KAULI MPYA KUTOKA CCM KYELA,FEDHA ZIMETOKA AU ZIMEUNGUA ,UCHUNGUZI UNAENDELEA.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya Bw.Elias Mwanjala amejitokeza hadhara kwa mara nyingine na kutoa kauli juu ya fedha ambazo alidai kuwa zimeteketea kwa moto wakati jengo la chama hicho lilipochomwa.
Bw.Mwanjala amesema kuwa ukweli wa fedha hizo kama zimeteketea kwa moto au kuchukuliwa na yeyote wameliachia vyombo vya ulinzi na usalama liendelee na uchunguzi.

