wa mtaa wa Mwafute kata ya Ilemi iliyoteketea kwa moto usiku wa September 5 kutokana na hitilafu kwenye mfumo wa Umeme.
Ujenzi huo umeanza baada ya Mbunge wa jimbo la Uyole kutoa ahadi ya kumjengea nyumba mzee Anyomwisye Mwalyaje alipomtembelea kutokana na kadhia ya nyumba yake kuteketea kwa moto pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani.
Afisa kutoka taasisi ya Tulia Trust kitendo cha habari Addi Kalinjila amesema ujenzi wa nyumba hiyo unaanza maramoja baada ya vifaa kufika eneo la ujenzi ili kurejesha maisha ya familia hiyo kama yalivyokua hapo awali.

