Author: Mbeya Yetu

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi amejumuika pamoja na waombolezaji wengine, kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Tixon Nzunda, shughuli iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Goba jijini Dar Es Salaam.Balozi Dk Nchimbi, ambaye alisoma pamoja na marehemu Nzunda Chuo Kikuu Mzumbe, pia aliwapatia pole familia ya marehemu kwa msiba huo, baada ya kusaini kitabu cha maombolezo. Mwili wa marehemu Nzunda, ambaye alifariki kwa ajali ya gari Juni 18, 2024 huko wilayani Hai, unatarajiwa kuzikwa nyumbani kwao, mkoani Songwe, Juni 22, 2024. @ccmtanzania @nchimbie

Read More

Serikali imesema uanzishwaji maeneo ya utawala katika Mamlaka za Serikali za Mitaa hufanyika kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) sura ya 287 na (Mamlaka za Miji) sura ya 288 pamoja na mwongozo wa uanzishwaji wa maeneo ya Utawala wa mwaka 2014. Hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Zainab Katimba, alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa jimbo la Mbeya Vijijini Mhe. Oran Njeza aliyeuliza ni lini Serikali itarekebisha mipaka ya vijiji vya Kata ya Utengule Usongwe ikiwemo Kijiji cha Mbalizi ambacho hakiungani kabisa na Vijiji vingine. “Kwa…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi wa mkoa wa Kigoma uliofanyika leo tarehe 19 Juni, 2024 katika Halmashauri ya Kigoma Ujiji. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi wa mkoa wa Kigoma uliofanyika leo tarehe 19 Juni, 2024 katika Halmashauri ya Kigoma Ujiji. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K akizungumza wakati akiwasilisha mada ambapo alisema amesema uboreshaji kwa awamu hii ya kwanza…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume na wahariri wa vyombo vya Habari kuhusu  maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura uliofanyika leo tarehe 12 Juni, 2024 mkoani Dar es Salaam.  ***** Na. Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewaasa wahariri wa vyombo vya habari kuwahabarisha na kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa Tume na wahariri wa vyombo vya…

Read More