Author: admin

Siku ya Kimondo ambayo imefanyika kwa mara ya kwanza katika kijiji cha Ndolezi wilayani Mbozi mkoa mpya wa Songwe umeonesha kila dalili ya kutoa fursa ya Utalii na Uwekezaji kutokana na Wajasiriamali wengi kujitokeza katika siku hiyo.

Kimondo cha Mbozi ni nyota inayosadikiwa kudondoka miaka mingi kutoka sayari ya juu ambapo uwepo wa Kimondo hicho adimu duniani kimekuwa ni moja katika vivutio vichache vya aina yake vya Utalii nchini na duniani kwa ujumla.

Read More