Author: Mbeya Yetu

JUMIKITA (Jumuiya ya Mitandao ya Kijamii Tanzania) kwa kushirikiana na TAHLISO (Shirikisho la Serikali za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania) inaandaa Kongamano la Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii nchini litakalofanyika tarehe 20/5/2024 kwenye ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam. JUMIKITA inapenda kuutaarifu umma kuwa, Kongamano hilo litakuwa na dhima kuu ya kujadili undishi wa habari kupitia mitandao ya kijamiii pamoja na upashanaji wa habari kupitia mitandao hiyo. Pamoja na dhima hiyo kuu, Kongamano hilo litajadili mafanikio ya miaka mitatu ya serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ikia ni pamoja na maadhimisho ya siku ya uhuru wa…

Read More

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Rufaa imetengua hukumu iliyotolewa na Mahakama kuu divisheni ya biashara katika moja ya kesi maarufu za mikopo chechefu baina ya kampuni ya State Oil dhidi ya Benki ya Equity kesi ambayo Mahakama Kuu hiyo chini ya Jaji Magoiga iliipa ushindi kampuni ya husika ambayo ilikopa dola milioni 18 (zaidi ya Shilingi Bilioni 45 za kitanzania) na kukataa kulipa kisha kukimbilia mahakamani Ikiongozwa na majaji watatu Rehema Mkuye, Abraham Mwampashi na Zainab Muruke mahakama hiyo imeona kasoro kadhaa za kiuendeshaji wa kesi katika mahakama kuu divisheni ya biashara iliyofunguliwa na kampuni ya State Oil ikitaka mahakama…

Read More

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K akifanya mahojiano kwenye kipindi cha Jambo kinachorushwa na TBC1 jijini Dar es Salaam leo tarehe 17 Mei, 2024 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K akifafanua jambo wakati wa mahojiano kwenye kipindi cha by Jambo kinachorushwa na TBC1 jijini Dar es Salaam leo tarehe 17 Mei, 2024. Kulia ni mtangazaji wa kipindi hicho, Janeth Leornard na Rajab Rajab. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K akifafanua jambo wakati…

Read More

Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha leo Mei 16, 2024 limepokea msaada wa pikipiki 20 toka benki ya CRDB kwa ajili ya kuimarisha usalama wa raia na mali zao katika Mkoa huo. Akikabidhi pikipiki hizo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe; Paul Makonda amesema pikipiki hizo zimetolewa kwa Jeshi la Polisi ikiwa ni utekelezaji wa sehemu ya ahadi yake aliyoitoa hivi karibuni ya kutoa pikipiki hamsini kwa Jeshi la Polisi kwa ajili ya kuimarisha usalama katika Jiji la Arusha hasa kwa kuzingatia ni kitovu cha Utalii hapa Nchini. Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa mbali na kutolewa kwa pikipiki hizo…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele akizungumza na waandishi wa habari Mjini Unguja, Zanzibar, leo tarehe 15 Mei, 2024, ambapo ametangaza kuwa uzinduzi wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utafanyika tarehe 01 Julai, 2024. (Picha na INEC). Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele (katikati) akizungumza na waandishi wa habari Mjini Unguja, Zanzibar, leo tarehe 15 Mei, 2024, ambapo ametangaza kuwa uzinduzi wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utafanyika tarehe 01 Julai, 2024. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Bw.…

Read More